Monday, September 16, 2013

SERIKALI KUENDELEA KULINDA BONDE LA MTO MARA



NA Berensi Alikadi-Serengeti.
16.9.2013
SERIKALI imesisitiza adhima yake ya kuendelea kulilinda bonde la mto Mara kutokana na umuhimu wa bonde hilo kwa nchi za Kenya na Tanzania kiuchumi.
Kauri hiyo ya serikali imetolewa na waziri mkuu Mizengo Pinda wakati alipokuwa akihutubia wananchi  wa Kenya na Tanzania kwenye kilele cha maadhimisho ya Mara day zilizofanyika katika uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine mjini Mugumu wilayani Serengeti mkoani Mara.
Waziri mkuu alisema kuwa  viongozi wanatakiwa kuendelea kuelimisha umma juu ya suala zima la uhifadhi wa mazingira katika mto mara kwani ndiyo njia pekee ya kununusuru bonde hilo.
Alisema kuwa Tanzania inashirikiana na Kenya kwa sababu chemichemi za mto Mara zimeanzia kwenye milima ya Mau nchini Kenya na kupitia katika hifadhi za masai Mara hadi Serengeti kwa upande wa Tanzania.
‘’Tanzania kwa kutambua ukubwa wa jambo hili tumekubali kutii protoko ya kulinda mto Mara na tutauheshimu’’alisema Pinda.
Alifafanua kuwa katika sera ya maji ya mwaka 2002 na sheria usimamizi wa maji ya mwak 2009 vimetambua bonde hilo kwa faida ya vizazi vya sasa na vijavyo hivyo tutumie maji vizuri na tunawahakikishia wenzetu wa Kenya kuwa tutaendelea kuheshimu makubaliano hayo.
Aliongeza kuwa pamoja na bonde hilo kuwepo lakini bado zipo changamoto mbalimbali zinazolikabili ikiwa ni pamoja na uharibifu wa mazingira,kilimo kando kando ya bonde hilo na uchomaji moto ovyo ambavyo aliwagiza viongozi wa maeneo hayo kuhakikisha wanasimamia visitokee tena.
Kwa upande wake naibu waziri wa maji,Mhandisi Binilith Mahenge alisema kuwa lengo kuu la kuanzishwa kwa kamisheni ya bonde la mto Mara ni kuhamasisha jamii katika kuhifadhi mistu na vyanzo vya maji na kwamba hadi sasa jumla ya miradi 122 ya uhifadhi wa mazingira imeanza kutekelezwa.
Awali akimkaribisha waziri mkuu kuongea na wananchi,mkuu wa mkoa wa Mara John Tupa alisema kuwa pamoja na mambo mengine sherehe hizi pia zinahusha tukio kubwa la wanyama aina ya nyumbu ambao uhama makundi kwa makundi toka hifadhi ya masai Mara na kuja katika hifadhi ya Serengeti.
Mwisho

Sunday, September 1, 2013

Kamanda Makuyu Magai ambaye aliamua kuacha wizi na kujisalimisha polisi

Makuyu Magai  mkazi wa Nyakato Maziwa  katika manispaa ya Musoma  ambaye aliamua kujisalimisha polisi na kuahidi kuacha wizi mara baada ya kuyoka gerezani 

MAKUYU MAGAI---NILIACHA WIZI BAADA YA KUHUBILIWA GEREZANI.


-Aliamua kwenda kujisalimisha polisi baada ya kutoka gerezani.
Na Berensi Alikadi.
1.9.2013
MAKUYU Magai ni mkazi wa mtaa wa Nyakato katika manispaa ya Musoma,alizaliwa mwaka 1973 huko katika kijiji cha Murangi wilaya ya Butiama mkoani Mara.
Baada ya kuhitimu masomo yake ya kidato cha nne katika shule ya sekondari Somanya  iliyoko katika kijiji cha Mugango wilaya hiyo ya Butiama mwaka 1993 aliamua kufanya shughuli mbalimbali za ujasiliamali baada ya matokeo yake kutokuwa mazuri hivyo kushindwa kuendelea na masomo ya juu.
Mnamo mwaka 1996 aliamua kwenda mjini Musoma na kuweka makazi yake mtaa wa nyakato maziwa ambapo aliamua kuanzisha ukumbi wa kuonyesha picha ambayo ndiyo shughuli ambayo ilikuwa ikimpatia kipato.
Magai anasema akiwa katika shughuli hiyo alishawishiwa na baadhi ya wezi ambao walikuwa wakiiba vitu mbalimbali na kumuuzia  kazi ambayo aliianza mwaka 2000.
Anasema baada ya kuendelea na shughuli hiyo hatimaye aliangukia kwenye mikono ya dora baada ya wezi waliokuwa wakiiba kukamatwa na kumtaja yeye kuwa ndiye alikuwa wakala mkubwa wa kununua vitu vya wizi ambapo alikamatwa mwaka huohuo wa 2000 na kupelekwa polisi ambako aliandaliwa mshitaka na kupelekwa mahabusu.
Baada ya kupelekwa gerezani na kuwasimulia wenzake kilichompeleka humo alipata waalimu ambao walimufundisha namna ya kuiba vitu vikubwa na namna gani ya kijihami na kumshauri aachane na kununua vitu vya wizi.
Baada ya kushawishiwa nililianza kufanya matukio mbalimbali ingawa  ingawa sikuweza kukamatwa na kesi hizo,mfano niliwahi kwenda kwenye duka la kituo cha mafuta na kumshawishi mlinzi aache kazi na kwamba nitampeleka sehemu nyingine ili aweze kupata kazi nzuri.

