Sunday, September 30, 2012

Bulaya na mwanafunzi bora wa mkwezi sekondary

Mbunge Bulaya akiwa na mwanafunzi Penina Wayoga mara baada ya kumtunuku  cheti cha mwanafunzi bora wa shule ya mkwezi iliyopo wilayani Bunda.picha na Berensi Alikadi

MBUNGE AWATAKA WATOTO WA KIKE KUSOMA KWA BIDII



NA Berensi Alikadi-Bunda

IMEELEZWA Kuwa  njia pekee ya kumsaidia mtoto wa kike ni kumpa elimu bora itakayomsaidia katika maisha yake ya baadaye na wala sivinginevyo.

Kauri hiyo imetolewa jana mjini Bunda na mbunge wa viti maalumu kundi la vijana wa chama cha mapinduzi mkoa wa Mara Ester Bulaya  wakati alipokuwa akiongea na wazazi na wanafunzi kwenye mahafali ya kwanza ya shule ya waschana ya Mkwezi iliyopo mjini Bunda.

Alisema kuwa mtoto wa kike anayonafasi kubwa ya kufanya vizuri kielimu kama ataendelezwa ipasavyo na kwamba ile dhana ya kumbeza mtoto wa kike kwa kutompa elimu sasa imepitwa na wakati.

Mbunge huyo aliwataka wazazi wa watoto hao waliohitimu kidato cha nne kuwasadia zaidi watoto hao ili waweze kuendelea na masomo ya vidato vya juu ambayo yawasaidia kuingia katika soko la ajira hapa nchini na nje ya nchi.

‘’Ndugu zangu wazazi watoto hawa sasa ndio wameanza hatua kubwa maana hii hatua waliyomaliza naweza kusema ni kama nusu hivyo wasaidieni ili waweze kufikia malengo ya maisha yao nina imani wanandoto nzuri ya kufika kileleni sasa tuwawezeshe ili wafaulu.’’alisema Bulaya.

Mbunge huyo alikubali kumsomesha mwanafunzi Penina Wayoga hadi kidato cha sita baada ya kupata vyeti sita ambavyo amefanya vizuri katika masomo ya hesabu,Fizikia,Sayansi uraia Jografia na bailogia ambapo aliibuka kidedea kwa kupewa vyeti sita.

Awali wakisoma risala ya kuhitimu masomo yao wanafunzi hao walisema kuwa walianza  masomo shuleni hapo  mwaka 2009 wakiwa wanafunzi 24 na sasa wamehitimu wakiwa 41 ambapo  sanaa wanafunzi 20na sayansi ni wanafunzi 21.

Walisema kwa muda wote waliosoma shuleni hapo wameweza kupata mafanikio mbalimbali ikiwa ni pamoja na shule hiyo kushika nafasi ya 4 kati ya shule 29 kimkoa,na shule kushika nafasi ya 36 kati ya shule 432 kikanda ambapo pia katika mtihani wa utimilifu walishika nafasi ya kumi kati ya shule 164 kimkoa.

Wanafunzi hao walibainisha kuwa pamoja na mafanikio hayo shule hiyo pia inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa maktaba,maabara jambo ambalo limechangia kudumaa kwa maendeleo ya elimu shuleni hapo.

Akisoma risala ya shule hiyo mkuu wa shule hiyo,Mwalimu Goodluck Muyenjwa alisema kuwa pamoja na shule hiyo kufanya vizuri lakini bado lipo tatizo la wazazi kutolipa ada kwa wakati jambo ambalo limesababisha uongozi wa shule hiyo kuwatowalipa watumishi mishahara kwa wakati.

Muyenjwa alisema kuwa shule hiyo pia inakabiliwa na tatizo la ukosefu wa umeme jambo limewafanya wanafunzi wa shule hiyo washindwe kujisomea ipasavyo na kumuomba mbunge huyo aweze kulifikisha kwa wahusika ombi ambalo alilikubali.
MWISHO.

Mbunge Bulaya akitunuku cheti kwa wahitimu wa kidato cha nne

Mbunge wa viti maalumu vijana ccm mkoa wa Mara Ester Bulaya kulia akimkabidhi cheti mwanafunzi Penina Wayoga ambaye aliibuka kidedea mwanafunzi bora katika mahafari ya kwanza ya shule hiyo ya waschana ya Mkwezi iliyopo wilayani Bunda .jana picha na Berensi Alikadi .

Saturday, September 29, 2012

Mkurugenzi wa wilaya ya Bunda akitoa maelezo kuhusu mradi mpya wa MAF

Mkurugenzi mtendaji wa wilaya ya Bunda Cprian Oyeir akitoa maelezo taarifa juu ya mradi wa MAF kwenye mkutano wa kutambulisha mradi huo uliofanyika katika ukumbi wa halimashauri ya wilaya hiyo,picha na Berensi Alikadi.

