Sunday, September 23, 2012

Kushuka kwa zao la pamba chanzo chatajwa


NA Berensi Alikadi-Bunda.

IMEELEZWA kuwa  ukosefu wa mitaji kwa wakulima ,usimamizi imara wa watalaam na utashi wa kisiasa vimekuwa vikichangia kushuka kwa uzalishaji wa zao la pamba wilayani Bunda kila mwaka.

Hayo yamesemwa jana na washiriki wa mkutano wa kuboresha kilimo cha pamba katika wilaya hiyo uliofanyika katika ukumbi wa Serengeti Resort chini ya uneyekiti wa mkuu wa wilaya hiyo Joshua Mirumbe.

Wakichangia mada katika mkutano huo baadhi ya wadau na wakulima wa zao hilo wamedai wakulima wengi hawana mitaji ya kuendeleza zao hilo na kwamba wengi wao wakishauza pamba hutumia pesa na kuzimaliza anbapo wengi wao hukosa hata pesa ya kununua pembejeo za msimu ujao.


Mkaguzi wa bodi ya pamba katika wilaya za Bunda na Serengeti,Igoro Maronga alisema kuwa suala la kilimo cha pamba sasa hivi kimekosa usimamizi kuanzia kwa maafisa ugani hadi kwa wanasiasa ambao pia wamekuwa halitilii maanani sana licha ya kufahamu kuwa ndilo zao pekee linalowapa tija wapiga kura wao.

Igoro alibainisha kuwa  ukiukwaji wa masharti  ya kanuni kumi za kilimo cha zao hilo,mbegu kutochanganywa vizuri viwandani na kutoweka mbolea za samadi mashambani kimekuwa chanzo kikubwa cha wakulima kupata mazao hafifu.

Naye Daudi Iramba afisa kilimo wa kata ya Hunyari alisema kuwa kumekuwepo na tabia ya baadhi ya makampuni kuunda vikundi vya wakulima vijijini bila kuwahusisha wataalam jambo ambalo limkuwa likiwapa shida maafisa ugani walioko vijijini  katika kufanya kazi na vikundi hivyo.

Akizugumza kwa niaba ya wakulima wa pamba,mkulima mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Mayaya alisema kuwa dawa nyingi wanazopelekewa wakulima kwa ajili ya zao hilo ni zile ambazo hazina ubora na kwamba yapo makampuni kama vile Olam,Alliance zilichangia pia mazao kuharibika na kwamba ni vema serikali ikariangalia hilo kwa upana zaidi.

‘’Changamoto kubwa inayotukabiri sisi licha ya hayo ni pamoja na wakulima kuchanganya mazao na ni vema wakulima wakawa wanapatiwa mafunzo ya mara kwa mara ili waweze kuwa na elimu ya kutosha maana hata hawa maafisa ugani wengine hawawafikii wakulima ipasaavyo’’alisema mkulima huyo.

Akifungua mkutano huo wa siku moja mkuu wa wilaya hiyo Joshua Mirumbe alisema lengo la mkutano  huo ni kuweka mkakati wa pamoja wa kuboresha zao la pamba ambalo ndilo zao la biashara kwa wilaya hiyo ambapo hivi sasa uzalishaji wake unashuka kila mwaka .

Mirumbe alisema kuwa kazi ya watumishi yaani maafisa ugani,makampuni ni kutoa elimu kwa wakulima kuhusu kilimo cha kisasa cha zao hilo na kwamba ndiyo maana ameitisha mkutano huo ili aweze kuwakutanisha wadau wa kilimo,wakulima na watalam kwa ajili ya kuweka mkakati wa pamoja.

Alisema kuwa katika msimu wa mwaka huu wilaya hiyo ilikuwa ikusanye  kilo million 10 lakini kutokana na ugonjwa ulizikumba kata za igundu na Namhura wilaya imefanikiwa kukusanya hadi sasa jumala ya kilo million 8 na kwamba huenda hali ikapamba kutokana na kwamba msimu bado unaendelea.

Mkutano huo umeshirikisha wadau wa kilimo, wakulima bora, maafisa ugani,wawakilishi wa makampuni,maafisa tarafa watendaji wa kata na waandishi wa habari.

Mwisho

No comments:

Post a Comment

Comments System

disqus

Disqus Shortname

msora

Popular Posts

Header Ads

ad