Siku iliyofuata nilienda kumtembelea mlinzi huyo na kumkuta amelala kesho yake tulienda na wenzangu usiku tukafungua tukaiba simu zote,matukio yangu yalikuwa ya kwenda kuwashawishi walinzi na kuwapa pesa ili sisi usiku tukaibe na kwa hili nataka nikwambie hakuna mlinzi ambaye siyo mwizi.
Makuyu anaeleza kuwa walipokuwa wakitoa vitu vya wizi mlinzi pia alikuwa akipata mgawo wake na kwamba kitendo cha kufungua duka na kuhamisha bidhaa kilikuwa ni cha muda mfupi sana.
Bidhaa tulizokuwa tukiiba tulikuwa tukienda kuwauzia wenye maduka na pia fahamu kuwa hata hawa wafanya biashara wa maduka ni wezi hili nalithibitisha hata kama nikiambiwa kutoa ushuhuda nitatoa ndiyo maana tulikuwa hatupati shida ya kuuza vitu vyetu vya wizi.
Makuyu anasema akiwa gerezani alifanikiwa kudhaminiwa lakini licha ya kupata dhamana hakuweza kukaa uraiani kwa amani kwani kila tukio baya la wizi lilipokuwa likitokea polisi walienda kumkamata hali ambayo ilimyima amani.
Mnamo tarehe 26/12/2009 alimpiga mtu mmoja ambaye aliwahi kumtukana na kisha akakimbilia Mwanza na kwamba siku hiyo walipokutana alimua kumpiga  na mtu huyo alikwenda kuripoti kituo cha polisi na kesho yake polisi walikwenda kumkamata na walipomfikisha kituoni  kama kawaida yao walimbambikiza kesi ya unyanga’nyi  wa kutumia silaha na kupatikana na bangi.
Niliendelea na kesi hiyo ambayo ilikuwa chini ya hakimu Richard Maganga lakini baada ya kuona haiendi vizuri niliandika barua ya kumtaka ajiondoe katika kesi hiyo lakini alikataa  na tarehe mwezi wa nane mwaka 2010.
Anasema ilipofika mwezi wa tisa tarehe 9 mwaka huohuo hakimu huyo alimufunga tena kifungo cha miaka 30 jera na kuchapwa viboko 24 kwa kosa la unyanga’nyi hata hivyo sikuridhika na hukumu hiyo ambapo nilikata rufaa ambayo ilinitoa mnamo tarehe 31 mwezi wa tano mwaka huu.
Makuyu anaeleza kuwa baada ya baada ya kuhukumiwa na Maganga alipelekwa katika gereza la Butimba jijini Mwanza na kwamba akiwa huko alijifunza mambo mengi na aliona mambo mwengi ambayo yalimusukuma kabisa kuacha wizi.
Kwakweli baada ya kurudi niliamua kwenda polisi tarehe 21.8.2013 na kuonana na mkuu wa upelelezi wa wilaya ambapo nilimuambia kuwa kuanzia sasa mimi ni raia mwema na pia nimeamua kuwatafuta nyie waandishi ili mfikishe taarifa hizi kwa jamii kuwa mimi siyo mwizi tena,
Niliamua mwenyewe kwenda polisi kujisalimisha na kwa hili sina shaka maana naamini mungu ananilinda maana hata kesi yangu nilishinda kwa nguvu zake maana hata wakili wa serikali aliyekuwa ananitetea alisema hawahi kuona kesi kama yangu,yaani mtu unafungwa mara mbili kwa mwezi mmoja.pasipo hata kujitetea.
Natoa wito kwa vijana wa nchi hii wabadirike kama nilivyobadirika mimi nimejionea mambo mengi gerezani,mfano vijana wa Musoma waache vikundi walivyonavyo kama vile Jamaica mokazi,midomo ya furu na uchakavu na watambue kuwa gereza siyo mahali pa kuishi na unapotoka gerezani hukai kwa amani kutokana na jamii kutokuamini.
Makuyu anabainisha wenzake waliokuwa wakifanya nao kazi hiyo ambao wameshauwawa kuwa ni pamoja na  Sauri Magembe Bwire maalufu kwa jina la Bebeto.Devis Manyama,Jumanne Mjungu na Stivin Wiliam ambao wote kwa hivi sasa ni marehemu na walikufa kwa kupigwa na wananchi
Lakini pia anamuomba rais Kikwete asitoe msamaha kwa wafungwa wa miaka mitano na kurudi chini kwani hao wanakuwa hawajifunza kitu chochote na ndio maana wakiachiwa huanza tena vitendo vya uharifu.
Huyo ndiye Makuyu Magai aliyeamua kijisalimisha polisi baada ya kutoka gerezani.
MWISHO.

