Wednesday, September 16, 2015

Wahamiaji wapata njia mpya Croatia


Kundi la kwanza la wahamiaji limewasili nchini Croatia ,ambayo ni njia mpya ya kuelekea mataifa ya Ulaya yaliopo kaskazini ,siku moja baada ya Hungary kufunga mpaka wake na Serbia.
Takriban wahamiaji 150 walivuka na kuingia katika mataifa ya muungano wa Ulaya kutoka Serbia.
Croatia inasema kuwa iko tayari kuwapokea moja kwa moja ama kuwaelekeza kule wanakotaka kwenda.
Wahamiaji wengi kutoka Syria wana matumaini ya kuelekea Ujerumani.
Masharti mapya yaliowekwa katika mipaka pamoja na mzozo kuhusu kugawana maelfu ya wahamiaji hao kumezua tofauti kubwa miongoni mwa mataifa ya Ulaya.
Mamia ya wahamiaji waliokwama walingojea nje usiku kucha ama katika mahema karibu na mpakawa Serbia na Hungaryc.

No comments:

Post a Comment

Comments System

disqus

Disqus Shortname

msora

Popular Posts

Header Ads

ad