Monday, September 16, 2013

SERIKALI KUENDELEA KULINDA BONDE LA MTO MARA



NA Berensi Alikadi-Serengeti.
16.9.2013
SERIKALI imesisitiza adhima yake ya kuendelea kulilinda bonde la mto Mara kutokana na umuhimu wa bonde hilo kwa nchi za Kenya na Tanzania kiuchumi.
Kauri hiyo ya serikali imetolewa na waziri mkuu Mizengo Pinda wakati alipokuwa akihutubia wananchi  wa Kenya na Tanzania kwenye kilele cha maadhimisho ya Mara day zilizofanyika katika uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine mjini Mugumu wilayani Serengeti mkoani Mara.
Waziri mkuu alisema kuwa  viongozi wanatakiwa kuendelea kuelimisha umma juu ya suala zima la uhifadhi wa mazingira katika mto mara kwani ndiyo njia pekee ya kununusuru bonde hilo.
Alisema kuwa Tanzania inashirikiana na Kenya kwa sababu chemichemi za mto Mara zimeanzia kwenye milima ya Mau nchini Kenya na kupitia katika hifadhi za masai Mara hadi Serengeti kwa upande wa Tanzania.
‘’Tanzania kwa kutambua ukubwa wa jambo hili tumekubali kutii protoko ya kulinda mto Mara na tutauheshimu’’alisema Pinda.
Alifafanua kuwa katika sera ya maji ya mwaka 2002 na sheria usimamizi wa maji ya mwak 2009 vimetambua bonde hilo kwa faida ya vizazi vya sasa na vijavyo hivyo tutumie maji vizuri na tunawahakikishia wenzetu wa Kenya kuwa tutaendelea kuheshimu makubaliano hayo.
Aliongeza kuwa pamoja na bonde hilo kuwepo lakini bado zipo changamoto mbalimbali zinazolikabili ikiwa ni pamoja na uharibifu wa mazingira,kilimo kando kando ya bonde hilo na uchomaji moto ovyo ambavyo aliwagiza viongozi wa maeneo hayo kuhakikisha wanasimamia visitokee tena.
Kwa upande wake naibu waziri wa maji,Mhandisi Binilith Mahenge alisema kuwa lengo kuu la kuanzishwa kwa kamisheni ya bonde la mto Mara ni kuhamasisha jamii katika kuhifadhi mistu na vyanzo vya maji na kwamba hadi sasa jumla ya miradi 122 ya uhifadhi wa mazingira imeanza kutekelezwa.
Awali akimkaribisha waziri mkuu kuongea na wananchi,mkuu wa mkoa wa Mara John Tupa alisema kuwa pamoja na mambo mengine sherehe hizi pia zinahusha tukio kubwa la wanyama aina ya nyumbu ambao uhama makundi kwa makundi toka hifadhi ya masai Mara na kuja katika hifadhi ya Serengeti.
Mwisho

No comments:

Post a Comment

Comments System

disqus

Disqus Shortname

msora

Popular Posts

Header Ads

ad