Ugonjwa huo unaambukiza siyo tu kwa kuchanganya damu kama ulivyo ukimwi,lakini pia kwa njia ya mate (busu),ute wa sehemu za siri na pia jasho.
Wataalamu wanasema kuanzia pale unapombukizwa hadi kuchukua uhai wa mtu ni miezi 6 tu. Ni hatari kwelikweli.
Unaua kwa kushambulia ini ambalo hubunguliwa na kuliletea magonjwa mbalimbali iliwemo kansa ya ini na ini kupukutika.
Kwa jijini Dar unaweza kupima HBV kwenye hospitali yoyote kubwa.Kwa upande wa Muhimbili wanachaji 85,000 kwa vipimo; kwani wao wanashauri ufanye na vipimo vingine pia ikiwemo mimengenyo ya ini yaani liver enzymes etc. Ukiwa na Bima ya Afya gharama haziumizi sana.
Hospitali za AAR wanapima kwa gharama ya 25,000/-. Pia maabala ndogo ndogo kadhaa mitaani zinapima, ikiwemo mojawapo ambayo iko jirani na kanisa la Gwajima, Ubungo ambao hupima kwa 10,000.
Ukipima,kuna mambo mawili;kukutwa nao au kukutwa negative.Ukikutwa positive,tafuta ushauri wa daktari.
Na ukikutwa negative unaenda kuchoma sindano za kinga katika hospitali yoyote hasa ya serikali.Kuna malipo.Yanatofautiana kati ya hospitali moja hadi nyingine.Habari njema ni kwamba hivi karibuni serikali imetangaza kupunguza bei ya chanjo hiyo.Lakini ziliadimika sana hapa karibuni.
Utaratibu wa kuchoma
Kinga ya kwanza: Mara baada ya kupima
Kinga ya Pili:Baada ya mwezi mmoja
Kinga ya Tatu:Baada ya miezi 6
Tujipende.Tujitunze.Tukapime.Tujilinde.Magrupu haya yasaidie na afya pia
No comments:
Post a Comment