Thursday, September 17, 2015

Wanajeshi wamkamata rais na waziri mkuu Burkina Faso

Kikosi  cha  ulinzi  wa  rais nchini  Burkina Faso kimetangaza mapinduzi leo siku  moja  baada  ya kuwakamata  rais  wa  mpito  na  waziri  mkuu jana, wakati nchi  hiyo  ikijitayarisha  kwa  uchaguzi  mkuu  wa  kwanza tangu  kupinduliwa kwa  kiongozi  wa  nchi  hiyo Blaise Compaore.
Akitangaza  mapinduzi luteni  kanali Mamadou Bamba amesema  mazungumzo  yanafanyika  hivi  sasa  kuunda serikali itakayoiongoza  nchi  hiyo  katika  uchaguzi  wa amani.
Kumekuwa  na  maandamano  mitaani nje  ya  Ikulu  ya rais na Baraza  la  Usalama  la  Umoja  wa  mataifa limeshutumu  vikali kukamatwa  kwa  viongozi  hao na kutaka  waachiliwe  haraka.
Wanajeshi  wa  kikosi  cha  ulinzi  wa  rais  wenye mafungamano  na  rais  wa  zamani Blaise Compaore waliingia  katika  mkutano  wa  baraza  la  mawaziri  jana na kumkamata  rais Michel Kafando, waziri  mkuu Isaac Zida na  mawaziri  wengine  wawili.
Kaimu spika  wa  bunge la Burkina Faso  Cherif Sy ameshutumu  vikali  leo kile  alichosema kuwa  ni mapinduzi  nchini  Burkina  Faso.
CHANZO BBC

No comments:

Post a Comment

Comments System

disqus

Disqus Shortname

msora

Popular Posts

Header Ads

ad