Thursday, September 17, 2015

13 wauwawa kwa bomu Baghdad

Kiasi  watu  13, ikiwa  ni  pamoja  na mshambuliaji  wa kujitoa  muhanga , wamekufa  leo  katika  mashambulizi mawili tofauti  katikati  ya  mji  mkuu  wa  Iraq Baghdad.
polisi  imesema  shambulio  la  kwanza  lilitokea  katika wilaya  ya  kibiashara  ya  Bab al-Sharj ambako  bomu liliripuka  katika  gari  iliyoegeshwa. Watu  wanane waliuwawa  na  wengine  40 wamejeruhiwa.
Mshambuliaji  wa  kujitoa  muhanga , akivalia  mkanda  wa miripuko , alijiripua  katika  eneo  la  Wathba , akijiuwa binafsi na  watu  wengine  wanne.  Maafisa wa polisi ni miongoni  mwa  waliouwawa.
Hakuna  kundi  lililodai  kuhusika  na  shambulio  hilo  hadi sasa. Mashambulizi  ya  hapo  kabla  yamedaiwa kutekelezwa  na  kundi  la  Dola  la  Kiislamu, ambalo linadhibiti  maeneo  makubwa  kaskazini  na  magharibi  ya Iraq.
CHANZO BBC

No comments:

Post a Comment

Comments System

disqus

Disqus Shortname

msora

Popular Posts

Header Ads

ad