Sunday, October 27, 2013

WACHIMBAJI WAFA KWA KUFIKIWA NA KIFUSI.


NA  Berensi Alikadi-Bunda
23/10/2013
WACHIMBAJI wawili wa madini katika mgodi ulioko katika kijiji cha Kamukenga wilayani Bunda mkoani Mara wamefariki dunia baada ya kufukiwa na kifusi.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo diwani wa kata ya Kiwasi mahali kilipo kijiji hicho,Lawi Nyamajeje alisema kuwa tukio hilo limetokea jana majira ya saa kumi na mbili alifajili.
Alisema kuwa siku hiyo ya tukio wachimbaji hao waliingia katika shimo hilo kwa ajili ya kuchimba dhahabu na kwamba wakiwa wanaendelea na kazi hiyo ghafula walipolomokewa na kifusi.
Diwani huyo alifafanua kuwa baada ya kufukiwa na kifusi hicho jitihada za kuwaokoa zilishindikana na kwamba walipofanikiwa kuwatoa tayari walikuwa wameshakufa.
Aliwataja waliokufa kuwa ni,Paskali Wiliam 16 mkazi wa kijiji cha Kamukenga na Robert Kamoga 18 mkazi wa wilayani Serengeti mkoani Mara.
Aidha aliongeza kuwa katika tukio hilo watu wawili walijeruhiwa vibaya na kwamba walikimbizwa katika hosptali ya wilaya ya Bunda kwa ajili ya matibabu.
Hata hivyo diwani huyo alisema kuwa baada ya tukio hilo waliweza kukaa na mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai wilaya ya Bunda pamoja na wachimbaji ili kuona namna ya usalama wa migodi hiyo ya wachimbaji wadogo wadogo kuendeshwa kwa usalama zaidi.
Polisi wilayani hapa wamethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba hakuna mtu yeyote anayeshikiliwa kutokana na tukio hilo
Mwisho




                                                       

No comments:

Post a Comment

Comments System

disqus

Disqus Shortname

msora

Popular Posts

Header Ads

ad