Mwakilishi wa UNDP akifafanua jambo kwenye mkutano

Mwakilishi wa shirikala la kimataifa la UNDP ,Amon Manyama akifafanua kuhusu mardi mpya wa MAF utakotekelezwa wilayani humo,picha na Berensi Alikadi

Mkuu wa wilaya akifungua mkutano

Mkuu wa wilaya ya Bunda Joshua Mirumbe akifungua mkutano wa siku moja wa kutambulisha mradi mpya wa MAF unaofadhiliwa na shirika lisilo la kiserikali la milenia ya tatu, utakaotekelzwa katika wilaya nzima ya Bunda kwa muda wa miezi mnne

Friday, September 28, 2012

Majeshi ya Amisom yauteka mji wa Kisimayo

Majeshi Kismayo
Hatimaye wanajeshi wa AMISOM wameuteka mji wa Kismayo.
Msemaji wa jeshi la Kenya Kanali Cyrus Oguna aliambia BBC kuwa wanajeshi wa Kenya kwa ushirikiano na wale wa Somalia walianza harakati zao mapema asubuhi ya leo.
Kwa sasa wanajeshi wa AMISOM wanaendelea na harakati zao kuingia ndani kabisa ya mjini huo. Kamanda wa majeshi hayo Luteni Generali Andrew Gutti, amesema AMISOM imewataka wenyeji wa mji wa Kismayo kuwa watulivu.
Kwenye taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari, Luteni Generali Gutti alisema kuwa nia na lengo la wanajeshi hao ni kuwakomboa watu wa Kismayo na kuwawezesha kuishi kwa amani na usalama.
Alidokeza kuwa harakati zinaendelea kulenga maeneo ya Al Shabaab mjini humo.
Aliongeza kuwa angewataka wapiganaji waliosalia Kismayo kujisalimisha
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, baadhi ya wapiganaji wa kundi hilo walio mjini humo, wameelezea nia yao kutaka kujisalimisha. Nayo AMISOM imewahikikishia usalama wao ikiwa wataweza kujisalimisha
Lakini mwandishi wa BBC anasema kuwa Al Shabaab husalimu amri kwa muda wakati wanapokabiliwa na majeshi yenye nguvu kuwaliko.
Ndege za kivita za Kenya zilifanya mashambulizi ya angani mapema wiki hii na kuharibu bohari lenye silaha za wapiganaji hao mjini humo.
Wiki iliyopita, Al Shabaab walijiandaa kuondoka Kismayo na hata kuwahamisha wapiganaji wao pamoja na silaha.
Mji huo wa bandarini ni muhimu kwa Al Shabaab kwani wanautumia kuingizia silaha na pia kuwatoza kodi wenyeji wa mji huo.
Hatua ya wao kupoteza mji huo, itakuwa ni pigo kubwa kwao, lakini wapiganaji hao wa Al Shabaab bado wana uwezo wa kufanya mashambulizi dhidi ya wanajeshi wa Somalia na wale wa Muungano wa Afrika hata katika sahamu ambazo wanajeshi hao wanadhibiti.
Chanzo BBC

Thursday, September 27, 2012

Jamani ee hivi ndivyo amba invyosombwa huko hapa Bunda

Lori la kampuni ya kuchambua pamba ya OLam ya mjini Bunda likiwa limebeba pamba kupita kiasi huku ikiwa haikufunikwa kiyume na sheria za bodi ya pamba,picha na Berensi Alikadi    

Wednesday, September 26, 2012

Mbunge wa vijana Mkoani Mara Ester Bulaya akikabidhi vifaa vya michezo.

Mbunge wa viti maalumu vijana CCM mkoa wa Mara Ester Bulaya mwenye Tshet Nyeusi Akikabidhi jezi za mipira wa miguu kwa mmoja wa viogozi wa jumuia hiyo toka katika wilaya ya Butiama juzi mjini Musoma,Ester ametoa vifaa vya milion saba na nusu kwa kata 34 za wilaya hiyo,picha na Berensi  Alikadi.

Monday, September 24, 2012

Jeshi la Kenya Matatani Somalia


Wanajeshi wa Kenya nchini Somalia
Ujumbe wa Umoja wa Afrika wa kudumisha amani nchini Somalia AMISOM, unasema utachunguza tuhuma kuwa wanajeshi wa Kenya waliwaia kwa kuwapiga risasi raia 7 wa Somalia wakati wa makabiliano na wapiganajai wa Al shabaab hapo jana Jumapili.
Wanajeshi hao inasemekana waliwaua raia saba katika kijiji cha Janaay Cabdalla wakati mapigano yalipotokea umbali wa kilomita 50 kutoka mji wa Kismaayo.
Msemaji wa kikosi cha Somalia, Mohemmed Hirsi, ameiambia BBC kuwa mauaji hayo yalitokea wakati jeshi la Kenya lilipovamiwa na wapiganaji wa Al Shabaab takriban kilomita sitini kutoka kwa ngome kubwa ya kundi hilo.
Msemaji wa AMISOM kanali Adi Aden amesema wakati ukweli wa kesi hiyo utakapojulikana watachukua hatua.
Msemaji huyo aliambia BBC kuwa wanajeshi wa Kenya waliwafyatulia risasi wanaume hao waliokuwa wameketi nje ya duka moja katika kijiji cha Janaay Cabdalla.
Wanajeshi wa Kenya na wale wa Somalia awali walivamiwa na wapiganaji wa Al Shebaab huku ripoti zikisema kuwa pande hizo mbili, zilipata majeruhi.
Kwa mujibu wa msemaji huyo, wanakijiji waliouawa ambao ni wanaume saba hawakuwa wanamgambo bali raia wa kawaida.
Duru zinasema kuwa wanaume hao walikuwa wamepiga foleni kununua sukari.Aidha msemaji wa jeshi la Muungano wa Afrika nchini Somalia, (AMISOM) alisema kuwa hawezi kuthibitisha tukio hilo, lakini madai hayo yatachunguzwa.
Wanajeshi wa Somalia wakiungwa mkono na wale wa Uganda na Kenya pamoja na vikosi vingine kutoka nchi tofauti za Afrika, wanakaribia kuuzingira mji wa Kismayo,na ili waweze kufanikiwa katika kuuteka mjihuo, wanachi wa pale watahitaji kushirikiana nao.
Wanajeshi wa Kenya wamewahi kutuhumiwa kwa kuwaua raia wakati wakifanya mashambulizi katika maeneo ya Al Shabaab .
Shirika la kuwahudumia wakimbizi UNHCR linakadiria takriban wakimbizi 10,000 wameutoroka mji wa Kismayo katika kipindi cha wiki moja iliyopita.
chanzo BBC

