Hivi karibuni, Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama Barabarani mkoa wa Simiyu, Belensi Alikadi, ambaye pia ni mmiliki wa mtandao huu, alipata fursa ya kuungana na wanaharakati mbalimbali wa masuala ya usalama barabarani, kwenye kuadhimisha Siku ya Mabalozi wa Usalama Barabarani nchini Tanzania.
Tukio hili ambalo lilifanyika kwa mara ya kwanza mkoani Dodoma mwaka huu, liliandaliwa na Mtandao wa Mabalozi wa Usalama Barabarani nchini (RSA Tanzania), mtandao ambao Bw. Belensi ni miongoni mwa wanachama wake.
Katika tukio hilo, aliweza kukutana na wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa ngazi mbalimbali katika Jeshi la Polisi upande wa kikosi cha Usalama Barabarani, sanjari na wale kutoka Mamlaka ya Udhibiti Usafirishaji wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA), ambapo waliweza kubadilishana mawazo kuhusu changamoto kadhaa zinazoikabili sekta ya usafirishaji nchini, na namna ya kukabiliana nazo.
Aidha, kwa kutambuliwa mchango wake katika harakati za usalama barabarani, pamoja na kuikuza taasisi hiyo katika mkoa wa Simiyu, Bw. Alikadi, pia alitunukiwa cheti cha shukrani kwa juhudi zake hizo
Aidha, kwa kutambuliwa mchango wake katika harakati za usalama barabarani, pamoja na kuikuza taasisi hiyo katika mkoa wa Simiyu, Bw. Alikadi, pia alitunukiwa cheti cha shukrani kwa juhudi zake hizo
Pichani, ni Mwenyekiti huyo akiwa katika matukio mbalimbali wakati wa maadhimisho hayo.
Akiwa na cheti cha shukrani alichotunukiwa na Taasisi ya Mabalozi wa Usalama Barabarani nchini, wakati wa hafla ya kuwatambua mabalozi wenye mchango mkubwa kwa taasisi hiyo
Akiwa na cheti cha shukrani alichotunukiwa na Taasisi ya Mabalozi wa Usalama Barabarani nchini, wakati wa hafla ya kuwatambua mabalozi wenye mchango mkubwa kwa taasisi hiyo
Katika viwanja wa Mashujaa mjini Dodoma, ambapo mabalozi walikutana kwa ajili ya maadhimisho ya siku hiyo. Mwenyekiti (mwenye suti nyeusi), akifurahia jambo na mabalozi wenzake.
Mwenyekiti Belensi Alikadi (wa pili kutoka kulia), akiwa na Mkurugenzi wa Usafirishaji kwa njia ya Barabara toka SUMATRA, Johansen Kahatano mwenye shati la drafti, na mabalozi wengine wakati wa maadhimisho hayo
Mwenyekiti Belensi Alikadi (wa pili kutoka kulia), akiwa na Mkurugenzi wa Usafirishaji kwa njia ya Barabara toka SUMATRA, Johansen Kahatano mwenye shati la drafti, na mabalozi wengine wakati wa maadhimisho hayo
Wakati akiwa njiani kuelekea Dodoma, kuhudhuria tukio hilo kubwa na la kihistoria kwa harakati za usalama barabarani nchini.
Akiwa na katibu wa RSA Mkoa wa Simiyu
Tukio hilo liliambatana na michezo mbalimbali. Hapa, Bw. Alikadi akiwa na kikosi cha RSA Yanga, ambacho kilishindana na RSA Simba siku hiyo
Akiwa na Kamanda mpya wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Afande Fortunatus Musilimu wakati wa hafla hiyo
No comments:
Post a Comment