Wednesday, June 10, 2015

Baada ya ushindi, ‘Messi’ atoa somo kwa wachezaji wa bongo kwa kile kilichompata

Ramadhani Singano 'Messi' (katikati) akizungumza na waandishi wa habari maara baada ya kikao chao na TFF kumalizika

Ramadhani Singano ‘Messi’ (katikati) akizungumza na waandishi wa habari maara baada ya kikao chao na TFF kumalizika
Baada ya uongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kutoa uamuzi juu ya sakata la kimkataba lililokuwa linamhusu winga Ramadhani Singano na klabu yake ya Simba ambapo TFF imeivunja mikataba yote miwili, wa Singano na wa Simba huku ikiwashauri Simba SC kukaa meza moja na Singano ili kujadiliana upya suala la mkataba mwingine kwa ajili ya msimu mwingine.
Singano amesema kuwa, anamshukuru Mungu kwa mikataba yote kuvunjwa na hiyo inamaanisha yeye ni mchezaji huru huku akisema amepata fundisho kubwa juu ya maswala ya mikataba na kuwashauri wachezaji wengine kutafuta watu wa kuwasaidia hasa pale inapokuja suala la kusaini mikataba ili kuzitumikia timu zinazohitaji saini zao.
“Wamesema (TFF) mikataba yote imefutwa kwahiyo mimi nikae chini na Simba tukubaliane upya kwasababu mimi kwasasa ni mchezaji huru, na kama ikitokea tumeshindwana basi mimi ntaongea na timu nyingine. Kikubwa tukae chini tuzungumze kama na wao bado wana nia na mimi”, amesema Singano.
“Ianabidi sasahivi ndiyo wanipe ‘proposal’ yao ya mkataba niiangalie halafu na mimi niingize vitu vyangu, waulete huo mkataba wao mpya niusome kwanza lakini kikubwa sio kukomoana. Mimi namshukuru Mungu kwakuwa wao wenyewe wamekubali kwamba hapa kuna utata na kukubali mikataba yote ifutwe tuanze upya, namshukuru sana Mungu kwa hili”, Singano alisisitiza.
“Nimejifunza kitu kimoja kwamba yani si kila kitu unachokiona ndo ukiamini hichohicho, inabidi ukione na ukifanyie utafiti. Nawashauri wachezaji wengine kabla ya kusaini mikataba na timu zao wasikose watu wa kuwaongoza, maana utakapokwama utaongozwa na mtu huyo,  lakini ukikosa utahangaika sana”, ameshauri Singano.
Kwa upande wa Simba SC kupitia kwa afisa habari wao Hajji Manara wamesema, kesho watafanya kikao cha kamati ya utendaji. Moja ya ajenda zao ni kujadili kuhusu suala la Singano na watatoa kauli ya timu baada ya kikao hicho kukamilika na kupata majibu juu ya jambo hilo.

Friday, June 5, 2015

mkutano wa NSSF Arusha

Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Crescentius Magori akimpatia maelekezo, MC wa Mkutano wa tano wa Wadau wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Sauda Simba wakati wa Mkutano huo unaonedelea leo, kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa AICC,jijini Arusha.

