Thursday, July 14, 2016

China yatangaza neema mkoa wa Simiyu

Mkuu wa mkoa wa simiyu Anthony mtaka mwenye suti nyeusi akiongea na balozi mdogo wa china Zhangy Biao mara baada ya kumalizika kwa kikao cha pomoja na balozi huyo kilichofanyika ofisini kwa mkuu huyo ,julai 13,2016-picha na Berensichina

Serikali ya china kuwekeza katika mkoa wa simiyu


SERIKALI YA CHINA IMESEMA IKO TAYARI KUWEKEZA KATIKA MKOA WA SIMIYU KWA KUJENGA VIWANDA MBALIMBALI VIKIWEMO VYA NGUO NA MAZIWA NA NYAMA KUTOKANA NA MKOA HUO  KUONYESHA KUWA NA RASILIMALI NYINGI KAMA MIFUGO NA PIA NDIO UNAONGOZA KWA KUZALISHA ZAO LA PAMBA NCHINI,
AKIONGEA NA VIONGOZI MBALIMBALI WA MKOA WA SIMIYU KUPITIA KWA MKALIMANI WAKE,YE TIANFA  BALOZI MDOGO WA CHINA NCHINI TANZANIA,ZHANG BIAO,AMESEMA  NCHI YAKE IKO TAYARI KUWEKEZA KATIKA VIWANDA KATIKA MKOA WA SIMIYU  ILI KUUSADIA MKOA HUO KUKUA KIUCHUMI IKIWA NI PAMOJA  NA KUWAPA AJIRA VIJANA WA MKOA WA SIMIYU.
KWA UPANDE WAKE MKUU WA MKOA WA SIMIYU ANTHONY MTAKA AMEMUHAKIKISHIA BALOZI HUYO KUWA MKOA WA SIMIYU UKO TAYARI KUWAPOKEA WAWEKEZAJI KUTOKA NCHINI CHINA  WATAKAOHITAJI KUWEKEZA KATIKA MKOA WA SIMIYU NA PIA WATAHAKIKISHA WANAWAPA USHIRIKINO WA KUTOSHA NA ULINZI PIA,,
BAADHI YA WADAU WA MAENDELEO WA MKOA WA SIMIYU WAMESEMA UJIO WA BALOZI HUYO NI FARAJA KWAO KWANI HUENDA UKAFUNGUA MILANGO NA FURSA KATIKA NYANJA MBALIMBALI ZA KIUCHUMI KATIKA MKOA HUU
BALOZI HUYO AMETEMBELEA MKOA WA SIMIYU IKIWA NI MWALIKO  WA  MKUU  WA MKOA WA SIMIYU  AMBAPO BAADA YA KUONDOKA MKOANI SIMIYU AMEELEKEA MKOANI MWANZA,
mwisho

Tuesday, July 12, 2016


mkuu wa hifadhi ya serengeti william mwakilema akiongea na waandishi wa habari kuhusu kukamatwa kwa mifugo hifadhini





Hawa ni baadhi ya Ngo'mbe wa wafugaji wa wilaya ya Bariadi walikomatwa wakichunga ndani ya hifadhi ya serengeti wiki iliyopita wafugaji hawa wamekuwa wakiingiza mifugo hiyo usiku kwa ajili ya kuchunga licha ya sheria ya tanapa na ile ya wanyma pori kukataza

WANUNUZI WAPAMBA SIMIYU WAONYWA KUTOWEKA MAJI




BERENSICHINA,SIMIYU,JULAI 12,2016,
,wanunuzi wa pamba wanaotia maji waonywa,
HABARI YA BIASHARA
SERIKALI MKOANI SIMIYU HAITAPOKEA PAMBA ILIYOWEKEWA MAFUTA YA KENGE KWA MADAI YA KUONGEZA KILO ,PAMBA INAYOWEKEWA MCHANGA NA MAJI KWANI KUFANYA HIVYO KUNAPUNGUZA UBORA WA PAMBA KATIKA SOKO LA DUNIA NA BADALA YAKE BEI KUENDELEA KUSHUKA NA HIVYO WAKULIMA KUKATA TAMAA KULIMA ZAO HILO NA KUJIKITA KATIKA MAZAO YA CHOROKO NA DENGU  ..

AGIZO HILO LIMETOLEWA NA MKUU WA MKOA WA SIMIYU ANTHONY MTAKA WAKATI WA MKUTANO BAINA YA WANUNUZI WA PAMBA NA WENYEVITI WA HALMASHAURI ZA WILAYA KUELEKEA  MSIMU WA UNUNUZI WA ZAO LA PAMBA AMBAPO BAADHI YA MAKAMPUNI YAMEANZA KUNUNUA  ,ILI  KUJUA BEI ELEKEZI IWAPO INAZINGATIWA .  

