Thursday, September 17, 2015

Wahamiaji wamiminika Croatia

:
Kroatien Serbien Flüchtlinge bei Tovarnik
Maelfu ya wakimbizi wameanza kumiminika nchini Croatia leo hii baada ya kurushiwa mabomu ya machozi nchini Hungary. Idadi ya wakimbizi hao walioingia Ujerumani jana pia imeripotiwa kuongezeka maradufu.
Wahamiaji nchini Croatia
Maelfu ya wakimbizi wanamiminika nchini Croatia kama njia mpya ya kuingilia Ulaya ya magharibi baada ya kufukuzwa nchini Hungary kwa kurushiwa mabomu ya kutoa machozi pamoja na maji ya kuwasha. Polisi wa Croatia imesema wahamiaji 5,650 wameingia nchini humo leo hii, lakini kundi la mwanzo la wahamiaji lilianza kuingia nchini humo mapema jana. Mamlaka husika zimekuwa zikitumia mabasi pamoja na treni kuwasafirisha na kuwapeleka katika vituo vya wakimbizi.
Mamlaka nchini Croatia zimesema zinaunda bodi maalumu ya kukabiliana na umiminikaji huwo wa wakimbizi. Waziri wa mambo ya ndani Ranko Ostojic ameseme hadi sasa Croatia imeweza kuidhibiti hali hiyo ila alionya kuwa pale wimbi la wakimbizi kutokea Serbia litakapoanza kuingia nchini humo basi hatua mpya zitahitajika kutumika.
Hapa Ujerumani msemaji mkuu wa Polisi amesema leo idadi ya wahamiaji walioingia nchini tangu jana imeongezeka marudufu hadi kufikia watu 7,266. Naye kansela wa Ujerumani Angela Merkel amesema leo kuwa Ujerumani inazingati njia za kuwasaidia wahamiaji kuzoea maisha ya Kijerumani na maadili ya nchi:
CHANZO BBC

No comments:

Post a Comment

Comments System

disqus

Disqus Shortname

msora

Popular Posts

Header Ads

ad