Kesi ya mawaziri watatu yatupwa nchini Kenya

Tobiko
Mwendesha mashtaka mkuu nchini Kenya Keriako Tobiko imeagiza kesi ya ufisadi dhidi ya mawaziri watatu na seneta wa jimbo la Nairobi Mike Sonko, kufutiliwa mbali.
Mawaziri hao pamoja na waziri wa kilimo, wa nishati na waziri wa uchukuzi Michael Kamau ambaye alifikishwa mahakamani siku ya alhamisi na kauchiliwa kwa dhamana ya shillingi milioni moja.
Mawaziri hao walisimamishwa kazi na rais Uhuru Kenyatta kufuatia ripoti zilizowahusisha na sakata za ufisadi.
Waziri wa kilimo alituhumiwa kuhusika na njama ya kuidhinisha uagizaji wa sukari bila kufuata sheria naye wa uchukuzi alituhumiwa kuidhinisha kandarasi iliyopewa kampuni moja ya usafirishaji na uagizaji mali.
Naye waziri wa nishati pamoja na seneta wa Nairobi Mike Sonko walikuwa wakichunguzwa kuhusiana na zabuni iliyotolewa na kampuni ya kusafirisha mafuta nchini Kenya, Kenya Pipeline.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na ofisi ya mwendesha mashtaka mkuu, Keriako Tobiko, kesi dhidi ya mawaziri hao zilifulitiliwa mbali kutokana na ukosefu wa ushahidi wa kutosha kuwafungulia mashtaka.
Maafisa wengine ambao kesi zao zimetupiliwa mbali ni pamoja na gavana wa Narok, Samuel Tunai na maafisa wengine saba wa kaunti hiyo ambao walikuwa wakikabiliwa na tuhuma za kutumia mamlaka yao vibaya.
Kesi pia iliondolewa kutokana na ukosefu wa ushahidi wa kutosha.
Taarifa hiyo imesema kuwa jumla ya faili ishirini na nane zimewasilishwa kwa ofisi ya mwendesha mashtaka, sita kati yao zikifungwa kutokana na ukosefu wa ushahidi wa kutosha.
Aidha faili kumi na saba zimeidhinishwa kupelekwa mahakamani, faili mbili nazo zikirejeshwa kwa tume hiyo na mwendesha mashtaka.
Kwa ujumla washukiwa sabini na wanne watafunguliwa mashtaka.
Miezi miwili iliyopita rais Kenyatta aliwasilisha bungeni majina ya maafisa wakuu wa serikali waliotuhumiwa kuhusika na ufisadi na kuwasimamisha kazi wote kwa muda wa miezi miwili.
Orodho hiyo ilikuwa na majina ya mawaziri watano na tayari kesi dhidi ya waziri wa ardhi imetupiliwa mbali. Hatma ya waziri wa leba bado ingali mikononi mwa tume hiyo.
Kwa miongo kadhaa wanaharakati wa kijamii na wafadhili wamelalamikia kukithiri wa ufisadi serikali.
chanzo BBC

Ndovu yatima wafunguliwa kituo

Tanzania imeanzisha kituo cha kwanza cha tembo yatima mjini Arusha.
Kituo hicho kinatarajiwa kuhifadhi watoto wa tembo waliopoteza wazazi wao kutokana na vitendo vya ujangili au sababu nyengine.
Hatua ya serikali ya kuanzisha kituo hicho inakuja baada ya utafiti wa serikali kubaini kuwa Tanzania hupoteza takriban tembo 30 kila siku.
Kituo hicho kinatarajiwa kutoa uangalizi kwa tembo wadogo wapatao 40, na watahifadhiwa mpaka watakapokuwa wakubwa na hatimae kurudishwa katika mazingira yao halisia.
Katika mahojiano ya hivi karibuni na BBC, waziri wa Utalii wa Tanzania Lazaro Nyalandu amebaini kwamba katika hifadhi ya taifa ya Ruaha pekee, tembo wapatao 12,000 walitoweka katika kipindi cha mwaka mmoja.
Waziri Nyalandu amekiri kwamba kiwango hicho ni kikubwa mno na kwamba kinatia wasiwasi hivyo kuongeza kwamba uchunguzi umefanyika kubaini chanzo cha tatizo hilo.
Ndovu yatima wafunguliwa kituo
Mamlaka maalumu ya Umoja wa Mataifa inayojihusisha na wanyama walio hatarini, imesema kwamba takwimu hizo zinaashiria kwamba Tanzania ni kitovu cha ujangili huku pembe za ndovu zikisafirishwa kupitia bandari ya Dar es
Salaam kwenda nchi jirani.
Tangu mwaka 2009, angalau tani 45 za pembe za ndovu zinaaminika kusafirishwa kwa njia za magendo kutoka Tanzania.
Ripoti zinasema Kenya hupoteza mabilioni ya dola kila mwaka kutokana na ufisadi.
chanzo BBC

