Wednesday, August 21, 2013

MKURUGENZI ABARIKI UFISADI


NA Mwandishi wetu Rorya.
21/8/2013
MKURUGENZI wa halimashauri ya wilaya ya Rorya mkoani Mara,Ephraem,Nguyaine amewaambia madiwani wa halimashauri hiyo kuwa kiasi cha shilingi million 14 zilizotumika kutengeneza gari la halimashauri hiyo analotumia ni pesa ndogo sana sawa na vijisent tu
Mkurugenzi huyo alitoa kauri hiyo juzi agost 13/2013 kwenye kikao cha baraza la madiwani hao lilifanyika katika wa Soa katika mji mdogo wa utegi.
Alisema kuwa anashangazwa na madiwani wanaodai kuwa pesa hizo ni nyingi zilizotumika katika matengenezo ya gari hilo lenye namba za usajili STK 5982 aina ya Toyota Land Cruser V8
‘’Mimi nawashangaa sana madiwani mnashangaa gari hilo kutengenezwa kwa gharama hiyo mbona wenzetu Tarime la kwao walitengeneza kwa million 70 na lile la mkuu wa mkoa lilitengenezwa kwa million 80’’alisema mkurugenzi huyo kwa dhihaka.
Hata hivyo kauri hiyo ya mkurugenzi huyo ilipingwa vikali na madiwani hao ambao walisema kuwa pesa hizo ni nyingi mno zilizotumika ukilinganisha na mahitaji ya halimashauri hiyo.
Diwani wa kata ya Mkoma kwa tiketi ya chadema,Lazaro Kitori alisema kuwa gari hilo pamoja na kutengezwa kwa gharama hiyo lakini lilifanya kazi kwa muda wa miezi sita tu na sasa limeharibika tena na kwamba huenda likahitaji pesa nyingi zaidi ya hizo.
Hoja hiyo iliungwa mkono na diwani wa kata ya Ikoma kwa tiketi ya chama cha mapinduzi ambaye pia aliunga mkono na kutaka gari hilo liuzwe kwani ni la anasa na linaitia hasara halimashauri hiyo ambayo bado ni change kimapato.
‘’Mwenyekiti mimi nashangaa sana mkurugenzi huyu anajibu majibu kirahisi hatuwezi kujilinganisha  na wilaya za Tarime wala na ofsi ya mkuu wa mkoa wenzetu wana mafungu ya kutosha kwakweli hili gari tuliuze tununue angalau tipa liwe linasomba mchanga katika shule zetu badala ya kuwa na gari ambalo ni la anasa’’alisema diwani huyo.
Hata hivyo baadhi ya wananchi wa wilaya hiyo waliohojiwa na gazeti hili kuhusiana na suala hilo wamedai kushangazwa na kauri ya kibabe ya mkurugenzi huyo kwani walidai kuwa halimashauri hiyo inakabiliwa matatizo mengi ukiwemo ukosefu wa huduma mbalimbali kwenye kata za halimashauri hiyo lakini mkurugenzi huyo halioni hilo bali anatumia pesa nyingi katika kutengeneza gari analotumia yeye.
‘’Huyu mkurugenzi wetu kwanza hana mahusiano na wananchi na muda mwingi jioni utamuona akiwa na gari hilo kwenye mabaa na sasa kama kweli madiwani wameona halina faidia ni bora liuzwe ili hizo pesa tujengewe hata zahanati na yeye anunuliwe gari ambalo siyo la anasa.’’alisema John Omondi mkazi wa Utegi
Katika hatua nyingine diwani wa tarafa ya Nyancha viti maalumu CCM,Pendo Odele amedai kuwa halimashauri hiyo imegawa kiasi cha shilingi milioni 400 kwa upendeleo katika kata nne huku zingine zikiachwa.
Diwani huyo alisema kuwa pesa hizo ambazo zilitolewa kwa ajili ya kujenga hostel katika shule mbalimbali za sekondari zilitolewa kinyemela kwani hazikupitia kwenye kamati ya fedha mipango na utawala lakini zoezi hilo lilifanywa na mkurugenzi na mwenyekiti wa halimashauri hiyo,Charles Ochere.
Alizitaja kata zilipewa pesa hizo kuwa ni kata ya Roche ambayo inaongozwa na mwenyekiti huyo ambayo ilipewa shilingi milioni mia moja,kata ya Labour ilipewa milioni mia moja,kata ya Kisumwa ilipewa milioni mia moja,kata ya Kigunga ilipewa million sabini na kata ya Thai ilipewa milioni therethini na kwamba pesa hizo zilitolewa mwezi wa nne mwaka huu.
Hata hivyo mwenyekiti wa halimashauri hiyo alipotakiwa kutoa ufafanuzi kuhusu pesa hizo pamoja na mkurugenzi wake hawakuweza kutoa majibu ya kulidhisha na kufauati hali hiyo madiwani wa kata 16 wameibuka na malalamiko hayo na kutaka wapewe majibu sahihi katika kikao kijacho.
Siku za hivi karibuni halimashauri ya wilaya ya Rorya imekuwa katika kashifa ya matumizi mabaya ya pesa za serikali hususani katika ujenzi wa nyumba za halimashauri hiyo

