Thursday, May 22, 2014
UZAZI WA MPANGO WAZINDULIWA SIMIYU
NA BERENSI
ALIKADI,SIMIYU
MEI 22,2014,
Imeelezwa
kuwa wanawake tkribani 454 kati ya vizazi
100,000 hufa kila mwaka kutokana na uzazi.
Mganga mkuu
wa mkoa wa simiyu,Dr,Mageda Kihurya mjini Bariadi kwenye uzinduzi wa kampeni ya
uzazi wa mpango ngazi ya mkoa iliyojulikana kama nyota ya kijani.
Alisema
tafiti zinaonyesha kuwa upo uhusiano mkubwa
kati ya matumzi ya uzazi wa mpango na afya ya mama na mtoto na kwamba
matumizi haya yanawez kupunguza vifovitokanavyo na na uzazi kwa asilimia 44 na kupunguza vifo
vya kupungza vifo vya watoto kwa asilimia
10-12.
Dr Mageda
alisema hiyo ni kwa sababu ya uzazi wa
mpango humuwezesha mama kupumzika kati ya mimba moja hadi nyingine na pia
humsaidia mama kuepuka mimba zisizotarajiwa na hivyo kupunguza
tatizo la utoaji mimba holela
Aidha
alifafanua kuwa sense ya watu na makazi ya mwaka 2012 inaonyesha kuwa nchi yetu
ina idadi ya ya watu milioni 45 ikiwa ni
ongezeka la kasi,idadi isiyowiana na
ongezeko la pato la kiuchumi la nchi yetu hali inayotulazimu sisi sote kuongeza
juhudi katika kuwekeza kwenye huduma za jamii kama vile elimu na afya.
Kwa upande
wake mwakilishi wa shirika la misaada la Marekani USAID kupitia chuo kikuu cha John Hopkins,,Dr Rose Madida
aliwataka wanawake kuzaa kwa kufuata uzazi wa mpango na kuachana na mila potofu
kuwa kuzaa watoto wengi utajili.
Baadhi ya
wananchi wanaotumia uzazi wa mpango mkoani hapa wamelitoa ushuhuda wao na
kueleza kuwa uzazi wa mpango ni njia sahihi ya kumsaidia mtu kujua namna
atakavyoweza kuituza familia aliyonayo.
Akizindua
mpango huo mkuu wa mkoa wa Paschal Mabiti pamoja na kuupongeza mpango huo
ameziagiza halimashauri za wilaya mkoani humo kupanga bajeti kwa ajili ya
kuusaidia mpango huo na kwamba hata serikali kuu itahakikisha inafanya hivyo.
Uzinduzi huo
ulioenda sambamba na upimaji wa virusi,ufungaji wa uzazi na mafunzo ya uzazi
salama toka katika mashirika mbalimbali kama vile umati,Amreef na
Ingenderheath.
mwisho
Sunday, May 18, 2014
SERIKALI KUTOIPA KAZI YA KUCHIMBA MABWAWA,KAMPUNI YA NYAKILANG’ANI
NA MWANDISHI WETU MEATU SIMIYU,MEI 18,2014.
serikali imesema kuanzia sasa haitaipa kampuni ya ujenzi Nyakirang’ani
ya mkoani mara kazi yeyote ya kuchimba mabwawa baada ya kampuni
kushindwa kukamilisha kazi za mabwawa mbalimbali hapa nchini.
kauli hiyo ya serikali imetolewa wilayani meatu mkoani simiyu na naibu
waziri wa maji,amosi makala mara baada ya kutembelea bwawa la mwanjoro
ambalo lilikuwa likijengwa na kampuni hiyo.
amesema mkandarasi huyo ameonyesha kiwango cha chini katika ujenzi wa
mabwawa anayopewa na kwamba kuanzia sasa hatapewa kazi yeyote ya
ujenzi wa mabwawa na wizara hicho hapa nchini kwani amekuwa
mkandarasi mbabaishaji na asiye na uwezo licha ya kupewa kazi hizo na
wizara.
‘’Nimefika mwenyewe nimejionea hali halisi ilivyo na nimeacha watalaam
wa wizara yangu waweze kufanya tathimini na watuleteea kabla
hatujasoma bajeti na mkandarasi huyu nimesema yeye na wizara yetu sasa
basi hatuwezi kupata hasara kwa kuwavumilia wakandarasi
wababaishaji.’’alisema Makala
mkuu wa wilaya hiyo.Rose mary kirigini
alimueleza naibu waziri huyo bwawa hilo lilianza kujengwa tangia mwaka
2009 hadi sasa na kwamba taarifa imekuwa ikionyesha kuwa limekamilika
kwa asilimia 80 jambo ambalo si kweli.na kwamba wakati umefika sasa
,kwa wananchi wa vijiji hivyo kulitumia bwawa hilo kwani wametaabika
kwa muda mrefu sana
Awali mhandisi wa maji toka sekretalieti ya mkoa,Gibson Kisaka amesema
hali ya upatikanaji wa maji katika mkoa huo haitoshi kutokana na
vyanzo vingi kuwa na maji yenye madini ya frolide na kwamba
wanaangalia uwezo wa kuongeza idadi ya mabwawa ili yaweze kukidhi
haja.
kwa upande wao wananchi wa vijiji vya mwanjoro na jinamo mahali
lilipo bwawa hilo wameiomba serikali kulisimamia bwawa hilo ili liweze
kukamilika kwani wamekuwa wakipata shida ya maji.