Afisa Ardhi Bunda aachana na ukapera

Afisa ardhi  wa wilaya ya Bunda Denis Masami akiwa na mke wake Maliacrala Alestus mara baada ya kufunga pingu za maisha katika kanisa katoriki la mjini Bunda.-picha na Berensi Alikadi

Sunday, September 23, 2012

Mbunge wa Somalia auwawa Mogadishu


Watu waliokuwa na silaha wamempiga risasi na kumuuwa mbunge wa baraza jipya mjini Mogadishu, Somalia.
Bunge la Somalia
Mbunge Mustaf Haji Mohamed alipigwa risasi wakati akitoka msikitini.
Bwana Mustaf Haji Mohamed ni mbunge wa kwanza kulengwa tangu bunge jipya rasmi kuchaguliwa mwezi Agosti.
Walioshuhudia tukio hilo wanasema mbunge huyo alipigwa risasi kadha.

Chanzo BBC

Wahitimu kidato cha nne waaswa



NA Berensi Alikadi-Bunda

SERIKALI wilayani Bunda imewaasa wanafunzi waliohitimu elimu ya kidato cha nne kutobweteka na elimu waliyopata badala yake watambue kuwa bado wanalojukumu kubwa la kusonga mbele kielimu.

Kauri hiyo imetolewa jana na mkuu wa wilaya hiyo Joshua Mirumbe katika hotuba yake iliyosomwa na afisa mifugo na uvuvi wa wilaya hiyo,Masuke Ogwa kwenye mahafali ya sita ya shule ya sekondari ya Ellys iliyoko katika mamlaka ya mji mdogo wa Bunda.

Alisema kuwa pamoja na wanafunzi hao kufanya mahafali hayo lakini watambue kuwa kuna kazi kubwa ya mtihani ambayo wanapaswa kuifikilia kila siku katika maisha yao na akawataka kutumia muda mwingi katika kujiandaa na mtihani ambao utafanyika hivi karibuni nchini kote.

‘’Niwapongeze kwa kuhitimu leo lakini naomba msibweteke tambueni kuwa kazi kubwa bado iko mbele yenu huu ni mwanzo tu mtaenda vyuo vikuu na vyuo vingine nawaomba mjitahidi na muwe mabalozi wazuri kumbukeni bila elimu hakuna maisha hivyo jitahidini musome kwa bidii na muepukane na vitendo viovu’’alkisema Masuke.

Awali wakisoma risala ya kuhitimu masomo yao wanafunzi hao walisema kuwa walianza masomo yao mwaka 2009 wakiwa wanafunzi 215 ambapo wamehitimu wakiwa wanafunzi 175 na kwamba wanafunzi wengine wameshindwa kuhitimu kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo utoro na mamba na utovu wa nidhamu.

Akitaoa taarifa ya shule hiyo kwa wazazi,mkuu wa shule hiyo Mwalimu Feston Onanda alisema kuwa tangia kuanzishwa kwa shule hiyo mwaka 2005 imekuwa ikifanya vizuri katika mtihani ya kidato cha pili na cha nne ambapo hadi sasa zaidi ya wanafunzi 48 toka katika shule hiyo wamefanikiwa kujiunga katika vyuo vikuu na vyuo mbalimbali hapa nchini.

Alisema kuwa katika kuhakikisha kiwango cha elimu shuleni hapo kinapanda  shule hiyo imeweka mikakati ikiwa ni pamoja na kusimamia ufundishaji na kuhakikisha kuwa wanafunzi wanatoa mazoezi ya mara kwa mara,kuhakikisha wanatoa mitihani ya kila wiki na kufauatilia mahudhulio ya wanafunzi ipasavyo.
Naye mkutugenzi wa shule hiyo Eliah John Maduhu alisema pamoja na mafanikio hayo bado kuna changamoto kubwa katika suala la elimu ambazo alizitaja kuwa baadhi ya wazazi kukosa ushirikiano na shule hivyo kufanya malezi ya wanafunzi kuwa mabaya,baadhi ya watoto kutoenda masomo na kufanya yao kutoridhisha.

Hata hivyo Maduhu aliomba serikali kuzisaidia shule binafsi kwa kuzipatia vifaa kama vile vitabu na vifaa vya maabara kwa masomo ya sayansi wakati wa mtihani kwani shule nyingi za binafsi hazipati vitabu na kuzingatia kuwa mitaala hubadirika siku kwa siku.