Diwani wa kata ya Turwa wilayani Tarime kwa tiketi ya Chadema,Ndesi Mbusiro akikabidhi madawati katika shule ya msingi Tagota ikiwa ni sehemu ya ahadi yake



DIWANI AKABIDHI MADAWATI


NA Berensi Alikadi-Tarime.
21/8/2013
DIWANI wa kata ya Turwa wilayani Tarime,Ndesi Mbusiro[CHADEMA} juzi alikabidhi madawati 8 na viti 13vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni moja katika shule ya msingi Tagota iliyoko katika kata ya Turwa wilayani hapo.
Akikabidhi vifaa hivyo kwa uongozi wa kijiji hicho pamoja na kamati ya shule hiyo diwani huyo alisema kuwa hiyo ni mojawapo ya ahadi alizoahidi katika shule hiyo wakati alipokuwa akiomba kura kwa wananchi wa kijiji hicho.
‘’Ndugu zangu ahadi ni deni nilipotoa ahadi katika shule hii kila nilipokuwa nikipita dhamira ilikuwa ikinisuta lakini leo nafurahi kwaambia wazazi na waalimu kuwa kile nilichokoahidi nimekitimiza na siyo hicho tu bali hata vingine ambavyo niliahidi nitajitahidi kadiri ya uwezo wangu ili niweze kutimiza’’alisema Ndesi
Alisema kuwa ana imani kuwa madawati hayo yatawasaidia wanafunzi wa shule hiyo ambao walikuwa na upungufu wa madawati ambapo pia viti hivyo vitawasaidia waalimu wa shule hiyo.
Awali mwalimu mkuu wa shule hiyo,Samweli Magoiga alisema kuwa shule hiyo illkuwa inakabiliwa na upungufu wa viti 32 na meza 43 na madawati139 hali ambayo imekuwa ikisababisha wanafunzi wa shule hiyo pamoja na waalimu kukaa kwa shida.
Alisema kuwa mapungufu mengine ni pamoja na uchakavu wa majengo na nyumba za waalimu na tatizo la umeme jambo alililomuomba diwani huyo alisimamie ambapo alisema kuwa wataendelea kuvifanyia marekebisho kadiri watakavyokuwa wanapata fedha toka halimashauri ya wilaya hiyo na kwa wafadhili.
Kwa upande wao baadhi ya wananchi wa kijiji hicho wamempongeza diwani huyo kwa kutekeleza ahadi yake na kwamba vifaa hivyo vitawasaidia waalimu na wanafunzi.
Mwenyekiti msitaafu wa kijiji hicho na mwenyekiti wa CCM kata ya Turwa,Eliakim Mwitentya alisema kuwa kiongozi bora ni Yule anayefanya kazi kwa vitendo hata kama anatoka chama cha upinzani na kwamba diwani huyo ameonyesha uongozi wa vitendo.
Naye mwenyekiti wa kamati ya shule hiyo Raheli Mwema amewataka waalimu wa shule hiyo kuvitunza ipasavyo kwani kuna baadhi ya shule zingine zimekuwa hazitunzi vifaa vya shule yakiwemo madawati na viti
Baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo waliongea na gazeti hili walimpongeza diwani huyo na kwamba watajitahidi kusoma kwa bidii kwani wamepata madawati mazuri ambayo yatasaidia kusoma wakiwa wamekaa pasipo na tatizo
Mwisho

