Saturday, October 5, 2013

SERIKALI KUENDELEA KUSAIDIANA NA MADHEHEBU YA DINI



NA Berensi Alikadi-Bunda.
6.10.2013
SERIKALI wilayani Bunda imeseme itaendelea kusaidiana na madhehebu ya dini wilayani humo ili kuiweka wilaya  hiyo katika hali ya amani na utulivu.
Kauri hiyo ya serikali imetolewa juzi  wakati wa misa ya kumuwekea mikono mchungaji mpya wa kanisa la Menonite la mjini Bunda,Stafa Nashon Waryuba.
Mkuu wa wilaya hiyo,Joshua Mirumbe ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasim katika sherehe hizo alisema kuwa madhehebu ya dini katika wilaya hiyo yanafanya kazi kubwa ya kuwaweka wananchi katika imani hivyo hayana budi kuheshimiwa.
Alisema kuwa kanisa la Menonite lina histolia kubwa hapa nchini na kwamba serikali inatambua mchango wake katika kuwaandaa wananchi waweze kumutumikia mungu kwani amani iliyopo hapa nchini imetokana na madhehebu ya dini
‘’Nafurahi sana kuwa leo Nashon sasa amekuwa mchungaji na kuanzia sasa tutakuita mchungaji lakini ufahamu kuwa kazi ya uchungaji ni ngumu maana unadili na waumini kila wakati hivyo ni lazima ujitume na sisi serikali tutakupa msaada kamatunavyoyapa madhehebu mengine.’’alisema Mirumbe.
Awali askofu wa kanisa la menonite jimbo la Serengeti,Christopher Ndege alisema kuwa kanisa linataka viongozi imara na shupavu wanaoweza kulisimamia na akamtaka mchungaji huyo awe mfano bora kwa waumini wa kanisa hilo.
Naye mchungaji Nashon akiwashukuru waamini wa kanisa hilo na makanisa mengine yaliyohudhulia hafla hiyo alisema kuwa atatumia karama yake aliyopewa na mwenyezi mungu katika kulitumikia kanisa hilo na jamii ya Kitanzania na akawaomba waendelee kumuombea na kumpa ushirikiano.
Kabla ya kuwekewa mikono na askofu ndege,mchungaji Nashon alikiri mbele ya waaumini wa kanisa hilo na kula kiapo cha uaminifu kama mchungaji na kisha alipewa hati maalumu ya uchungaji na askofu huyo.
Mwisho

No comments:

Post a Comment

Comments System

disqus

Disqus Shortname

msora

Popular Posts

Header Ads

ad