Sunday, September 1, 2013

WANAKIJIJI WADAI KULAWITIA NA KUNAJISIWA KISHIRIKINA


NA Berensi Alikadi,Bunda.
1/9/2013
WANANCHI  vijiji vya kata ya Butimba katika tarafa ya Kenkyombyo wilayani Bunda mkoani Mara wanaishi kwa hofu kubwa kutokana na kuibuka kwa vitendo vya kishirikina katika vijiji hivyo.
Wakiongea na Tanzania daima ilipotembelea vijiji hivyo jana wananchi hao wamedai kuwa kwa muda wa wiki nzima sasa kumekuwepo na vitendo vya kishirikiana ambapo watu wasiofahamika wamekuwa wakienda katika vijiji hivyo majira ya usiku na kuwanajisi wanawake na bila wao kujitambua.
Aidha walifafanua kuwa baada ya watu hao kuwafanyia vitendo hivyo huchukuwa pesa na kuondoka ambapo wao huwa hawajitambui kabisa.
Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Buramba wameliambia Tanzania daima kuwa tatizo hilo siyo kwa akina mama tu bali watu hao ambao kwa lugha ya kijita wanafahamika kama [wafafuti] wamekuwa wakiwalawiti hata wanaume jambo ambalo limezuia hofu kubwa.
‘’Kwakweli Mwandishi hali hii inasikitisha sana watu hawa haifahamiki wanakuja saa ngapi isipokuwa tu asubuhi wewe unakuta umenajisiwa na una mbegu za kiume sasa inashangaza hapo awali walianzia kwa wanawake lakini sasa hata wanaume’’alisema mtu huyo ambaye hakutaka atajwe gazetini.
Diwani wa kata hiyo Ngunya  Msalaba amekiri kuwepo kwa hali hiyo na kwamba mnamo agost 26 mwaka huu majira ya saa tano usiku kaya tano za wafanyakazi wa kiwanda cha kuchambua pamba cha Bulamba walikumbana na dhahama hiyo
Msalaba alisema kuwa baada ya kuwepo kwa matukio hayo waliamua kufanya mkutano wa hadhara katika kijiji hicho ambapo walikubaliana mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwarudisha makwao waganga wote wa kienyeji ambao wamehamia katika vijiji vya kata hiyo.
Alisema kuwa jambo lingine walilokubaliana na pamoja na wageni wote wanaokwenda kufanya kazi katika kiwanda hicho wawe na vitambulisho vinavyotambulika na wavipeleke kwa viongozi wa kijiji hicho.
Sambamba na hilo diwani huyo alidai kuwa wameanzisha jeshi la sungusungu  kwa ajili ya kulinda usiku na mchana ili kama watamuona mtu mgeni waweze kumuhoji.
‘’Lakini pia tumeunda jeshi la sungusungu ambalo litalinda mchana na usiku ingawaje pia ni kazi ya ziada maana watu wenyewe wanakuja usiku kazi ipo mimi sijawahi kusikia jambo hili’’alisema diwani huyo.
Kufutia hali hiyo diwani huyo ametoa wito kwa wananchi hao kuwa na subira wakati wakiendelea kulifanyia uchunguzi suala hilo ambalo alisema linatia shaka maisha ya wananchi wa kata hiyo.
Tatizo hilo la wananchi kuingilia na kunajisiwa kishirikina limeshamili sana katika kipindi cha miaka zaidi ya miwili hasa katika jimbo la Mwibara ambako hivi karibuni wananchi wa vijiji vya Kasahunga walikumbwa na tatizo hilo
Mwisho

No comments:

Post a Comment

Comments System

disqus

Disqus Shortname

msora

Popular Posts

Header Ads

ad