DIWANI AKABIDHI SHULE MADAWATI


NA Berensi Alikadi-Tarime.
21/8/2013
DIWANI wa kata ya Turwa wilayani Tarime,Ndesi Mbusiro[CHADEMA} juzi alikabidhi madawati 8 na viti 13vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni moja katika shule ya msingi Tagota iliyoko katika kata ya Turwa wilayani hapo.
Akikabidhi vifaa hivyo kwa uongozi wa kijiji hicho pamoja na kamati ya shule hiyo diwani huyo alisema kuwa hiyo ni mojawapo ya ahadi alizoahidi katika shule hiyo wakati alipokuwa akiomba kura kwa wananchi wa kijiji hicho.
‘’Ndugu zangu ahadi ni deni nilipotoa ahadi katika shule hii kila nilipokuwa nikipita dhamira ilikuwa ikinisuta lakini leo nafurahi kwaambia wazazi na waalimu kuwa kile nilichokoahidi nimekitimiza na siyo hicho tu bali hata vingine ambavyo niliahidi nitajitahidi kadiri ya uwezo wangu ili niweze kutimiza’’alisema Ndesi
Alisema kuwa ana imani kuwa madawati hayo yatawasaidia wanafunzi wa shule hiyo ambao walikuwa na upungufu wa madawati ambapo pia viti hivyo vitawasaidia waalimu wa shule hiyo.
Awali mwalimu mkuu wa shule hiyo,Samweli Magoiga alisema kuwa shule hiyo illkuwa inakabiliwa na upungufu wa viti 32 na meza 43 na madawati139 hali ambayo imekuwa ikisababisha wanafunzi wa shule hiyo pamoja na waalimu kukaa kwa shida.
Alisema kuwa mapungufu mengine ni pamoja na uchakavu wa majengo na nyumba za waalimu na tatizo la umeme jambo alililomuomba diwani huyo alisimamie ambapo alisema kuwa wataendelea kuvifanyia marekebisho kadiri watakavyokuwa wanapata fedha toka halimashauri ya wilaya hiyo na kwa wafadhili.
Kwa upande wao baadhi ya wananchi wa kijiji hicho wamempongeza diwani huyo kwa kutekeleza ahadi yake na kwamba vifaa hivyo vitawasaidia waalimu na wanafunzi.
Mwenyekiti msitaafu wa kijiji hicho na mwenyekiti wa CCM kata ya Turwa,Eliakim Mwitentya alisema kuwa kiongozi bora ni Yule anayefanya kazi kwa vitendo hata kama anatoka chama cha upinzani na kwamba diwani huyo ameonyesha uongozi wa vitendo.
Naye mwenyekiti wa kamati ya shule hiyo Raheli Mwema amewataka waalimu wa shule hiyo kuvitunza ipasavyo kwani kuna baadhi ya shule zingine zimekuwa hazitunzi vifaa vya shule yakiwemo madawati na viti
Baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo waliongea na gazeti hili walimpongeza diwani huyo na kwamba watajitahidi kusoma kwa bidii kwani wamepata madawati mazuri ambayo yatasaidia kusoma wakiwa wamekaa pasipo na tatizo
Mwisho

DIWANI AKABIDHI SHULE MADAWATI


NA Berensi Alikadi-Tarime.
21/8/2013
DIWANI wa kata ya Turwa wilayani Tarime,Ndesi Mbusiro[CHADEMA} juzi alikabidhi madawati 8 na viti 13vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni moja katika shule ya msingi Tagota iliyoko katika kata ya Turwa wilayani hapo.
Akikabidhi vifaa hivyo kwa uongozi wa kijiji hicho pamoja na kamati ya shule hiyo diwani huyo alisema kuwa hiyo ni mojawapo ya ahadi alizoahidi katika shule hiyo wakati alipokuwa akiomba kura kwa wananchi wa kijiji hicho.
‘’Ndugu zangu ahadi ni deni nilipotoa ahadi katika shule hii kila nilipokuwa nikipita dhamira ilikuwa ikinisuta lakini leo nafurahi kwaambia wazazi na waalimu kuwa kile nilichokoahidi nimekitimiza na siyo hicho tu bali hata vingine ambavyo niliahidi nitajitahidi kadiri ya uwezo wangu ili niweze kutimiza’’alisema Ndesi
Alisema kuwa ana imani kuwa madawati hayo yatawasaidia wanafunzi wa shule hiyo ambao walikuwa na upungufu wa madawati ambapo pia viti hivyo vitawasaidia waalimu wa shule hiyo.
Awali mwalimu mkuu wa shule hiyo,Samweli Magoiga alisema kuwa shule hiyo illkuwa inakabiliwa na upungufu wa viti 32 na meza 43 na madawati139 hali ambayo imekuwa ikisababisha wanafunzi wa shule hiyo pamoja na waalimu kukaa kwa shida.
Alisema kuwa mapungufu mengine ni pamoja na uchakavu wa majengo na nyumba za waalimu na tatizo la umeme jambo alililomuomba diwani huyo alisimamie ambapo alisema kuwa wataendelea kuvifanyia marekebisho kadiri watakavyokuwa wanapata fedha toka halimashauri ya wilaya hiyo na kwa wafadhili.
Kwa upande wao baadhi ya wananchi wa kijiji hicho wamempongeza diwani huyo kwa kutekeleza ahadi yake na kwamba vifaa hivyo vitawasaidia waalimu na wanafunzi.
Mwenyekiti msitaafu wa kijiji hicho na mwenyekiti wa CCM kata ya Turwa,Eliakim Mwitentya alisema kuwa kiongozi bora ni Yule anayefanya kazi kwa vitendo hata kama anatoka chama cha upinzani na kwamba diwani huyo ameonyesha uongozi wa vitendo.
Naye mwenyekiti wa kamati ya shule hiyo Raheli Mwema amewataka waalimu wa shule hiyo kuvitunza ipasavyo kwani kuna baadhi ya shule zingine zimekuwa hazitunzi vifaa vya shule yakiwemo madawati na viti
Baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo waliongea na gazeti hili walimpongeza diwani huyo na kwamba watajitahidi kusoma kwa bidii kwani wamepata madawati mazuri ambayo yatasaidia kusoma wakiwa wamekaa pasipo na tatizo
Mwisho