Wananchi hao wamesema kuwa wamekuwa wakifuta maji kwa umbalimrefu kwa
kutumia wanyama aina ya punda na kwamba bei ya maji kijijini hapo ni
shilingi mia tano kwa ndoo moja.
Makala anatembelea maeneo mbalimbali yaliyo na kero ya maji kabla ya
kuwasilishwa kwa bajeti ya wizara hiyo tarehe 30mwezi huu.
mwisho
serikali imesema kuanzia sasa haitaipa kampuni ya ujenzi Nyakirang’ani
ya mkoani mara kazi yeyote ya kuchimba mabwawa baada ya kampuni
kushindwa kukamilisha kazi za mabwawa mbalimbali hapa nchini.
kauli hiyo ya serikali imetolewa wilayani meatu mkoani simiyu na naibu
waziri wa maji,amosi makala mara baada ya kutembelea bwawa la mwanjoro
ambalo lilikuwa likijengwa na kampuni hiyo.
amesema mkandarasi huyo ameonyesha kiwango cha chini katika ujenzi wa
mabwawa anayopewa na kwamba kuanzia sasa hatapewa kazi yeyote ya
ujenzi wa mabwawa na wizara hicho hapa nchini kwani amekuwa
mkandarasi mbabaishaji na asiye na uwezo licha ya kupewa kazi hizo na
wizara.
‘’Nimefika mwenyewe nimejionea hali halisi ilivyo na nimeacha watalaam
wa wizara yangu waweze kufanya tathimini na watuleteea kabla
hatujasoma bajeti na mkandarasi huyu nimesema yeye na wizara yetu sasa
basi hatuwezi kupata hasara kwa kuwavumilia wakandarasi
wababaishaji.’’alisema Makala
mkuu wa wilaya hiyo.Rose mary kirigini
alimueleza naibu waziri huyo bwawa hilo lilianza kujengwa tangia mwaka
2009 hadi sasa na kwamba taarifa imekuwa ikionyesha kuwa limekamilika
kwa asilimia 80 jambo ambalo si kweli.na kwamba wakati umefika sasa
,kwa wananchi wa vijiji hivyo kulitumia bwawa hilo kwani wametaabika
kwa muda mrefu sana
Awali mhandisi wa maji toka sekretalieti ya mkoa,Gibson Kisaka amesema
hali ya upatikanaji wa maji katika mkoa huo haitoshi kutokana na
vyanzo vingi kuwa na maji yenye madini ya frolide na kwamba
wanaangalia uwezo wa kuongeza idadi ya mabwawa ili yaweze kukidhi
haja.
kwa upande wao wananchi wa vijiji vya mwanjoro na jinamo mahali
lilipo bwawa hilo wameiomba serikali kulisimamia bwawa hilo ili liweze
kukamilika kwani wamekuwa wakipata shida ya maji.
Wananchi hao wamesema kuwa wamekuwa wakifuta maji kwa umbalimrefu kwa
kutumia wanyama aina ya punda na kwamba bei ya maji kijijini hapo ni
shilingi mia tano kwa ndoo moja.
Makala anatembelea maeneo mbalimbali yaliyo na kero ya maji kabla ya
kuwasilishwa kwa bajeti ya wizara hiyo tarehe 30mwezi huu.
mwisho
![]() |
Click here to Reply or Forward
|
Why this ad?Ads –
Subscribe to:
Posts (Atom)
Comments System
disqus
Disqus Shortname
msora
Popular Posts
-
SABABU RASMI ZA MGAWANYIKO WA WENGE MUSICA BCBG 4X4 TOUT TERRAIN NA MIAKA MITATU YA MWANZO YA BCBG NA MAISON MERRE – (Sehemu...
-
Huha Makuja Nyungi (kushoto), akiwa anaelekea mahakamani muda mfupi kabla ya kusomewa hukumu hiyo. Kulia ni mtuhumiwa mwingine katika ke...
-
Mwezeshaji wa mada ya kwanza kuhusu umuhimu wa TIKA, ndugu Derick Ndetabula akitoa mada kwa washirik.
Header Ads
