Tuesday, September 19, 2017

NGO'MBE 345 WAPIGWA MNADA MEATU



Na Berensichina,sept 17,2017,ngombe 345 wapigwa mnada,
hakimu mkazi mwandamizi mfawidhi wa mahakama ya mkoa wa simiyu john nkwabi ameamuru kutaifishwa na kipigwa mnada jumla ya  ngombe 345 waliokamatwa wakichunga katika pori la akiba la maswa kinyume cha sheria ya wanyamapori
akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mnada huo uliofanyika wilayani meatu meneja wa pori la akiba la maswa lusato masinde amesema wameamua kuuza mifugo hiyo baada ya mahakama kutoa  amri kulingana na sheria ya wanyama pori namba 5,2009 kifungu cha 111.
aidha meneja huyo amewaonya wafugaji ambao watakaidi agizo la mhe.rais la kuondoa mifugo yao kwa hiyari na kuacha kuchungia katika pori hilo  kwani msako wa kukamata mifugo hiyo ni endelevu na mifugo itakayokamatwa itaendelea kutaifishwa kwa mjibu wa sheria
kwa upande wake darali aliyesimamia zoezi la kuuza ngo’mbe hao kutoka kampuni ya abajaja christopher kabenga amewataka wanunuzi wote kuhakikisha wanatembea na stakabadhi halisi waliyopewa wakati watakapo kuwa wanasafirisha mifugo hiyo ili kuepuka usumbufu njianii

No comments:

Post a Comment

Comments System

disqus

Disqus Shortname

msora

Popular Posts

Header Ads

ad