Sunday, September 30, 2012

MBUNGE AWATAKA WATOTO WA KIKE KUSOMA KWA BIDII



NA Berensi Alikadi-Bunda

IMEELEZWA Kuwa  njia pekee ya kumsaidia mtoto wa kike ni kumpa elimu bora itakayomsaidia katika maisha yake ya baadaye na wala sivinginevyo.

Kauri hiyo imetolewa jana mjini Bunda na mbunge wa viti maalumu kundi la vijana wa chama cha mapinduzi mkoa wa Mara Ester Bulaya  wakati alipokuwa akiongea na wazazi na wanafunzi kwenye mahafali ya kwanza ya shule ya waschana ya Mkwezi iliyopo mjini Bunda.

Alisema kuwa mtoto wa kike anayonafasi kubwa ya kufanya vizuri kielimu kama ataendelezwa ipasavyo na kwamba ile dhana ya kumbeza mtoto wa kike kwa kutompa elimu sasa imepitwa na wakati.

Mbunge huyo aliwataka wazazi wa watoto hao waliohitimu kidato cha nne kuwasadia zaidi watoto hao ili waweze kuendelea na masomo ya vidato vya juu ambayo yawasaidia kuingia katika soko la ajira hapa nchini na nje ya nchi.

‘’Ndugu zangu wazazi watoto hawa sasa ndio wameanza hatua kubwa maana hii hatua waliyomaliza naweza kusema ni kama nusu hivyo wasaidieni ili waweze kufikia malengo ya maisha yao nina imani wanandoto nzuri ya kufika kileleni sasa tuwawezeshe ili wafaulu.’’alisema Bulaya.

Mbunge huyo alikubali kumsomesha mwanafunzi Penina Wayoga hadi kidato cha sita baada ya kupata vyeti sita ambavyo amefanya vizuri katika masomo ya hesabu,Fizikia,Sayansi uraia Jografia na bailogia ambapo aliibuka kidedea kwa kupewa vyeti sita.

Awali wakisoma risala ya kuhitimu masomo yao wanafunzi hao walisema kuwa walianza  masomo shuleni hapo  mwaka 2009 wakiwa wanafunzi 24 na sasa wamehitimu wakiwa 41 ambapo  sanaa wanafunzi 20na sayansi ni wanafunzi 21.

Walisema kwa muda wote waliosoma shuleni hapo wameweza kupata mafanikio mbalimbali ikiwa ni pamoja na shule hiyo kushika nafasi ya 4 kati ya shule 29 kimkoa,na shule kushika nafasi ya 36 kati ya shule 432 kikanda ambapo pia katika mtihani wa utimilifu walishika nafasi ya kumi kati ya shule 164 kimkoa.

Wanafunzi hao walibainisha kuwa pamoja na mafanikio hayo shule hiyo pia inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa maktaba,maabara jambo ambalo limechangia kudumaa kwa maendeleo ya elimu shuleni hapo.

Akisoma risala ya shule hiyo mkuu wa shule hiyo,Mwalimu Goodluck Muyenjwa alisema kuwa pamoja na shule hiyo kufanya vizuri lakini bado lipo tatizo la wazazi kutolipa ada kwa wakati jambo ambalo limesababisha uongozi wa shule hiyo kuwatowalipa watumishi mishahara kwa wakati.

Muyenjwa alisema kuwa shule hiyo pia inakabiliwa na tatizo la ukosefu wa umeme jambo limewafanya wanafunzi wa shule hiyo washindwe kujisomea ipasavyo na kumuomba mbunge huyo aweze kulifikisha kwa wahusika ombi ambalo alilikubali.
MWISHO.

No comments:

Post a Comment

Comments System

disqus

Disqus Shortname

msora

Popular Posts

Header Ads

ad