KAMUAHANDA, DAMU YA MWANGOSI BADO INAKULILIA.


Na Berensi Alikadi.
30/8/2013
LEO ni mwaka mmoja tangia kifo cha aliyekuwa mwandishi wa kituo cha chanel ten mkoani Iringa Marehemu Daudi Mwangosi.
Kama tunavyofahamu Mwangosi aliuwawa na polisi sept 2mwaka 2002 akiwa kazini huko katika kiijiji cha Nyaroro wilayani Mfindi mkoani Iringa ambako alikuwa amekwenda kuandika habari za mkutano wa chama cha demkorasia na maendeleo [Chadema].
Siku hiyo Mwangosi alikwenda pale kijijini akiwa katika majukumu yake ya kikazi ambako alitaka kuwahahabarisha wananchi kilichosemwa katika mkutano huo lakini maskini hakuweza kutimiza lengo lake na badala yake polisi kwa amri ya Kamuhanda walimugeuza uji.
Hakuna ubishi katika hilo kuwa mwandishi huyo hakuuwawa na polisi kwani taarifa za awali toka kwa waandishi wenyewe wa mkoa wa Iringa zinasema kuwa aliyekuwa kamanda wa polisi mkoa huo Michael Kamuhanda ambaye bado serikali inamkumbatia aliitisha mkutano na waandishi wa habari ofisini kwakwe  na katika mkutano huo baada ya kueleza adhima yake ya kuuzuia mkutano wa chadema,marehemu mwangosi alionekana kuumuliza maswali mengi ambayo yalionekana kumukera kamanda huyo.
Maswali ya Mwangosi kwa kamanda  huyo wa polisi huenda ndiyo yaliongeza chuki nap engine kuongeza hasira ya siku nyingi ambayo alikuwa nayo dhidi yake na hivyo akamuweka kiporo.
Taarifa zinaonyesha kuwa mara baada ya mkutano huo baadhi ya askari polisi waliwazuia waandishi wasiende kwenye mkutano huo jambo ambalo kwa mwandishi ni kosa kwani yeye pia anatakiwa kutimiza majukumu yake kama polisi walivyokwenda kwenye mkutano huo.
Habari zilieleza kuwa baada ya waandishi wa habari kufika katika eneo la kijiji cha Nyaroro na kufanikiwa kukusanya habari  walielekea kwenye eneo la kusini mashariki kupitia barabara kuu  Dar-Tunduma mahali ambalo ndipo alipouwawa mwangosi
Katika eneo hilo polisi waliwapiga waandishi wa habari na viongozi wa chadema pasipo sababu waandishi waliopigwa ni pamoja wale waliokuwa wakiandikia magazeti ya nipashe,mtanzania,Tanzania daima lakini adhima yao kuu ilikuwa kumua Mwngosi jambo ambalo walilitimiza pasipo kuacha shaka.
Siku hiyo ya tukio wakati baadhi ya waandishi walipokuwa wakipigwa na polisi, Mwangosi alimukimbilia kamanda Kamuahanda na kumuomba awamuru polisi  wake waache kumpiga mwandishi wa gazeti la nipashe Godfrey Mushi lakini hakumuelewa wala kumusikiliza  na badala yake walimushika na kumugeuzia kibao na kuanza kumpiga hadi askari mwingine alipomupiga na bomu tumboni lililosambaza mwili wake huku kamanda Kamuahanda akishuhudia na huo ndio ukawa mwisho wa maisha  ya Daudi Mwangosi.
Leo tunapotimiza mwaka mmoja tangia kifo cha mwandishi huyo hatuna budi kutafakali vitendo vya kikatili vinavyofanyiwa waandishi wa habari huku serikali ikiangalia pasipo kuchukua hatua.
Hivi ndugu msomaji hata wewe una kila sababu ya kujiuliza kulikuwa na sababu gani ya kuwazuia waandishi wa habari kwenda kwenye huo mkutano ,walikuwa na kosa gani hata kama wangepiga picha.
Katika hali ya haraka Napata picha kuwa siku hiyo polisi walikuwa na ajenda yao ya siri kama kawaida yao na ndio maana hawakutaka waandishi wafike huko na pingine huenda walipanga kabisa kuwauwa viongozi wa chadema na kuwepo kwa waandishi kulizima adhima hiyo na ndio maana hasira zao walimalizia kwa kuwapiga na kumuua Mwangosi.
Waandishi wa habari siku zote wako kazini kwa kufuata taratibu zao na namna walivyofundishwa kufanya kazi na wala hawafanyi kazi zao kwa kuamuliliwa na polisi lakini cha kushangaza sasa polisi wamekuwa wakiwakiwaingilia na hata kuwazuia kufanya kazi jambo ni ukiukwaji wa katiba ya nchi ibara ya 18.
Kwa miongo mingi sasa wananchi wamekuwa wakishuhudia namna waandishi wanavyonyanyaswa na jeshi la polisi,wako waliowahi kupigwa,kungo’lewa kucha,kumwagiwa tindikali kuporwa vifaa vyao vya kazi kama kamera na sasa mwaka jana dunia imeshuhudia waziwazi jeshi hili chini ya kiongozi aliyekabidhiwa kuuongoza mkoa akisimamia mwandishi anauwawa kwakweli inatisha na inaumiza sana.
Ni waandishi hawa hawa ambao kila siku polisi wanapokamata majambazi wale wasiowapa rushwa na vitu vile ambavyo huwa hawana mgawo huwaita na kuuza sura zao ili jamii iwaone kama kweli wanafanya kazi kumbe wengi wao ni mafisadi wakubwa.
Kilichonishangaza zaidi ni pale serikali hadi leo imemukingia kifua Kamuahanda huku kesi hiyo akipewa askari mdogo ambaye pia kila kukicha polisi wenzake wamekuwa wakimfanyia maagizo hata wakati wa kumpeleka mahakamani jambo linaloonyesha dhahili kuwa mauaji ya Daudi Mwangosi yalipangwa na wala si vinginevyo.