Alibino ni wenzetu tuwalinde

Wachambuzi waonya Al Shabab yatanua operesheni zake Kenya

Wapiganaji wa kundi la Somalia la Al Shabab wanazidi kutanua mashambulizi yao kaskazini mashariki mwa Kenya na wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanaitaka Kenya kuchukua hatua madhubuti kuwakata makali waasi hao
Kenya imeweza kuyatuma majeshi yake kwa wingi kusini mwa Somalia lakini inaonekana kushindwa kuyalinda maeneo kadhaa nchini mwake dhidi ya kitisho cha kundi la waasi la Al Shabab.
Maafisa wa usalama kutoka nchi za magaharibi wanaonya Kenya inapaswa kuchua hatua za haraka kulizuia kundi hilo dhidi ya kukita mizizi nchini humo na kuendelea kuwasajili vijana kuwa wapiganaji wake wapya.
Wachambuzi wanasema Al Shabab haina tena hamu ya kuendelea na operesheni zake Somalia kwani wameshindwa kutokana na kampeini kabambe ya kijeshi ya Umoja wa Afrika, wamepoteza makali na mashambulizi yao ambayo siku hizi si mengi kama miaka ya nyuma nchini Somalia, hayapati kuangaziwa pakubwa na vyombo vya habari.
Al Shabab wameelekeza uasi Kenya
Hali nchini Kenya ni tofauti, waasi hao wa Al shabab wamepata mazingira mapya ya kuendeleza itikadi zao za kijihadi, kupata wapiganaji wapya na uwezekano mkubwa wa kuiyumbisha nchi hiyo.
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta na Makamu wa Rais William Ruto Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta na Makamu wa Rais William Ruto
Kenya imejikuta inakabiliwa na kibarua kigumu kufuatia kuibuka kwa seli za al shabab na mkakati wao wa kuyatuma majeshi yake mwaka 2011 kusini mwa Somalia kwa lengo la kulitokomeza kundi hilo na kuimarisha usalama katika mipaka yake kunaonekana kutozaa matunda yaliyohitajika.
Matokeo yake, waasi hao wamekuwa wakiingia na kutoka Kenya, wakifanya mashambulizi chungu nzima yakiwemo mauaji ya watu wengi na kurejea nchini mwao bila taabu licha ya mapambano makali kutoka kwa majeshi ya umoja wa Afrika na mashambulizi ya angani yanayofanywa na ndege za kijeshi zisioendeshwa na marubani za Marekani nchini Somalia.
Katika kaunti ya Mandera, abiria 28 waliokuwa wakisafiri kwa basi kutoka mji huo kuelekea Nairobi waliuawa na waasi hao mwaka jana, siku chache baadaye wafanyakazi wa mgodini 36 walishambuliwa na kuuawa katika eneo hilo hilo.
Mwezi Aprili mwaka huu, al shabab ilishambulia chuo kikuu cha Garissa na kuwaua takriban wanafunzi 150. Duru za kiusalama zinasesma waasi hao wa Al shabab wanafanya pia operesheni nyingine ambazo hazigongi vichwa vya habari kwasababu hakuna mauaji ya watu wengi lakini ambazo vile vile zinatia wasiwasi mkubwa.
Kwa mfano mwezi uliopita waasi hao waliingia katika kijiji cha Yumbis katika kaunti ya Garissa, kufanya ibada katika msikiti mmoja kwa saa kadhaa, kuwatisha wakaazi wa eneo hilo na kuondoka bila ya kupata pingamizi lolote.
Al Shabab yaingia na kutoka Kenya bila taabu
Wiki hii inaripotiwa waasi hao wameingia katika kijiji kimoja katika kaunti jirani ya Mandera na kusababisha shule kufungwa na wakaazi kuyatoroka makaazi yao.
Ramani ya Kenya ikionyesha maeneo ya ksakazini yanayoshambuliwa na Al Shabab Ramani ya Kenya ikionyesha maeneo ya ksakazini yanayoshambuliwa na Al Shabab
Wataalamu wa masuala ya kiusalama wanaishauri serikali ya Kenya kuimarisha udhibiti wao katika maeneo ya mipaka ikizingatiwa kuwa vyanzo vingi mipakani havina ulinzi wa kutosha na hakuna miundo mbinu ya kuzuia kuingia na kutoka kwa urahisi kwa waasi hao.
Suala la iwapo Kenya inahitaji kuyaondoa majeshi yake nchini Somalia, limekuwa likizua mjadala mkali miongoni mwa wanasiasa nchini humo lakini inaonekana serikali ambayo imekuwa ikisisitiza haitayaondoa majeshi yake kwani kwa kufanya hivo ni kuwapa magaidi ushindi, inabadili mkakati.
Mwenyekiti wa kamati ya Seneti kuhusu usalama wa kitaifa na uhusiano wa nchi za kigeni Yusuf Hajji amedokeza katika mahojiano na kituo cha redio cha Kenya cha Capital kuwa mkakati wa kuyaondoa majeshi Somalia sio mwiko na ni jambo amablo linajadiliwa kwa kina kuona namna bora ya kulitekeleza na kuwahamisisha vijana kutoshawishika na itikadi kali za kijihadi kama sehemu ya kulitafutia ufumbuzi tatizo hilo la Al Shabab.
chanzo idhaa ya kiswahili ya sauti ya ujerumani

Tuwalinde wasipotee

Comments System

disqus

Disqus Shortname

msora

Popular Posts

Header Ads

ad