Mwisho


Kushuka kwa zao la pamba chanzo chatajwa


NA Berensi Alikadi-Bunda.

IMEELEZWA kuwa  ukosefu wa mitaji kwa wakulima ,usimamizi imara wa watalaam na utashi wa kisiasa vimekuwa vikichangia kushuka kwa uzalishaji wa zao la pamba wilayani Bunda kila mwaka.

Hayo yamesemwa jana na washiriki wa mkutano wa kuboresha kilimo cha pamba katika wilaya hiyo uliofanyika katika ukumbi wa Serengeti Resort chini ya uneyekiti wa mkuu wa wilaya hiyo Joshua Mirumbe.

Wakichangia mada katika mkutano huo baadhi ya wadau na wakulima wa zao hilo wamedai wakulima wengi hawana mitaji ya kuendeleza zao hilo na kwamba wengi wao wakishauza pamba hutumia pesa na kuzimaliza anbapo wengi wao hukosa hata pesa ya kununua pembejeo za msimu ujao.


Mkaguzi wa bodi ya pamba katika wilaya za Bunda na Serengeti,Igoro Maronga alisema kuwa suala la kilimo cha pamba sasa hivi kimekosa usimamizi kuanzia kwa maafisa ugani hadi kwa wanasiasa ambao pia wamekuwa halitilii maanani sana licha ya kufahamu kuwa ndilo zao pekee linalowapa tija wapiga kura wao.

Igoro alibainisha kuwa  ukiukwaji wa masharti  ya kanuni kumi za kilimo cha zao hilo,mbegu kutochanganywa vizuri viwandani na kutoweka mbolea za samadi mashambani kimekuwa chanzo kikubwa cha wakulima kupata mazao hafifu.

Naye Daudi Iramba afisa kilimo wa kata ya Hunyari alisema kuwa kumekuwepo na tabia ya baadhi ya makampuni kuunda vikundi vya wakulima vijijini bila kuwahusisha wataalam jambo ambalo limkuwa likiwapa shida maafisa ugani walioko vijijini  katika kufanya kazi na vikundi hivyo.

Akizugumza kwa niaba ya wakulima wa pamba,mkulima mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Mayaya alisema kuwa dawa nyingi wanazopelekewa wakulima kwa ajili ya zao hilo ni zile ambazo hazina ubora na kwamba yapo makampuni kama vile Olam,Alliance zilichangia pia mazao kuharibika na kwamba ni vema serikali ikariangalia hilo kwa upana zaidi.

‘’Changamoto kubwa inayotukabiri sisi licha ya hayo ni pamoja na wakulima kuchanganya mazao na ni vema wakulima wakawa wanapatiwa mafunzo ya mara kwa mara ili waweze kuwa na elimu ya kutosha maana hata hawa maafisa ugani wengine hawawafikii wakulima ipasaavyo’’alisema mkulima huyo.

Akifungua mkutano huo wa siku moja mkuu wa wilaya hiyo Joshua Mirumbe alisema lengo la mkutano  huo ni kuweka mkakati wa pamoja wa kuboresha zao la pamba ambalo ndilo zao la biashara kwa wilaya hiyo ambapo hivi sasa uzalishaji wake unashuka kila mwaka .

Mirumbe alisema kuwa kazi ya watumishi yaani maafisa ugani,makampuni ni kutoa elimu kwa wakulima kuhusu kilimo cha kisasa cha zao hilo na kwamba ndiyo maana ameitisha mkutano huo ili aweze kuwakutanisha wadau wa kilimo,wakulima na watalam kwa ajili ya kuweka mkakati wa pamoja.

Alisema kuwa katika msimu wa mwaka huu wilaya hiyo ilikuwa ikusanye  kilo million 10 lakini kutokana na ugonjwa ulizikumba kata za igundu na Namhura wilaya imefanikiwa kukusanya hadi sasa jumala ya kilo million 8 na kwamba huenda hali ikapamba kutokana na kwamba msimu bado unaendelea.

Mkutano huo umeshirikisha wadau wa kilimo, wakulima bora, maafisa ugani,wawakilishi wa makampuni,maafisa tarafa watendaji wa kata na waandishi wa habari.

Mwisho

Sunday, September 16, 2012

Wanafunzi 10777 kufanya mtihani wa darasa la saba


NA Berensi Alikadi-Bunda.

JUMLA ya wanafunzi 10777 wanatarajia kufanya mtihani wa kuhitimu darasa la saba  mwaka huu 2012 katika wilaya ya Bunda.utakaofanyika kesho nchini kote

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana,afisa elimu ya msingi wa wilaya hiyo Labani Bituro alisema kuwa kati ya wanafunzi hao wavulana ni 5452 na wasichana ni 5325.tofauti na mwaka jana ambapo wanafunzi 12931 walifanya mtihani huo

Alisema wanafunzi hao wanatarajia kufanya mtihani huo katika shule 155 ambazo ni za serikali na shule 151 ni za watu binafsi na kwamba maandalizi yote yameshakamilika ikiwa ni pamoja na kutoa mafunzo kwa wasimamizi watakaosimamia mtihani huo.

Bituro  alisema kuwa wilaya hiyo imeandaa vituo 478 katika majimbo yote ya Mwibara na Bunda ambako mitihani hiyo itafanyika  na kwamba maandalizi yamekamilika kwa asilimia mia moja.

