Thursday, September 3, 2015

Watu 2 wauawa Bujumbura na wakimbizi waelekea Tanzania


Published in Jamii

Maandamano nchini Burundi
Watu wawili wameuawa katika mji mkuu wa Burundi, Bujumbura kufuatia makabiliano makali ya risasi Jumanne Usiku.
Kumekuwa na machufuko zaidi katika wilaya zilizoadhirika kwenye maandamano ya kupinga uamuzi wa rais Pierre Nkurunziza wa kuwania muhula wa tatu.
Baadhi ya mitaa mjini humo zimezingirwa na maafisa wa ulinzi.
Nchini Tanzania, idadi ya wakimbizi kutoka Burundi, inaendelea kuongezeka kila uchao. Umoja wa Mataifa umesema kuwa wakimbizi mia nne kutoka Burundi huvuka mpaka na kuingia Tanzania kila siku.
Kufikia sasa zaidi ya wakimbizi elfu tisini wamekimbilia nchi jirani ya Tanzania tangu mzozo wa kisiasa kuanza nchini Burundi, Aprili mwaka huu.
Idadi ya watu mashuhuri wanaouawa nchini humo imekithiri katika siku za hivi karibu.BBC
Read more...


No comments:

Post a Comment

Comments System

disqus

Disqus Shortname

msora

Popular Posts

Header Ads

ad