AMESEMA KUWA MKOA WA SIMIYU UNAZALISHA ZAO LA PAMBA NCHINI KWA ASILIMIA 60 AMBAPO MWAKA JANA ZILINUNULIWA KILO MILIONI 70 ZA PAMBA HIVYO KAMA MKOA HAWATAKUBALI KUONA ZAO HILO LINATOWEKA  KUTOKANA NA WATU WACHACHE KUJENGA MAZOEA YA KUIWEKEA MAJI PAMBA,MAFUTA YA KENGE NA MAWE LAZIMA HATUA ZICHUKULIWE DHIDI YAO KURUDISHA UBORA WA ZAO HILO KATIKA SOKO LA DUNIA.


AIDHA MKUU HUYO WA MKOA  AMETUMA SALAAM KWA WANUNUZI WA ZAO HILO WANAOHARIBU MIZANI NA KUWAIBIA WAKULIMA NA KUWATAKA WAACHE MARA MOJA

KWA UPANDE WA WADAU WA PAMBA WAMEYATAKA MAKAMPUNI YA UNUNUZI KULIPA USHURU WA AWALI KATIKA HALMASHAURI HUSIKA  KABLA YA KUANZA UNUNUZI.

MWISHO,



HIFADHI YA SERENGETI YAKANUSHA KUTOWAPIGA WAFUGAJI WALIOKAMATWA WAKIINGIZA MIFUGO HIFADHINI



BERENSICHINA,SERENGETI,JULAI 12,2016,.
,Hifadhi ya Serengeti yakanusha kutowapiga wafugaji,
SIKU CHACHE BAADA YA WAFUGAJI WILAYANI BARIADI MKOANI SIMIYU KUDAI KUPIGWA NA ASKARI WA HIFADHI YA TAIFA YA SERENGETI WAKATI WA ZOEZI WA UKAMATAJI MIFUGO INAYOINGIA HIFADHINI KINYUME CHA SHERIA,HIFADHI HIYO IMEKANUSHA TAARIFA HIZO NA KUSISITIZA HAKUNA MFUGAJI ALIYEPIGWA NA KAMA YUPO AJITOKEZE HADHARANI,
AKIONGEA NA WAANDISHI WA HABARI OFISINI KWAKE MKUU WA HIFADHI HIYO ,WILLIAM MWAKILEMA AMESEMA HAKUNA MTU YEYOTE ALIYEPIGWA BALI KILICHOKAMATWA NI MIFUGO KUTOKANA NA WAFUGAJI HAO  KUBUNI MBINU MPYA YA KUINGIZA MIFUGO USIKU NDANI YA HIFADHI KWA AJILI YA KUCHUNGA NA KWAMBA WAO WATAENDELEA KUWAKAMATA WAFUGAJI HAO KWA SABABU WANAVUNJA SHERIA YA TANAPA,SURA NAMBA 282 KAMA ILIVYOFANYIWA MAREKEBISHO MWAKA 2002
KWA UPANDE WAKE MWENYEKITI WA CHAMA CHA WAFUGAJI KANDA YA ZIWA MLIDA MSHOTA AMBAYE AMEONEKANA KUTOKUWA NA MSIMAMO KUHUSU SUALA HILO ALIPOHOJIWA NA ITV KUHUSIANA NA MADAI HAYO YA WAFUGAJI AMEKIRI KUWA KUTOKANA NA UHABA WA MALISHO WAFUGAJI HAO WAMEKUWA WAKIINGIZA MIFUGO HIFADHINI KWA AJILI YA KUCHUNGA KAMA ANAVYOELEZA,.
BAADHI YA VIJANA WALIOKUTWA NA CAMERA YA ITV NDANI YA HIFADHI HIYO WAMEKIRI KUTUMWA NA WAZAZI WAO KUCHUNGIA NDANI YA HIFADHI NA KWAMBA WANAPOJARIBU KUKATAA  HUPIGWA NA WAZAZI NA WALIOAJILIWA KUCHUNGA MIFUGO HUTISHIWA KUFUKUZWA KAZI,
HIVI KARIBUNI MAKAMU WA RAIS SAMIA SURUHU ALIWAAGIZA WAKUU WA WILAYA NA MIKOA KUHAKIKISHA WANAONDOA MABOMA YOTE YA WAFUGAJI YALIYOKARIBU NA HIFADHI ZA TAIFA HAPA NCHINI.
Mwisho

Habari za siku nyingi wapendwa wa blog hii ni matumaini yangu kuwa hamjambo wote na mnaendelea vizuri na shughuli za kila siku,nipende kuchukuwa fursa hii kuwaomba radhi kuwa sikuwa hewani kwa muda mrefu na hii ni kutokana na kutingwa na majukumu ya kazi,lakini niwataarifu kuwa kuanzia leo niko tayari kabisa kuwaletea habari mbalimbali za mkoa wa simiyu na maeneo mengine kwa lengo la kuwahabarisha kinachojili ni matumaini yangu kuwa tutakuwa wote katika kupata kila matukio  na habari motomoto za kila siku za ukweli na uhakika na siyo za kupika,
Niwatakie kila laheri katika shuguli zenu,
 wasalaam
Berensichina,Alikadi,mkurugenzi wa Habari motomoto

Comments System

disqus

Disqus Shortname

msora

Popular Posts

Header Ads

ad