Alifafanua kuwa wilaya imejiandaa ipasavyo kuhakikisha kuwa mtihanai huo utafanyika kwa amani na utulivu na kwamba wasimamizi wote wamekula kiapo na kwamba yeyote atakayekiuka kiapo alichokula na kuvujisha mtihani kwa kupewa hongo atachukuliwa hatua kali ikiwa ni pamoja na kupelekwa mahakamani.

Afisa elimu huyo aliwataka wale wote waliochaguliwa kusimamia mtihani huo kuwa waaminifu na kuifanya kazi hiyo kwa kufuata maadili na  uangalifu mkubwa kama walivyokula kiapo ili kuileta heshima wilaya hiyo.

''Tumewapa mafunzo ya kutosha na wamekula kiapo na kwa sababu ni waalimu wana dhamana ya serikali nina imanai kuwa wataifanya kazi hiyo vizuri lakini pia kwa yule atakayejichanganya akadanayika na vipesa akatoa majibu huyo kazi ni kwake maana hatutamuonea aibu naomba watambue hilo''alisema Bituro.

Nao baadhi ya wanafunzi wa shule mbalimbali za  wilaya hiii ambao wamehojiwa na gazeti hili kwa nyakati tofauti wamesema kuwa wamejiandaa ipasavyo katika kukabiliana na mtihanai huo wa darasa la saba ambapo wengi wao walionyesha kujiandaa ipasavyo.

''Kwakweli tumejiandaa vizuri sana kutokana na maandalizi na masomo tulivyofundishwa na waalimu wetu tuna imanai kuwa tutafanya mtihanai huo kwa ufanisi zaidi na tuna imani kuwa mungu atatusaidia''walisema wanafunzi wa shule ya msingi Kabalimu iliyoko katika mamlaka ya mji mdogo wa Bunda.

Mwisho





Friday, September 14, 2012

Njama ya mashanbulizi yatibuliwa Kenya


Magwanda ya mabomu ya kujilipua
Polisi nchini Kenya wamenasa magwanda yenye mabomu ya kujilipua pamoja na zana zengine ambazo zilikuwa zitumike kwa mashambulizi ya kigaidi mjini Nairobi.
Washukiwa wawili wamekamatwa katika msako huo uliofanywa asubihi ya leo katika mtaa wa Eastleigh mjini Nairobi.
Msemaji wa polisi nchini Kenya Eric Kiraithe anasema kuwa maguruneti kumi na mbili pamoja na bunduki aina ya AK 47 pia zilinaswa wakati wa msako uliofanywa na polisi mtaani humo.
"tunaamini kuwa silaha hizi zilinuiwa kutumika kufanya mashambulizi ya kigaidi mjini Nairobi'' alisema bwana Kiraithe.
Msako huo uliofanywa na polisi Ijumaa uliongozwa na polisi wa kupambana na ugaidi baada ya polisi kupata habari kutoka kwa raia.
Na baada ya masaa kadhaa ya kuwahoji washukiwa, magwanda manne ya mabomu ya kujitoa mhanga , mabomu mawili na silaha zingine zilipatikana ndani ya nyumba ya mshukiwa mmoja.
Polisi wanaamini kuwa mabomu hayo yalikuwa na vilipuzi vyenye uzito wa kilo arobaini na yangetumika kushambulia baadhi ya sehemu za mji mkuu Nairobi na miji mingine mikubwa.
Bwana Kiraithe amelaumu kundi la Al Shabab. Amesema kuwa washukiwa wengine 8 wako mbioni baada ya washukiwa Abdul majid Mohammed raia mkenya na Suleiman Abdi Aden msomali, kukamatwa na polisi wa Kenya.
Wangali wanahojiwa na polisi na watafikishwa mahakamani baadaye wiki ijayo.
Silaha hizo zinasemekana kufanana na zile zilizotumika katika mashambulizi ya kigaidi yaliyofanyika nchini Uganda dhidi ya watu waliokuwa wanatazama fainali ya kombe la dunia mwaka 2010, ambapo watu 76 waliuawa
Kundi la Al-Shabab lilikiri kufanya mashambulizi nchini Uganda, wakisema kuwa wanapinga nchi hiyo kujihusisha na harakati dhidi ya kundi hilo nchini Somalia.
Kenya imeshambuliwa karibuni na kundi la al-Shabab baada ya kupeleka vikosi vyake Somalia.
Chanzo-BBC

walibania wamsubiri kwa shangwe na furaha papa Benedikt 16

Matukio ya Kisiasa

Walibnan wamsubiri kwa shangwe na furaha Papa Benedikt wa 16

Kiongozi wa kanisa katoliki ulimwenguni, Benedikt wa 16, ameondoka Vatikani kuelekea Libanon ambako anatarajiwa kuwatolea mwito wakristo milioni 15 wa Mashariki ya kati waishi kwa amani pamoja na waislamu .
Akiongoza ujumbe mkubwa wa makadinali kadhaa, Papa Benedikt wa 16 anatarajiwa kuwasili wakati wowote kutoka sasa  mjini Beirut.
Ziara hii inasadif miaka 15 baada ya ile ziara ya kihistoria iliyofanywa na mtangulizi wake,Johanna Paulo wa Pili, aliyeitaja kuwa ni "Risala",nchi hiyo ya mchanganyiko wa waumini wa dini tofauti na ambao wanatofautiana tangu katika suala la siasa ya ndani mpaka kuhusiana na vita nchini Syria.
Pirikapirika za kumkaribisha kiongozi huyo wa kanisa katoliki ulimwenguni zimeshika kasi, huku hatua za usalama zikiimarishwa mjini Beirut tangu angani mpaka ardhini.

