Wednesday, April 2, 2014

WADAU WA AFYA SIMIYU WARIDHIA KUTUMIKA MFUMO WA TIBA KWA KADI.



WADAU WA AFYA SIMIYU WARIDHIA KUTUMIKA MFUMO WA TIBA KWA KADI.

Na Berensi Alikadi. Simiyu,

Wadau wa afya katika halmshauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu,  wameridhia kutumika kwa mfumo mpya wa utoaji wa huduma za afya kwa njia ya tiba kwa kadi (TIKA), mfumo unaolenga kupunguza kero ya upatikanaji wa dawa pamoja na vifaa tiba katika vituo vya afya na hospitali.

Wadau hao wamefikia uamuzi huo kwenye washa iliyofanyika kwenye ukumbi wa kanisa katoliki mjini Bariadi.

Mbali na kuridhia kutumika kwa mfumo huo mpya, ambao uko chini ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ( NHIF), wadau hao wamedai  kuwa ili kupatikana mafanikio ya kutumika kwa mfumo huo ni vema  kuwepo kwa usimamizi mkubwa wa fedha za zitakazotokana na huduma hiyo.

Wakiongea kwa nyakati tofauti walisema uanzishwaji wa mfuko wa afya ya jamii Mjini (TIKA),  kutasaidia wananchi kuweza kutibiwa kwa uarahisi kuliko ilivyo sasa ambapo wananchi hao uangaika katika kutafuta fedha za matibabu.

Walifafanua  kuwa mfumo huo wa tiba kwa kadi malengo yake yana faida kubwa kwa wananchi ambao hawana uwezo wa kuweza kumudu gharama za matibabu, ambapo walieleza kuwa usimamizi wa fedha za wanachama wa huduma hiyo ni lazima kuwa mkubwa.

“ tunipongeza serikali kwa kuleta mfuno huu, sisi hatuna shaka ikiwa utaletwa kwa wananchi wetu, kwani unalenga kutatua kero waliyonayo ya kila siku katika kupata huduma za afya, pamoja na hayo ni lazima usimamizi wa fedha za wananchi wetu watakao kuwa wananchama katika mfumo huu, unatakiwa kuwa mkubwa sana ili fedha zao zisitafunwe na wachache” Alisema Selina Deusi.

 Akitoa maelezo ya juu ya faida ya mfumo huo Mwakilishi wa Mkurugenzi mkuu wa Bima ya Taifa ya Afya Elltruder Mbogolo, alisema kuwa lengo la kuletwa kwa mfumo huu, itasaidia kupungua kwa kero za upatikanaji wa dawa pamoja na vifaa tiba katika vituo vya afya na ospitali.

Semina hiyo iliyokuwa imeudhuliwa na wadau mablimabli wakiwemo, viongozi wa dini, wazee maarufu, viongozi wa vyama vya siasa, vijana, madiwani wa halmshauri ya mji, wanawake, pamoja na waremavu, ambapo mfumo wa Tiba kwa Kadi (TIKA) umelenga kutumika katika halmshauri za miji, manispaa pamoja na jiji.

Akifungua washa hiyo kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Simiyu,Katibu Tawala wa mkoa huo,Mwanvua Jirumbi amewataka viongozi wa halimashauri zote za mkoa huo kuhakikisha wanasiamia ipasavyo mradi huo ili mradi huo uweze kuwanufaisha wananchi.

Washa hiyo ya siku moja iliwashirikisha wadau mbalimbali wakiwemo viongozi madhehebu ya dini,makundi ya walemavu na vyama vya siasa.

MWISHO

Washiriki wa washa ya TIKA wakiwa wanafuatilia mada

Washiriki  wa washa ya TIKA wakiwa wanafruatilia mada.

Waandishi wa habari wakifuatilia mada

Waandishi wa habari wa mkoa wa Simiyu wakifuatilia kwa karibu washa ya TIKA.

Tuesday, April 1, 2014

Washiriki wa washa wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa wilaya ya Bariadi

Washiriki wa washa kuhusu mradi wa TIKA wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa wilaya ya Bariadi.

Afisa afya wa wilaya ya Meatu akielezea uzoefu wa wilaya yake kuhusu huduma ya TIKA

Afisa afya wa wilaya ya Meatu,Bi Anna Muleba akitoa maelezo namna wilaya hiyo ilivyofanikiwa katika mradi wa huduma ya TIKA Katika washa hiyo

Makundi mbalimbali yakiwemo yale ya walemavu wa ngozi wakiwa katika washa

 Washiriki toka makundi mbalimbali yakiwemo  ya watu wenye ulemavu wa ngozi wakiwa katika washa ya TIKA.

Ndugu Geofrey Matumaini akitoa mada

Mwezeshaji wa mada ya tatu kuhusu  ubora wa huduma ya afya ya jamii ,ndugu  Geofrey Matumaini akitoa mada kwenye washa hiyo.

Washiriki wakifutilia mada

Washiriki wa washa ya huduma ya TIKA wakisikiliza mada kwa makini  wa kwanza mwenye suti nyeusi ni kuu wa wilaya ya Bariadi Erasto Sima 

Ndugu Derick Ndetabula akitoa mada kwenye washa

Mwezeshaji wa mada ya kwanza kuhusu umuhimu wa TIKA, ndugu Derick Ndetabula akitoa mada kwa washirik.

sekretalieti ikiwa inafutilia mafunzo hayo

Sekretarieti nayo ilikuwa ikifuatilia na kuandika muhutasari wa washa hiyo.

Mwenyekiti wa halimashauri ya mji akiuliza swali

Mwenyekiti wa halimashauri ya mji wa Bariadi,Robert Lweyo akiuliza swali kuhusu huduma ya TIKA katika washa hiyo.

Madiwani na wadau wakifuatilia mafnzo ya huduma ya TIKA

Madiwani wa halimashauri ya mji wa Bariadi wakiwa pamoja na wadau mbalimbali wakifuatilia mafunzo kuhusu huduma ya bima ya TIKA katika ukumbi wa kanisa  katoliki.

Katibu Tawala wa mkoa wa Simiyu akifungua washa ya Mradi wa TIKA

Katibu tawala wa mkoa wa Simiyu,Bi Mwamvua Jirumbi akifungua washa  ya mradi wa tika kwa niaba ya mkuu wa mkoa huo ambaye hakuweza kuhudhulia.

Mwakilishi wa mkurugenzi wa mfuko wa taifa wa bima ya afya akitoa salam za mfuko huo kwa niaba ya mkurugenzi

Mwakilishi wa mkurugenzi wa mfuko wa bima ya afya ,Bi Ellenrtruder Mbogoro akitoa salamu za mfuko huo kwa wadau wa washa ya mradi wa Tika iliyofanyika jana April 1 katika ukumbi wa kanisa katoliki mjini Bariadi.

Mkurugenzi wa halimashauri ya mji wa bariadi akisema neno kwenye washa ya mradi wa Tika

Mkurugenzi wa halimashauri ya mji wa Bariadi,Bi Elika Musika aliyesimama akitoa maelezo kuhusu washa ya huduma ya tiba kwa kadi yaani[TIKA] kwa washiriki wa washa hiyo iliyofanyika jana  April 1/2014 kwenye ukumbi wa kanisa katoriki mjini Bariadi

Comments System

disqus

Disqus Shortname

msora

Popular Posts

Header Ads

ad