Nilitegemea sana rafiki yangu Nchimbi atamuchukulia hatua ya kinidhamu Kamuahanda lakini matokeo yake akahamishiwa makao makuu ya polisi ili kumficha huko wananchi wasifahamu kinachoendelea zaidi na hadi leo imekuwa kimya hakuna hata kiongozi wa polisi wala serikali wanaoweza kuzungumzia suala hili licha ya tasinia hii pia kuwa na wizara kamili.
Jeshi la polisi liliundwa kwa ajili  ya kulinda raia na mali zao wakiwemo waandishi wa habari lakini cha kushangaza leo jeshi hili limekuwa kinala wa kuuwa na wa kwanza pia kukimbilia kukanusha kwa kutumia vyombo vyao vya serikali kama vile TBC na magazeti ya uhuru na mzalendo ili kuwapoteza wananchi pasipo kufahamu kuwa wananchi leo hawadanganyiki.
Wakati leo wanahabari hapa nchini wanaungana na watanzania wengine katika kukumbuka mauji haya ya kinyama aliyofanyiwa Mwangosi hatuna budi kulaani kwa nguvu zetu na kulitaka jeshi la polisi liache kutumika kiasiasa.
Hatuna budi kuitaka serikali itamuke ni lini itawalinda waandishi wa habari wawapo kazini na ni lini polisi wataacha uhasama na waandishi wa habari maana kila kukicha chuki kati ya waandishi na jeshi hili inazidi kuongezeka kutoka na vitendo vya uonevu wanavyofanyiwa wakiwa kazini.
Polisi watambue kuwa waandishi ni sehemu ya jamii ya kitanzania nayo ina haki sawa katika nchi hii na pia inafahamu maovu mengi na kama siku ikiamua kumwaga mboga basi hapo ndipo kutakapokuwapo kilio na kusaga meno.
Waache vitisho na kuingailia uhuru wa habari waache waandishi wafanye kazi zao kama tasnia uhuru wakumbuke hayo mabomu waliyotumia kumuua Mwangosi ni kodi yetu wananchi wakiwemo waandishi wa habari.
Leo familia ya Daudi Mwangosi inataabika lakini Kamuhanda anaishi maisha mazuri tena ameongezewa cheo kumbe polisi akiuwa mwandishi anaongezewa cheo na gari zuri la kiyoyozi hakuna hatua zilizochukuliwa na lakini naamini mungu yupo na damu ya Mwangosi itaendelea kumulilia siku hadi siku.
Waandishi wa habari leo hawana uhuru wa kufanya kazi katika nchi yao,hawana uhuru wa kuhudhulia hata mikutano ya kisiasa hususa ni ile ya vyama vya upinzani kasoro ya chama cha mapinduzi ambacho hata kama kikikosea polisi husema amina’’.
Ndiyo maana waandishi sasa tunaomba katiba ijayo waandishi watambuliwe na uwe mhimili kamili kama mihimili mingine kwani wana mchango mkubwa katika nchi hii na tunataka tuachwe huru na hatutaki kuingilia na polisi na kupigwa mabomu pasipo sababu.
Tunataka polisi waache kutugeuza kama kiti moto bali watautambue na watuheshimu kama wanavyoheshimu hao wanaowatuma kutupiga mabomu na wafahamu kuwa hiyo kazi ina mwisho na mwisho wao siku zote huwa ni mbaya na wengi wao wamekuwa wakikimbilia kuomba msaada kwa waandishi ili waweze kuandikiwa mambo yao pindi wakwamapo kulipwa mafao yao ya kusitaafu uhamisho nk.
Sisi wote ni watanzania wala polisi wasijione wao wako juu ya sheria na kutukandamiza lazima waandishi wote tuungane kwa nguvu zetu na tukatae biashara hii ya polisi kutufanya sambusa kila mtu ana haki ya kutimiza wajibu wake kikazi hivyo hata mwandishi kuhudhulia mkutano ni haki yake na tunataka polisi msituchagulie cha kuandika nyie milisomea mguu pande na sisi tulisomea kuandika hivyo tuacheni tulivyo na kalamu zetu na nyie na bunduki zenu lakini mkijua hiyo ni kodi ya walalahoi na siyo ya kwenu.
Tunayo kila sababu ya kulaani vitendo viovu dhidi ya polisi wanavyofanyiwa waandishi kumbukeni haya manyanyaso hayakuanzia kwa Mwangosi tu bali wako wengi akina Katabalo na wengine mnaowafahamu sasa lazima tusema manyanyaso ya polisi dhidi ya wanahabari sasa basi.
Damu ya Mwangosi iliyomwagika akiwa anatetea kazi yake iwe chachu kwa waandishi wote hapa nchini,tutafakali kwa pamoja juu ya maisha yetu ya kila siku na namna tunavyowindwa ili roho zetu ziondoke,lazima tumukumbuke mwenzetu kwa uchungu mkubwa na tuongeze msikamano katika kudai haki yetu ya kupata habari mahali popote.
Kamwe ushujaa wako hautasaulika katika tasinia ya habari kila kizazi naamini kitasoma historia yako ambayo itaandikwa kila kukicha na wapenda haki sisi tunaamini ulikufa katika haki na tutaendelea kukumbuka kila siku na mchango wako katika habari utakumbukwa daima siku zote.
Lakini kwa jeshi la polisi hususa ni kamanda Kamuhanda lazima atatmbue kuwa kila kukicha damu ya Mwangosi itaendelea kumulilia kila siku maana bila yeye Mwangosi bado tungekuwa naye.
Tunasema Mwangosi amepumzika lakini tuliobaki tutaendeleza mambano ya kutetea uhuru wa kupata habari pasipo kuogopa vitisho vya polisi.
Pumzika kwa amani Kamanda Mwangosi.