Kanisa kuu la St. George mjini Beirut Libanon
Jamii zote za wakaazi wa Libanon,wakristo tangu wakatoliki mpaka waorthodox,waislam tangu wa sunni mpaka wa shiya na wadruz wamejiandaa kumkaribisha Papa Benedikt wa 16.
"Libanon inasubiri ziara ya amani"-ndio kichwa cha maneno cha magazeti ya leo nchini Libanon, huku mabango na biramu yaliyoandikwa kwa lugha za kiarabu, kifaransa, kijerumani na kingereza yametundikwa majiani yakiwa na maandishi yasemayo kwa mfano "Ni ushahidi dhahiri wa jinsi anavyolipenda eneo la Mashrik".
Mizinga 21 itafyetuliwa kwa hishma yake mara tu Papa Benedikt wa 16 atakapowasili uwanja wa ndege na kupokelewa na viongozi wa Libanon, akiwemo pia rais Michel Suleiman-kiongozi pekee wa ulimwengu wa kiarabu ambae ni mkristo.
Katika ziara yake hii ya pili katika eneo la mashariki ya kati, baada ya ile ya mwaka 2009 katika "ardhi takatifu", Papa Benedikt  wa 16 anatarajiwa kuhutubia  angalao mara sabaa. Atawakabidhi maaskofu wa eneo hilo "Nasaha" iliyoandaliwa mwaka 2010 na kusimmiwa na yeye mwenyewe Papa Benedikt wa 16-inayotoa muongozo wa kile kinachostahiki kufuatwa na kanisa katoliki katika eneo la Mashariki ya Kati.

Papa Benedikt wa 16 na mtumishi wake Paolo Gabriele
Tukio la kusisimua linatarajiwa kuwa mkutano wa Papa Benedikt wa 16 na vijana wa kiislamu na kikristo kesho huko Bkerke,makao makuu ya uongozi wa kanisa la Maronite.
Kwa mujibu wa waandalizi, wajumbe wa kikristo wa Palastina, Misri, Cyprus, Jordan, Iraq na Syria wanatazamiwa kuhudhuria hafla hiyo.
Ziara ya Papa Benedikt wa 16 itamalizika jumapili ijayo kwa misa ya hadhara katika uwanja mashuhuri wa Waterfront mjini Beirut.
Mwandishi:Hamidou Oummilkheir/AFP
Mhariri: Miraji Othman

RADI YAUWA MMOJA,YAJERUHI WAWILI-BUND


NA Berensi Alikadi-Bunda

MTU mmoja amefariki dunia na wengine wawili kujeruhiwa vibaya baada ya kupigwa na radi.

Akielezea tukio hilo jana kwa waandishi wa habari mwenyekiti wa kamati ya maafa ya wilaya hiyo Joshua Mirumbe alisema kuwa tukio hilo limetokea sept 12 mwaka huu majira ya saa 10 jioni katika kijiji cha Mikomariro tarafa ya Chamliho.

Alimtaja aliyekufa kuwa ni Marwa Magena 65 mkazi wa kijiji cha Masinki wilayani Serengeti ambaye alikuwa amefika kijijini hapo kwa ajili ya kusalimia ndugu yake ambaye anaishi katika hicho.

Mirumbe ambaye pia ni mkuu wa wilaya hiyo alisema kuwa siku hiyo mvua kubwa ilikuwa katika kijiji hicho ambayo iliambatana na radi iliyompiga mtu huyo ambaye alikufa hapohapo.

Alifafanua kuwa pamoja na radi hiyo kuuwa mtu huyo pia iliwajeruhi watu wengine wawili,ambao ni Rbobhi Nyamhanga na Tiri Nyamhanga wote wakazi wa kijiji cha Mekomariro.

‘’Hawa wawili wamejeruhiwa vibaya na mmoja kati yao,Rhobi Nyamhanga amepelekwa Bugando kwa matibabu zaidi na mwenzake amelazwa katika hospital ya Butiama kwa matibabu zaidi,bado sijapata maendeleo yao nikipata nitawaambia’’alisema Mirumbe.

