Tuesday, September 19, 2017

RPC MARA AHIDI USHIRIKIANO NA ASKARI WA SERENGETI



na Berensichina,bunda,sept20,2017,Rpc Mara ahidi ushirikiano na askari wa hifadhi ya Serengeti.
kamanda wa polisi mkoa wa mara kamishina msaidizi wa polisi jafari mohamed amesema jeshi la polisi mkoani mara litahakikisha linashilikiana na askari wa hifadhi ya taifa ya serengeti katika kuhakikisha wanakomesha vitengo vya ujangili katika hifadhi hiyo,
kamanda jafari ameyasema hayo mara baada ya kumalizika kwa kikao kazi kilichofanyika wilayani bunda ambacho kimewahusha wahifadhi toka hifadhi ya taifa ya serengeti waendesha mashitaka  wakuu wavitengo vya ulinzi wa wanyamapori na ofisi ya mwandesha mashitaka mkoa wa mara lengo likiwa ni kuweka mkakati namna ya kupambana na ujangili,
akizungumza kwa niaba ya wahifadhi wa hifadhi hiyo,mhifadhi emanuel matungwa amesema changamoto ya ujangili katika hifadhi hiyo ni kubwa kwani kila kukicha majangili wanabuni mbinu mpya hivyo jitihada za pamoja zinahitajika katika kupambana na vitendo hivyo,
kwa upande wake wakili wa serikali mwandamizi toka  wa mkoani mara anisus kahindura,amesema ofisi yake imejipanga ili kuhakikisha kesi za nyara zinamalizika mapema ili kuondoa msongamano wa kesi hizo mahakamani

No comments:

Post a Comment

Comments System

disqus

Disqus Shortname

msora

Popular Posts

Header Ads

ad