NA Berensi Alikadi-Bunda
SERIKALI wilayani Bunda
imewaasa wanafunzi waliohitimu elimu ya kidato cha nne kutobweteka na elimu
waliyopata badala yake watambue kuwa bado wanalojukumu kubwa la kusonga mbele
kielimu.
Kauri hiyo imetolewa jana na
mkuu wa wilaya hiyo Joshua Mirumbe katika hotuba yake iliyosomwa na afisa
mifugo na uvuvi wa wilaya hiyo,Masuke Ogwa kwenye mahafali ya sita ya shule ya
sekondari ya Ellys iliyoko katika mamlaka ya mji mdogo wa Bunda.
Alisema kuwa pamoja na
wanafunzi hao kufanya mahafali hayo lakini watambue kuwa kuna kazi kubwa ya
mtihani ambayo wanapaswa kuifikilia kila siku katika maisha yao na akawataka kutumia muda mwingi katika
kujiandaa na mtihani ambao utafanyika hivi karibuni nchini kote.
‘’Niwapongeze kwa kuhitimu
leo lakini naomba msibweteke tambueni kuwa kazi kubwa bado iko mbele yenu huu
ni mwanzo tu mtaenda vyuo vikuu na vyuo vingine nawaomba mjitahidi na muwe
mabalozi wazuri kumbukeni bila elimu hakuna maisha hivyo jitahidini musome kwa bidii
na muepukane na vitendo viovu’’alkisema Masuke.
Awali wakisoma risala ya
kuhitimu masomo yao wanafunzi hao walisema kuwa walianza masomo yao mwaka 2009
wakiwa wanafunzi 215 ambapo wamehitimu wakiwa wanafunzi 175 na kwamba wanafunzi
wengine wameshindwa kuhitimu kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo utoro na
mamba na utovu wa nidhamu.
Akitaoa taarifa ya shule hiyo
kwa wazazi,mkuu wa shule hiyo Mwalimu Feston Onanda alisema kuwa tangia
kuanzishwa kwa shule hiyo mwaka 2005 imekuwa ikifanya vizuri katika mtihani ya
kidato cha pili na cha nne ambapo hadi sasa zaidi ya wanafunzi 48 toka katika
shule hiyo wamefanikiwa kujiunga katika vyuo vikuu na vyuo mbalimbali hapa
nchini.
Alisema kuwa katika kuhakikisha
kiwango cha elimu shuleni hapo kinapanda
shule hiyo imeweka mikakati ikiwa ni pamoja na kusimamia ufundishaji na
kuhakikisha kuwa wanafunzi wanatoa mazoezi ya mara kwa mara,kuhakikisha wanatoa
mitihani ya kila wiki na kufauatilia mahudhulio ya wanafunzi ipasavyo.
Naye mkutugenzi wa shule hiyo
Eliah John Maduhu alisema pamoja na mafanikio hayo bado kuna changamoto kubwa
katika suala la elimu ambazo alizitaja kuwa baadhi ya wazazi kukosa ushirikiano
na shule hivyo kufanya malezi ya wanafunzi kuwa mabaya,baadhi ya watoto
kutoenda masomo na kufanya yao
kutoridhisha.
Hata hivyo Maduhu aliomba
serikali kuzisaidia shule binafsi kwa kuzipatia vifaa kama
vile vitabu na vifaa vya maabara kwa masomo ya sayansi wakati wa mtihani kwani
shule nyingi za binafsi hazipati vitabu na kuzingatia kuwa mitaala hubadirika
siku kwa siku.
Mwisho
No comments:
Post a Comment