Hata hivyo mkuu huyo aliwatahadhalisha wananchi kuwa makini na mvua zinazoanza kunyesha ikiwa ni pamoja na kuweka nyumba zao imara ili zisije zikaezuliwa na upepo.
MWISHO

Onyo la WHO na vifo 31 kutokana na Ebola DRC


Virusi vya Ebola
Idadi ya watu waliofariki kutokana na mlipuko wa homa ya Ebola, katika Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo, imefika watu 31 hadi kufikia sasa na hata inatishia kuathiri miji kadhaa.
Hili ndilo onyo limetolewa na shirika la afya duniani WHO.
Mipuko wa kwanza wa homa hiyo uliripotiwa tarehe kumi na saba mwezi wa saba katika mkoa wa Kaskazini Mashariki wa Orientale.
Afisaa mmoja wa shirika hilo Eugene Kabambi aliambia shirika la habari la Reuters kuwa hali ni mbaya sana na kwamba bado haijadhibitiwa.
Ni rahisi sana kuambukizana homa ya Ebola na homa hiyo huuwa asilimia tisini ya watu ambao huambukizwa.
Hakuna tiba inayojulikana kwa homa hiyo wala chanjo. Homa hiyo husambaa kwa kugusana na husababisha mgonjwa kuvuja sana damu.
Idadi ya vifo vilivyotokana na homa yenyewe katika miji ya Isoro na Viadana, imeongezeka maradufu kwa zaidi ya wiki moja hadi watu 31.
Homa ya Ebola
Inaarifiwa wauguzi watano wamefariki kutokana na homa hiyo.
"homa hii bado haijadhibitiwa. Badala yake hali ni mbaya zaidi hata kuliko awali. Ni mbaya sana'' alisema bwana Kabambi.
"ikiwa hakuna hatua zitachukuliwa sasa hivi, homa hiyo itasambaa hadi maeneo mengine na hata katika miji mikuu,'' aliongeza Bwana Kabamba.
Mwezi jana mlipuko wa aina mbaya sana ya homa hiyo katika nchi jirani ya Uganda ilisababisha vifo vya watu 16 lakini wafanyakazi wa afya wanasema kuwa milipuko hiyo miwili haina uhusiano wowote.

Washukiwa wa mashambulizi wakamatwa Libya




Kundi linaloshukiwa kuafnya mashambulizi mjini Benghazi
Maafisa nchini Libya wamewakamata washukiwa kadhaa wa machafuko yaliyosababisha kifo cha balozi wa Marekani nchini humo pamoja maafisa wengine wanne wa ubalozi huo mjini Benghazi.
Waziri mkuu mpya wa Libya Mustafa Abu Shaqur aliambia BBC kuwa uchunguzi unaoendelea kuhusiana na kisa hicho unaonekana kufanikiwa.
Shambulizi lilifanyika siku ya Jumanne wakati wa maandamano yaliyopinga filamu iliyotengezwa nchini Marekani kumkejeli Mtume Mohammed.
Maandamano sawa na hayo yamesambaa katika nchi za kiarabu na mataifa ya Kaskazini mwa Afrika.
Maandamano zaidi yanatarajiwa kufanyika baada ya maombi ya Ijumaa
Makabiliano kati ya polisi wa kupambana na ghasia pamoja na waandamanaji yameendelea usiku kucha katika mji mkuu wa Misri, Cairo ambako makundi ya wapiganaji wa kiisilamu pamoja na watu wengine waliitisha maandamano ya amani ya watu milioni moja baadaye leo Ijumaa.
Hapo jana kulizuka ghasia zaidi nje ya ubalozi wa Marekani mjini Cairo kati ya polisi na waandamanaji wanaokashifu filamu ambayo wanasema kuwa inakejeli imani ya Kiislamu.
Runinga ya Misri ilionyesha gari likiteketezwa moto na watu wengine wakikimbia vitoza machozi.
Waandamanaji walitaka kufukuzwa kwa balozi wa Marekani nchini humo huku polisi wakiwafyatulia mabomu ya kutoa machozi waandamanaji waliokuwa wakirusha mawe.
Nchini Yemen waandamanaji walivamia ubalozi wa Marekani wakichoma moto magari kabla ya vikosi vya ulinzi kuwadhibiti kwa kuwafukuza kutoka eneo hilo.
Maandamano zaidi pia yamefanyika katika nchi za Tunisia, Morocco, Sudan, Mauritania na Iran.
Wakati huohuo maafisa wa Marekani wanasema serikali ya nchi hiyo inachunguza ikiwa mashambulio ya jumanne kwenye ubalozi wa Marekani katika mji wa Libya wa Benghazi yalikuwa ni ya kupangwa au la .
Balozi wa Marekani nchini Libya , Christopher Stevens, aliuawa .
Maafisa wa Marekani wameelezea mashambulio hayo kama yenye utata na yenye kupangwa kitaalamu na kuna tetesi kwamba makundi ya jihad huenda yalihusika .
Awali ilifikiriwa kuwa mashambulio hayo yalikuwa na uhusiano na maandamano ya kupinga filamu iliyokuwa inamkejeli Mtume Mohammed.
Takriban waandamanaji mia mbili wamekusanyika karibu na ubalozi wa Marekani mjini Cairo Misri kwa usiku wa pili kuelezea hasira yao juu ya filamu hiyo .

Aliyekuwa balozi wa Marekani nchini Libya Christopher Stevens
Awali waandamanaji walirusha mawe kwenye ubalozi huo na vikosi vya usalama vikafyatua mabomu ya kutoa machozi kuwa tawanya.
Watu wenye silaha waliokuwa na maguruneti walichomo moto jengo la ubalozi na walioshuhudia wanasema watu hao walizingira eneo hilo.
Rais Obama amelaani vikali shambulio hilo na ameahidi kushirikiana na serikali ya Libya kuwafikisha mbele ya sheria wahusika
Chanzo BBC

DRA YATOA MSAADA WA VIFAA VYA THAMANI YA MILION 3,736,000



Na Berensi Alikadi-Bunda.