KAMUAHANDA, DAMU YA MWANGOSI BADO INAKULILIA


.
Na Berensi Alikadi.
30/8/2013
LEO ni mwaka mmoja tangia kifo cha aliyekuwa mwandishi wa kituo cha chanel ten mkoani Iringa Marehemu Daudi Mwangosi.
Kama tunavyofahamu Mwangosi aliuwawa na polisi sept 2mwaka 2002 akiwa kazini huko katika kiijiji cha Nyaroro wilayani Mfindi mkoani Iringa ambako alikuwa amekwenda kuandika habari za mkutano wa chama cha demkorasia na maendeleo [Chadema].
Siku hiyo Mwangosi alikwenda pale kijijini akiwa katika majukumu yake ya kikazi ambako alitaka kuwahahabarisha wananchi kilichosemwa katika mkutano huo lakini maskini hakuweza kutimiza lengo lake na badala yake polisi kwa amri ya Kamuhanda walimugeuza uji.
Hakuna ubishi katika hilo kuwa mwandishi huyo hakuuwawa na polisi kwani taarifa za awali toka kwa waandishi wenyewe wa mkoa wa Iringa zinasema kuwa aliyekuwa kamanda wa polisi mkoa huo Michael Kamuhanda ambaye bado serikali inamkumbatia aliitisha mkutano na waandishi wa habari ofisini kwakwe  na katika mkutano huo baada ya kueleza adhima yake ya kuuzuia mkutano wa chadema,marehemu mwangosi alionekana kuumuliza maswali mengi ambayo yalionekana kumukera kamanda huyo.
Maswali ya Mwangosi kwa kamanda  huyo wa polisi huenda ndiyo yaliongeza chuki nap engine kuongeza hasira ya siku nyingi ambayo alikuwa nayo dhidi yake na hivyo akamuweka kiporo.
Taarifa zinaonyesha kuwa mara baada ya mkutano huo baadhi ya askari polisi waliwazuia waandishi wasiende kwenye mkutano huo jambo ambalo kwa mwandishi ni kosa kwani yeye pia anatakiwa kutimiza majukumu yake kama polisi walivyokwenda kwenye mkutano huo.
Habari zilieleza kuwa baada ya waandishi wa habari kufika katika eneo la kijiji cha Nyaroro na kufanikiwa kukusanya habari  walielekea kwenye eneo la kusini mashariki kupitia barabara kuu  Dar-Tunduma mahali ambalo ndipo alipouwawa mwangosi
Katika eneo hilo polisi waliwapiga waandishi wa habari na viongozi wa chadema pasipo sababu waandishi waliopigwa ni pamoja wale waliokuwa wakiandikia magazeti ya nipashe,mtanzania,Tanzania daima lakini adhima yao kuu ilikuwa kumua Mwngosi jambo ambalo walilitimiza pasipo kuacha shaka.
Siku hiyo ya tukio wakati baadhi ya waandishi walipokuwa wakipigwa na polisi, Mwangosi alimukimbilia kamanda Kamuahanda na kumuomba awamuru polisi  wake waache kumpiga mwandishi wa gazeti la nipashe Godfrey Mushi lakini hakumuelewa wala kumusikiliza  na badala yake walimushika na kumugeuzia kibao na kuanza kumpiga hadi askari mwingine alipomupiga na bomu tumboni lililosambaza mwili wake huku kamanda Kamuahanda akishuhudia na huo ndio ukawa mwisho wa maisha  ya Daudi Mwangosi.
Leo tunapotimiza mwaka mmoja tangia kifo cha mwandishi huyo hatuna budi kutafakali vitendo vya kikatili vinavyofanyiwa waandishi wa habari huku serikali ikiangalia pasipo kuchukua hatua.
Hivi ndugu msomaji hata wewe una kila sababu ya kujiuliza kulikuwa na sababu gani ya kuwazuia waandishi wa habari kwenda kwenye huo mkutano ,walikuwa na kosa gani hata kama wangepiga picha.