DIWANI AKABIDHI SHULE MADAWATI


NA Berensi Alikadi-Tarime.
21/8/2013
DIWANI wa kata ya Turwa wilayani Tarime,Ndesi Mbusiro[CHADEMA} juzi alikabidhi madawati 8 na viti 13vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni moja katika shule ya msingi Tagota iliyoko katika kata ya Turwa wilayani hapo.
Akikabidhi vifaa hivyo kwa uongozi wa kijiji hicho pamoja na kamati ya shule hiyo diwani huyo alisema kuwa hiyo ni mojawapo ya ahadi alizoahidi katika shule hiyo wakati alipokuwa akiomba kura kwa wananchi wa kijiji hicho.
‘’Ndugu zangu ahadi ni deni nilipotoa ahadi katika shule hii kila nilipokuwa nikipita dhamira ilikuwa ikinisuta lakini leo nafurahi kwaambia wazazi na waalimu kuwa kile nilichokoahidi nimekitimiza na siyo hicho tu bali hata vingine ambavyo niliahidi nitajitahidi kadiri ya uwezo wangu ili niweze kutimiza’’alisema Ndesi
Alisema kuwa ana imani kuwa madawati hayo yatawasaidia wanafunzi wa shule hiyo ambao walikuwa na upungufu wa madawati ambapo pia viti hivyo vitawasaidia waalimu wa shule hiyo.
Awali mwalimu mkuu wa shule hiyo,Samweli Magoiga alisema kuwa shule hiyo illkuwa inakabiliwa na upungufu wa viti 32 na meza 43 na madawati139 hali ambayo imekuwa ikisababisha wanafunzi wa shule hiyo pamoja na waalimu kukaa kwa shida.
Alisema kuwa mapungufu mengine ni pamoja na uchakavu wa majengo na nyumba za waalimu na tatizo la umeme jambo alililomuomba diwani huyo alisimamie ambapo alisema kuwa wataendelea kuvifanyia marekebisho kadiri watakavyokuwa wanapata fedha toka halimashauri ya wilaya hiyo na kwa wafadhili.
Kwa upande wao baadhi ya wananchi wa kijiji hicho wamempongeza diwani huyo kwa kutekeleza ahadi yake na kwamba vifaa hivyo vitawasaidia waalimu na wanafunzi.
Mwenyekiti msitaafu wa kijiji hicho na mwenyekiti wa CCM kata ya Turwa,Eliakim Mwitentya alisema kuwa kiongozi bora ni Yule anayefanya kazi kwa vitendo hata kama anatoka chama cha upinzani na kwamba diwani huyo ameonyesha uongozi wa vitendo.
Naye mwenyekiti wa kamati ya shule hiyo Raheli Mwema amewataka waalimu wa shule hiyo kuvitunza ipasavyo kwani kuna baadhi ya shule zingine zimekuwa hazitunzi vifaa vya shule yakiwemo madawati na viti
Baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo waliongea na gazeti hili walimpongeza diwani huyo na kwamba watajitahidi kusoma kwa bidii kwani wamepata madawati mazuri ambayo yatasaidia kusoma wakiwa wamekaa pasipo na tatizo
Mwisho

Comments System

disqus

Disqus Shortname

msora

Popular Posts

Header Ads

ad