Thursday, September 17, 2015

Serikali ya mpito Burkina faso yapindult

 

Kumefanyika mapinduzi nchini Burkina Fasso.
Kikosi cha walinzi wa rais kimetangaza katika runinga ya taifa kwamba kimevunjilia mbali kile ilichokitaja kuwa serikali ya mpito isiyoambilika.
Mwanachama wa kikosi hicho jenerali Gilbert Diendere ametajwa kuwa kiongozi mpya wa mpito.
Waandamanaji nje ya makao makuu ya rais nchini Burkina Faso
Mipaka yote imefungwa huku amri ya kutotoka nje ikiwekwa.Mkuu wa bunge amelitaka jeshi kuingilia kati ili kuzuia hatua hiyo aliyoitaja kuwa ya kundi dogo la wanajeshi.
Kikosi cha walinzi wa rais kimefyatua risasi hewani katika mji mkuu wa Ouagadougou huku watu wakikongamana kufanya maandamano.
Rais wa mpito Michel Kafando amepokonywa madaraka yake huku serikali yake ikivunjiliwa mbali, kwa mujibu wa afisa mmoja wa jeshi aliyezungumza katika runinga ya taifa nchini humo RTB.
n Rais wa Mpito Michel Kafando na waziri mkuu Isaac Zida
''Tumeweka baraza la kitaifa la demokrasia litakalopanga uchaguzi wa kidemokrasia,'' alisema afisa huyo aliyevaa sare za kijeshi ambaye hakutambulika.
Hatua hiyo inajiri baada ya viongozi wa serikali hiyo ya mpito nchini Burkina Faso kuzuiliwa na walinzi wanaomtii aliyekuwa kiongozi wa taifa hilo Blaise Campaore aliyeng'atuliwa mamlakani.
Hakuna majeraha yalioripotiwa lakini kumedaiwa kuwepo kwa hali ya wasiwasi huku maduka yakifunga biashara mapema na raia wengi kuelekea majumbani mwao.
Afisa aliyetangaza kuvunjwa kwa serikali Burkina faso
Maandamano ya ghasia yalioshirikisha kulichoma bunge yalimshinikiza rais aliyehudumu kwa mda mrefu Campaore kung'atuka mamlakani mnamo mwezi Octoba mwaka 2014.
Bwana kafando na luteni kanali Zida walipewa jukumu la kuandaa uchaguzi mpya wa urais mwezi ujao.
Wao pamoja na maafisa wengine walitekwa nyara na walinzi wa RSP, mkuu wa bunge la mpito Moumina Cherrif Sy,alisema katika taarifa.
chanzo BBC

No comments:

Post a Comment

Comments System

disqus

Disqus Shortname

msora

Popular Posts

Header Ads

ad