Katika hali ya haraka Napata picha kuwa siku hiyo polisi walikuwa na ajenda yao ya siri kama kawaida yao na ndio maana hawakutaka waandishi wafike huko na pingine huenda walipanga kabisa kuwauwa viongozi wa chadema na kuwepo kwa waandishi kulizima adhima hiyo na ndio maana hasira zao walimalizia kwa kuwapiga na kumuua Mwangosi.
Waandishi wa habari siku zote wako kazini kwa kufuata taratibu zao na namna walivyofundishwa kufanya kazi na wala hawafanyi kazi zao kwa kuamuliliwa na polisi lakini cha kushangaza sasa polisi wamekuwa wakiwakiwaingilia na hata kuwazuia kufanya kazi jambo ni ukiukwaji wa katiba ya nchi ibara ya 18.
Kwa miongo mingi sasa wananchi wamekuwa wakishuhudia namna waandishi wanavyonyanyaswa na jeshi la polisi,wako waliowahi kupigwa,kungo’lewa kucha,kumwagiwa tindikali kuporwa vifaa vyao vya kazi kama kamera na sasa mwaka jana dunia imeshuhudia waziwazi jeshi hili chini ya kiongozi aliyekabidhiwa kuuongoza mkoa akisimamia mwandishi anauwawa kwakweli inatisha na inaumiza sana.
Ni waandishi hawa hawa ambao kila siku polisi wanapokamata majambazi wale wasiowapa rushwa na vitu vile ambavyo huwa hawana mgawo huwaita na kuuza sura zao ili jamii iwaone kama kweli wanafanya kazi kumbe wengi wao ni mafisadi wakubwa.
Kilichonishangaza zaidi ni pale serikali hadi leo imemukingia kifua Kamuahanda huku kesi hiyo akipewa askari mdogo ambaye pia kila kukicha polisi wenzake wamekuwa wakimfanyia maagizo hata wakati wa kumpeleka mahakamani jambo linaloonyesha dhahili kuwa mauaji ya Daudi Mwangosi yalipangwa na wala si vinginevyo.
Nilitegemea sana rafiki yangu Nchimbi atamuchukulia hatua ya kinidhamu Kamuahanda lakini matokeo yake akahamishiwa makao makuu ya polisi ili kumficha huko wananchi wasifahamu kinachoendelea zaidi na hadi leo imekuwa kimya hakuna hata kiongozi wa polisi wala serikali wanaoweza kuzungumzia suala hili licha ya tasinia hii pia kuwa na wizara kamili.
Jeshi la polisi liliundwa kwa ajili  ya kulinda raia na mali zao wakiwemo waandishi wa habari lakini cha kushangaza leo jeshi hili limekuwa kinala wa kuuwa na wa kwanza pia kukimbilia kukanusha kwa kutumia vyombo vyao vya serikali kama vile TBC na magazeti ya uhuru na mzalendo ili kuwapoteza wananchi pasipo kufahamu kuwa wananchi leo hawadanganyiki.
Wakati leo wanahabari hapa nchini wanaungana na watanzania wengine katika kukumbuka mauji haya ya kinyama aliyofanyiwa Mwangosi hatuna budi kulaani kwa nguvu zetu na kulitaka jeshi la polisi liache kutumika kiasiasa.
Hatuna budi kuitaka serikali itamuke ni lini itawalinda waandishi wa habari wawapo kazini na ni lini polisi wataacha uhasama na waandishi wa habari maana kila kukicha chuki kati ya waandishi na jeshi hili inazidi kuongezeka kutoka na vitendo vya uonevu wanavyofanyiwa wakiwa kazini.
Polisi watambue kuwa waandishi ni sehemu ya jamii ya kitanzania nayo ina haki sawa katika nchi hii na pia inafahamu maovu mengi na kama siku ikiamua kumwaga mboga basi hapo ndipo kutakapokuwapo kilio na kusaga meno.
