Sunday, August 4, 2013

MME AUWA MKE KWA KUMYONGA NAYE AUWAWA



NA Berensi Alikadi,Bunda.
5/8/2013
WATU wawili wamefariki dunia juzi wilayani Bunda mkoani Mara katika matukio mawili tofauti likiwemo la mme kuuwa mke wake na kisha yeye pia kuuwawa.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo  lililotokea agost 2mwaka huu afisa mtendaji wa kata ya Mcharo Waziri kingialimtaja mwanamke mmoja aliyekuwa akifahamika kwa jina la Pamera Samson mkazi wa kijiji cha Kisangwa wilayani hapa alifariki dunia baada ya kunyongwa na mme wake.
Mashuhuda wa tukio hilo wameliambia Tanzania daima kuwa mwanamke huyo ambaye kwa sasa ni marehemu alikuwa ametengana na mme wake kutokana na matatizo ya ugomvi miezi miwili iliyopita na kwamba mme wake huyo aliyekuwa akifahamika kwa jina la Bature Masanja alikuwa amehamia katika kijiji cha Maliwanda kilichopo katika wilaya hiyo.
Imeelezwa kuwa siku ya tukio kulikuwa na sherehe nyumbani kwao  na mwanamke ya kufungua nyumba na kwamba mme wake huyo pia alifika hapo na kwamba wakiwa wanasherekea ndipo majira ya usiku alipomuomba mke wake watoke waende sehemu kwa madai kuwa alikuwa na mazungumzo naye.
Mashuhuda hao walifafanua kuwa baada ya kutoka naye walienda mbali kidogo na hapo nyumbani kwao na kwamba alipofika umbali fulani alimkamata mke wake wake huyo na kumbaka ambapo baadaye alimaliza akamnyonga.
‘’Jana yake asubuhi ndio mwili wake huyo mama ulionekana baada ya watu waliokuwa wakienda shambani kuukuta na ndipo walipotoa taarifa hizo lakini kwa kuwa watu walimuona anaondoka na huyo mme wake na kwa vile hakuweza kurudi tena pale ukweni kwakwe waliamini kuwa ndiye aliyefanya tukio hilo’’alisema mwalimu mmoja wa shule ya msingi Kisangwa ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini.
Alifafanua kuwa baada ya taarifa hizo kuenea kijijini hapo walipiga yowe na kuanza kumsaka mme wake huyo na ndipo walipompata akiwa amejificha mlimani nyuma ya shule ya msingi Sengerema na kwamba baada ya kukamatwa alikiri kuwa ndiye aliyemuua mke wake.
Kufuatia hali hiyo wananchi walishikwa na hasira na ndipo walipoanza kumpiga na kumkatakata kwa mapanga sehemu mbalimbali za mwili wake pasipo huruma hadi alipokata roho.
Polisi wilayani hapa waliweza kufika eneo la tukio na kukuta mtu huyo akiwa tayari ameshakufa ambapo wariruhusu mwili huo uzikwe na ule wa mke wake pia na kwamba hakuna mtu yeyote anayeshikiliwa kutokana na tukio hilo.
MWISHO.

No comments:

Post a Comment

Comments System

disqus

Disqus Shortname

msora

Popular Posts

Header Ads

ad