Sunday, September 1, 2013

MAKUYU MAGAI---NILIACHA WIZI BAADA YA KUHUBILIWA GEREZANI.


-Aliamua kwenda kujisalimisha polisi baada ya kutoka gerezani.
Na Berensi Alikadi.
1.9.2013
MAKUYU Magai ni mkazi wa mtaa wa Nyakato katika manispaa ya Musoma,alizaliwa mwaka 1973 huko katika kijiji cha Murangi wilaya ya Butiama mkoani Mara.
Baada ya kuhitimu masomo yake ya kidato cha nne katika shule ya sekondari Somanya  iliyoko katika kijiji cha Mugango wilaya hiyo ya Butiama mwaka 1993 aliamua kufanya shughuli mbalimbali za ujasiliamali baada ya matokeo yake kutokuwa mazuri hivyo kushindwa kuendelea na masomo ya juu.
Mnamo mwaka 1996 aliamua kwenda mjini Musoma na kuweka makazi yake mtaa wa nyakato maziwa ambapo aliamua kuanzisha ukumbi wa kuonyesha picha ambayo ndiyo shughuli ambayo ilikuwa ikimpatia kipato.
Magai anasema akiwa katika shughuli hiyo alishawishiwa na baadhi ya wezi ambao walikuwa wakiiba vitu mbalimbali na kumuuzia  kazi ambayo aliianza mwaka 2000.
Anasema baada ya kuendelea na shughuli hiyo hatimaye aliangukia kwenye mikono ya dora baada ya wezi waliokuwa wakiiba kukamatwa na kumtaja yeye kuwa ndiye alikuwa wakala mkubwa wa kununua vitu vya wizi ambapo alikamatwa mwaka huohuo wa 2000 na kupelekwa polisi ambako aliandaliwa mshitaka na kupelekwa mahabusu.
Baada ya kupelekwa gerezani na kuwasimulia wenzake kilichompeleka humo alipata waalimu ambao walimufundisha namna ya kuiba vitu vikubwa na namna gani ya kijihami na kumshauri aachane na kununua vitu vya wizi.
Baada ya kushawishiwa nililianza kufanya matukio mbalimbali ingawa  ingawa sikuweza kukamatwa na kesi hizo,mfano niliwahi kwenda kwenye duka la kituo cha mafuta na kumshawishi mlinzi aache kazi na kwamba nitampeleka sehemu nyingine ili aweze kupata kazi nzuri.

Siku iliyofuata nilienda kumtembelea mlinzi huyo na kumkuta amelala kesho yake tulienda na wenzangu usiku tukafungua tukaiba simu zote,matukio yangu yalikuwa ya kwenda kuwashawishi walinzi na kuwapa pesa ili sisi usiku tukaibe na kwa hili nataka nikwambie hakuna mlinzi ambaye siyo mwizi.
Makuyu anaeleza kuwa walipokuwa wakitoa vitu vya wizi mlinzi pia alikuwa akipata mgawo wake na kwamba kitendo cha kufungua duka na kuhamisha bidhaa kilikuwa ni cha muda mfupi sana.
Bidhaa tulizokuwa tukiiba tulikuwa tukienda kuwauzia wenye maduka na pia fahamu kuwa hata hawa wafanya biashara wa maduka ni wezi hili nalithibitisha hata kama nikiambiwa kutoa ushuhuda nitatoa ndiyo maana tulikuwa hatupati shida ya kuuza vitu vyetu vya wizi.
Makuyu anasema akiwa gerezani alifanikiwa kudhaminiwa lakini licha ya kupata dhamana hakuweza kukaa uraiani kwa amani kwani kila tukio baya la wizi lilipokuwa likitokea polisi walienda kumkamata hali ambayo ilimyima amani.
Mnamo tarehe 26/12/2009 alimpiga mtu mmoja ambaye aliwahi kumtukana na kisha akakimbilia Mwanza na kwamba siku hiyo walipokutana alimua kumpiga  na mtu huyo alikwenda kuripoti kituo cha polisi na kesho yake polisi walikwenda kumkamata na walipomfikisha kituoni  kama kawaida yao walimbambikiza kesi ya unyanga’nyi  wa kutumia silaha na kupatikana na bangi.
Niliendelea na kesi hiyo ambayo ilikuwa chini ya hakimu Richard Maganga lakini baada ya kuona haiendi vizuri niliandika barua ya kumtaka ajiondoe katika kesi hiyo lakini alikataa  na tarehe mwezi wa nane mwaka 2010.
Anasema ilipofika mwezi wa tisa tarehe 9 mwaka huohuo hakimu huyo alimufunga tena kifungo cha miaka 30 jera na kuchapwa viboko 24 kwa kosa la unyanga’nyi hata hivyo sikuridhika na hukumu hiyo ambapo nilikata rufaa ambayo ilinitoa mnamo tarehe 31 mwezi wa tano mwaka huu.
Makuyu anaeleza kuwa baada ya baada ya kuhukumiwa na Maganga alipelekwa katika gereza la Butimba jijini Mwanza na kwamba akiwa huko alijifunza mambo mengi na aliona mambo mwengi ambayo yalimusukuma kabisa kuacha wizi.
Kwakweli baada ya kurudi niliamua kwenda polisi tarehe 21.8.2013 na kuonana na mkuu wa upelelezi wa wilaya ambapo nilimuambia kuwa kuanzia sasa mimi ni raia mwema na pia nimeamua kuwatafuta nyie waandishi ili mfikishe taarifa hizi kwa jamii kuwa mimi siyo mwizi tena,
Niliamua mwenyewe kwenda polisi kujisalimisha na kwa hili sina shaka maana naamini mungu ananilinda maana hata kesi yangu nilishinda kwa nguvu zake maana hata wakili wa serikali aliyekuwa ananitetea alisema hawahi kuona kesi kama yangu,yaani mtu unafungwa mara mbili kwa mwezi mmoja.pasipo hata kujitetea.
Natoa wito kwa vijana wa nchi hii wabadirike kama nilivyobadirika mimi nimejionea mambo mengi gerezani,mfano vijana wa Musoma waache vikundi walivyonavyo kama vile Jamaica mokazi,midomo ya furu na uchakavu na watambue kuwa gereza siyo mahali pa kuishi na unapotoka gerezani hukai kwa amani kutokana na jamii kutokuamini.
Makuyu anabainisha wenzake waliokuwa wakifanya nao kazi hiyo ambao wameshauwawa kuwa ni pamoja na  Sauri Magembe Bwire maalufu kwa jina la Bebeto.Devis Manyama,Jumanne Mjungu na Stivin Wiliam ambao wote kwa hivi sasa ni marehemu na walikufa kwa kupigwa na wananchi
Lakini pia anamuomba rais Kikwete asitoe msamaha kwa wafungwa wa miaka mitano na kurudi chini kwani hao wanakuwa hawajifunza kitu chochote na ndio maana wakiachiwa huanza tena vitendo vya uharifu.
Huyo ndiye Makuyu Magai aliyeamua kijisalimisha polisi baada ya kutoka gerezani.
MWISHO.

No comments:

Post a Comment

Comments System

disqus

Disqus Shortname

msora

Popular Posts

Header Ads

ad