Waache vitisho na kuingailia uhuru wa habari waache waandishi wafanye kazi zao kama tasnia uhuru wakumbuke hayo mabomu waliyotumia kumuua Mwangosi ni kodi yetu wananchi wakiwemo waandishi wa habari.
Leo familia ya Daudi Mwangosi inataabika lakini Kamuhanda anaishi maisha mazuri tena ameongezewa cheo kumbe polisi akiuwa mwandishi anaongezewa cheo na gari zuri la kiyoyozi hakuna hatua zilizochukuliwa na lakini naamini mungu yupo na damu ya Mwangosi itaendelea kumulilia siku hadi siku.
Waandishi wa habari leo hawana uhuru wa kufanya kazi katika nchi yao,hawana uhuru wa kuhudhulia hata mikutano ya kisiasa hususa ni ile ya vyama vya upinzani kasoro ya chama cha mapinduzi ambacho hata kama kikikosea polisi husema amina’’.
Ndiyo maana waandishi sasa tunaomba katiba ijayo waandishi watambuliwe na uwe mhimili kamili kama mihimili mingine kwani wana mchango mkubwa katika nchi hii na tunataka tuachwe huru na hatutaki kuingilia na polisi na kupigwa mabomu pasipo sababu.
Tunataka polisi waache kutugeuza kama kiti moto bali watautambue na watuheshimu kama wanavyoheshimu hao wanaowatuma kutupiga mabomu na wafahamu kuwa hiyo kazi ina mwisho na mwisho wao siku zote huwa ni mbaya na wengi wao wamekuwa wakikimbilia kuomba msaada kwa waandishi ili waweze kuandikiwa mambo yao pindi wakwamapo kulipwa mafao yao ya kusitaafu uhamisho nk.
Sisi wote ni watanzania wala polisi wasijione wao wako juu ya sheria na kutukandamiza lazima waandishi wote tuungane kwa nguvu zetu na tukatae biashara hii ya polisi kutufanya sambusa kila mtu ana haki ya kutimiza wajibu wake kikazi hivyo hata mwandishi kuhudhulia mkutano ni haki yake na tunataka polisi msituchagulie cha kuandika nyie milisomea mguu pande na sisi tulisomea kuandika hivyo tuacheni tulivyo na kalamu zetu na nyie na bunduki zenu lakini mkijua hiyo ni kodi ya walalahoi na siyo ya kwenu.
Tunayo kila sababu ya kulaani vitendo viovu dhidi ya polisi wanavyofanyiwa waandishi kumbukeni haya manyanyaso hayakuanzia kwa Mwangosi tu bali wako wengi akina Katabalo na wengine mnaowafahamu sasa lazima tusema manyanyaso ya polisi dhidi ya wanahabari sasa basi.
Damu ya Mwangosi iliyomwagika akiwa anatetea kazi yake iwe chachu kwa waandishi wote hapa nchini,tutafakali kwa pamoja juu ya maisha yetu ya kila siku na namna tunavyowindwa ili roho zetu ziondoke,lazima tumukumbuke mwenzetu kwa uchungu mkubwa na tuongeze msikamano katika kudai haki yetu ya kupata habari mahali popote.
Kamwe ushujaa wako hautasaulika katika tasinia ya habari kila kizazi naamini kitasoma historia yako ambayo itaandikwa kila kukicha na wapenda haki sisi tunaamini ulikufa katika haki na tutaendelea kukumbuka kila siku na mchango wako katika habari utakumbukwa daima siku zote.
Lakini kwa jeshi la polisi hususa ni kamanda Kamuhanda lazima atatmbue kuwa kila kukicha damu ya Mwangosi itaendelea kumulilia kila siku maana bila yeye Mwangosi bado tungekuwa naye.
Tunasema Mwangosi amepumzika lakini tuliobaki tutaendeleza mambano ya kutetea uhuru wa kupata habari pasipo kuogopa vitisho vya polisi.
Pumzika kwa amani Kamanda Mwangosi.


