NA Berensi
Alikadi Musoma.
20/7/2013
WAALIMU na
wanafunzi wa shule ya sekondari ya Bweri iliyoko katika manispaa ya Musoma
wamesema moshi mwingi unaotoka katika kiwanda cha nguo cha Mutex ni hatari kwa afya
yao na kwamba umekuwa ukiwapa wakati mgumu wa kufundisha shuleni hapo.
Waalimu hao
walitoa kilio chao hicho jana kwa mbunge wa jimbo la Musoma Vicent Nyerere kwa
tiketi ya Chadema wakati alipotembelea shule hiyo na kisha kuongea na waalimu
na wanafunzi.
Walisema
kuwa kwa muda mrefu sasa moshi mwingi unaotoka katika kiwanda hicho cha nguo
umekuwa ukiwaathiri wao pamoja na wanafunzi wakati wa masomo kwani umekuwa
ukiingia madarani jambo ambalo sasa limeonekana kuwa sugu na kwamba wao licha
ya kulalamika lakini hawaoni jitihada zozote zinazofanyika na uongozi wa
manispaa ili kuzuia moshi huo.
‘’Kwakweli
mbunge huu moshi unatuumiza sana sisi waalimu tunafundisha kwa shida na hata
watoto wetu wanasoma kwa shida sana leo kwa vile umetutembelea tunaomba tukueleze
kabisa kero hii ili uweze kuona namna ya kutusaidia’’alisema Mwalimu Madede
Pamoja na
kero hiyo pia waalimu hao walimwambia mbunge huyo kuwa kumekuwepo na tatizo la
vikundi vya Jamaica Mokas ambavyo vimekuwa ni tishio kwa waalimu na kwamba
imefikia hatua mpaka vinakuja shuleni hapo na kuvizia waalimu jambo ambalo ni
hatari kwao kwani shule yao haina uzio.
Aidha kero
nyingine waliyomwambia mbunge huyo ni pamoja na wao kunywa maji machafu ambayo
hayakuchujwa wala kuwekewa dawa na kwamba maji hayo yako kwenye eneo la mkondo
wa kiwanda cha nguo kinapomwaga maji machafu jambo ambalo walidai kuwa afya zao
ziko hatalini.
Akijibu hoja
hizo mbunge huyo alisema kuwa suala la kiwanda cha Mutex kutoa moshi ni hatari
ambapo aliahidi kwenda yeye mwenyewe kiwandani hapo ili aweze kuonana na
mhusika.
Kuhusu kero
ya maji aliwahakikishia waalimu hao kuwa atajitahidi kuonana na uongozi wa
Muwasa ili kufahamu ni kwa nini hawaweki dawa katika maji lakini pia akawapa
matumaini kuwa upo mradi mkubwa wa maji unaojengwa eneo la makoko na kwamba
unatarajia kukamilikwa mwakani ambapo wananchi wa Musoma sasa hawatakuwa tena
na shida ya maji.
Mbunge huyo
pia alitumia fursa hiyo kuwaasa wanafunzi wa shule hiyo kusoma kwa bidii na
kuachana na kujiunga na vikundi viovu kwani wazazi wao wanajitahidi kuwalipia
karo hivyo njia pekee ya kujinasua katika umasikini ni elimu na wala si jambo
linguine.
Akiwa katika
shule hiyo mbunge huyo pia aliweza kukagua jengo la maabara ya kisasa ambalo
limejengwa kwa gharama ya kiasi cha shilingi pesa ambayo imetokana na mfuko wa
jimbo.
Mwisho
No comments:
Post a Comment