Sunday, August 4, 2013

DIWANI WA CHADEMA AFICHUWA MBINU ZA CCM-TARIME


 DIWANI WA CHADEMA AFICHUA NJAMA ZA CCM TARIME.
NA Berensi Alikadi-Tarime.
5/8/2013
Diwani wa kata ya Turwa katika halimashauri ya mji wa Tarime kupitia chama cha demokrasia na maendeleo [Chadema] Charles Ndessi Mbusiro amesema chama cha mapinduzi CCM wilayani Tarime kimepora uwanja wa michezo pasipo ridhaa ya wananchi.
Diwani huyo alitoa tuhuma hizo juzi julai 28 mwaka huu wakati alipokuwa akihutubia maelfu ya wananchi wa Tarime waliohudhulia maadhimisho ya miaka mitano tangia kifo cha aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya Chadema marehemu Chacha Zakayo Wangwe maadhimisho yaliyofanyika kwenye uwanja wa michezo wa Serengeti.
Amesema kuwa uwanja huo ni mali ya wananchi wote wa Tarime lakini chama cha mapinduzi kwa hila zake baada ya kuona uwanja huo ukitumiwa mara kwa mara na Chadema katika mikutano yake wamefanya ujanja na kupata hadi ambapo sasa wanadai kuwa ni mali yao.
‘’Ndugu zangu wananchi wa Tarime napenda kuwafahamisha kuwa uwanja huu mliopo sasa CCM wamefanya njama na wameuchukuwa na wanadai kuwa ni wakwao na tayari wanataka kujenga vibanda na wameshagawana vibanda kila kioongozi ana milango yake sijui kama wananchi mnalijua hilo’’alisema diwani huyo huku akijibiwa na wananchi kuwa hatujui na tunataka waurudishe.
Diwani huyo ambaye pia ni mwenyekiti wa madiwani wa Chadema wilaya ya Tarime alidai kuwa uwanja huo ulijengwa na wananchi wote kipindi cha mfumo wa chama kimoja na kwamba CCM haina hati miliki wala haina mamlaka ya kupora kiwanja hicho ambapo amesema wakiongoza halimashauri CCM wajuwe kuwa kiwanja hicho kitarudi mikononi mwa wananchi na wala si vinginevyo hayuko tayari kuona nguvu za wananchi zinaporwa na kundi la watu wachache.

Alifafanua kuwa tayari wanataka ccm iwambie kama ni chama cha biashara ama ni chama cha siasa kwani viongozi wa chama hicho ndio waliojipanga kufanya biashara katika uwanja huo na kwamba hata kodi wanazokusanya sasa hivi kwa wamachinga ni za kuwaibiwa wananchi hivyo Chadema haitakuwa na mzaha katika hilo ni lazima kitaeleweka.
Diwani huyo alieleza kuwa kitendo cha chama hicho kupora kiwanja hicho huku wakijua kuwa siyo mali yao kinaonyesha dhahiri njisi kisivyowatakia mema wananchi wake na kwamba kitendo hicho lazima kilaaniwe na kila mwananchi wa Tarime mpenda maendeleo.
Wakiongea na gazeti hili kwa nyakati tofauti baadhi ya wananchi wa mji wa Tarime wamedai kusikitishwa na kitendo hicho ambacho walisema ni cha kifisadi na kwamba jambo hilo si la kufumbia macho.
‘’Unajuwa hawa  watu wa magamba wamezoea sana dhuruma na ufisadi hiki kiwanja ni cha wananchi wote na wala si cha CCM sasa leo nimeshangaa kusikia kuwa wamekichukuwa kwa nguvu ili kiwe mali yao kwakweli hili halitawezekana tumechoka kuonewa liwalo na liwe lazima wakirudishe’’alisema mwananchi mmoja Mwita Mseti mkazi wa mtaa wa  rebu.
Kufuatia tuhuma hizo gazeti hili lilimtafuta katibu wa chama hicho wilaya,ili aweze kujibu tuhuma hizi lakini hakuweza kupatikana na wala mwenyekiti wake pia hakuweza kupatikana.
mwisho

No comments:

Post a Comment

Comments System

disqus

Disqus Shortname

msora

Popular Posts

Header Ads

ad