WANAKIJIJI WADAI KULAWITIA NA KUNAJISIWA KISHIRIKINA


NA Berensi Alikadi,Bunda.
1/9/2013
WANANCHI  vijiji vya kata ya Butimba katika tarafa ya Kenkyombyo wilayani Bunda mkoani Mara wanaishi kwa hofu kubwa kutokana na kuibuka kwa vitendo vya kishirikina katika vijiji hivyo.
Wakiongea na Tanzania daima ilipotembelea vijiji hivyo jana wananchi hao wamedai kuwa kwa muda wa wiki nzima sasa kumekuwepo na vitendo vya kishirikiana ambapo watu wasiofahamika wamekuwa wakienda katika vijiji hivyo majira ya usiku na kuwanajisi wanawake na bila wao kujitambua.
Aidha walifafanua kuwa baada ya watu hao kuwafanyia vitendo hivyo huchukuwa pesa na kuondoka ambapo wao huwa hawajitambui kabisa.
Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Buramba wameliambia Tanzania daima kuwa tatizo hilo siyo kwa akina mama tu bali watu hao ambao kwa lugha ya kijita wanafahamika kama [wafafuti] wamekuwa wakiwalawiti hata wanaume jambo ambalo limezuia hofu kubwa.
‘’Kwakweli Mwandishi hali hii inasikitisha sana watu hawa haifahamiki wanakuja saa ngapi isipokuwa tu asubuhi wewe unakuta umenajisiwa na una mbegu za kiume sasa inashangaza hapo awali walianzia kwa wanawake lakini sasa hata wanaume’’alisema mtu huyo ambaye hakutaka atajwe gazetini.
Diwani wa kata hiyo Ngunya  Msalaba amekiri kuwepo kwa hali hiyo na kwamba mnamo agost 26 mwaka huu majira ya saa tano usiku kaya tano za wafanyakazi wa kiwanda cha kuchambua pamba cha Bulamba walikumbana na dhahama hiyo
Msalaba alisema kuwa baada ya kuwepo kwa matukio hayo waliamua kufanya mkutano wa hadhara katika kijiji hicho ambapo walikubaliana mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwarudisha makwao waganga wote wa kienyeji ambao wamehamia katika vijiji vya kata hiyo.
Alisema kuwa jambo lingine walilokubaliana na pamoja na wageni wote wanaokwenda kufanya kazi katika kiwanda hicho wawe na vitambulisho vinavyotambulika na wavipeleke kwa viongozi wa kijiji hicho.
Sambamba na hilo diwani huyo alidai kuwa wameanzisha jeshi la sungusungu  kwa ajili ya kulinda usiku na mchana ili kama watamuona mtu mgeni waweze kumuhoji.
‘’Lakini pia tumeunda jeshi la sungusungu ambalo litalinda mchana na usiku ingawaje pia ni kazi ya ziada maana watu wenyewe wanakuja usiku kazi ipo mimi sijawahi kusikia jambo hili’’alisema diwani huyo.
Kufutia hali hiyo diwani huyo ametoa wito kwa wananchi hao kuwa na subira wakati wakiendelea kulifanyia uchunguzi suala hilo ambalo alisema linatia shaka maisha ya wananchi wa kata hiyo.
Tatizo hilo la wananchi kuingilia na kunajisiwa kishirikina limeshamili sana katika kipindi cha miaka zaidi ya miwili hasa katika jimbo la Mwibara ambako hivi karibuni wananchi wa vijiji vya Kasahunga walikumbwa na tatizo hilo
Mwisho

Comments System

disqus

Disqus Shortname

msora

Popular Posts

Header Ads

ad