 BAADA ya watu wasiofahamika kuchoma mabweni mawili ya kidato cha pili katika sekondari ya Ikizu iliyoko wilayani Bunda mkoani Mara inayomilikiwa na kanisa la Kisabato ,shirika lisilo la kiserikali la ADRA la mkoani Arusha  limetoa msaada wa vitu mbalimbali ili kusaidia wanafunzi waliounguliwa na vitu vyao.

Akizungumza na wanafunzi wa shule hiyo kabla ya kukabidhi vifaa hivyo,mwenyekiti ya kanisa hilo jimbo la Mara mchungaji Daudi Makoye alisema kuwa shirika hilo limetoa vifaa hivyo baada ya kupata taarifa ya kuchomwa kwa mabweni hali ambayo imesababisha wanafunzi kukosa mahali pa kulala na kukosa vifaa muhimu zikiwemo nguo,magodoro na madftari yao.

Mwenyekiti alivitaja vifaa hivyo vilivyotolewa kuwa ni  masweta122,suruali  94,mashati mashati 82 ,blanket 83,matandiko 94 na majaketi42 vyote vikiwa na thamani ya shilingi million 3,736,000.ambapo alisema kuwa wanatarajia kupata misaada mingine toka kwa wananchi wenye mapenzi mema  hususa ni viongozi wa serikali ambao walisoma katika shule hiyo.

Akikabidhi vifaa hivyo kwa wanafunzi hao mkuu wa wilaya hiyo Joshua Mirumbe alilipongeza shirika hilo kwa mchango wake mkubwa lililotoa kwa kanisa hilo wa kutoa vifaa hivyo ambapo aliyataka mashirika mengine pia kuiga mfano wa shirika hilo.

Mirumbe ambaye pia alisoma katika shule hiyo alisema kuwa shirika hilo limekuwa likichangia katika miradi mbalimbali ya maendeleo katika nchi mbalimbali za afrika na kwamba mchango wake huo iliotoa utasaidia wanafunzi hao ambao vifaa vyao viliungulia kwenye mabweni hayo.

Aidha mkuu huyo aliwapongeza wanafunzi waliopatwa na mkasa huo kwa kuonyesha moyo wa uvumilivu wa kuendelea na masomo ambapo amewaomba waendelee kusoma kwa bidii na kujiandaa na mitihani wakati ambapo serikali ya wilaya na mkoa vikiendelea kutafuta misaada mbalimbali kwa ajili yao.

‘’Napenda niwafahamishe kuwa sisi kama wilaya tunaendelea kuomba misaada mbalimbali toka kwa wananchi na mashirika tumeshayaomba mashirika yanayonunua pamba hapa kwetu kama vile kampuni ya Mathayo, Badugu,Olam, Aliance na Bulamba Ginery ili waweze kutusaidia na michango hiyo ikija tutaiwasilisha hapa tuwape ‘’alisema Mirumbe.

Alitumia pia fursa hiyo kuwaambia wanafunzi hao kuwa tume aliyoiunda bado inaendelea na kazi na kwamba itakapomaliza kazi yake itatoa taarifa kuhusiana na tukio hilo ambalo linahusishwa na mlipuko na wala siyo umeme kama ambavyo imekuwa ikidaiwa na baadhi ya watu.

Mwisho


DDH Bunda hawana X-Ray
Na Tezra Lusenga Bunda;
Septe 13, 2012;

HOSPTAL teule ya wilaya ya Bunda mkoani Mara haina huduma ya mashine ya X-Ray kwa zaidi ya miezi sita ambapo hali hiyo imekuwa kisababisha kero kwa wagonjwa wanaohitaji huduma hiyo.

Hayo yameleezwa leo na mganga mkuu wa wilaya ya Bunda, Dk. Riner Kapinga, kwenye kikao cha baraza la madiwani kilichoketi katika ukumbi wa halmashari mjini Bunda.

Dk. Kapinga amesema kuwa X-Ray iliyokuwepo katika hospitali hiyo iliharibika na kwamba kwa kipindi hicho chote wagonjwa wamekuwa wakitaabika sana na kulazimika kupelekwa katika hospitali za misheni Kibara, hospitali ya mkoa wa Mara mjini Musoma na katika hospitali ya rufaa Bugando ya jijijini Mwanza.

Amesema kuwa kufuatia hali hiyo halmashauri ya wilaya ya Bunda, imetoa kiasi cha sh. Milioni mbili kwa ajili ya kuleta mafundi wa kampuni Philips, iliyoingia mkataba na wizara ya afya ili waweze kuangalia uwezekano wa kuitengeneza X-Ray hiyo.

Wakichangia kwenye kikao hicho, madiwani wamesema kuwa hospitali hiyo inakabiliwa na changamoto nyingi, ikiwa ni pamoja na ukosefu wa maji ya kutosha hali ambayo imekuwa ikisababisha kukithiri kwa uchafu hospitalini hapo.

Diwani wa kata ya Balili ambako ndiko iliko hospitali hiyo, Bw. Georges Miyawa, amesema kuwa hupungufu huo wa maji umesababisha baadhi ya vyoo katika hospitali hiyo kuziba, hali ambayo imesababisha uchafu kutiririka hovyo.

Aidha, mhandisi wa maji katika mji mdogo wa Bunda, Injinia Idd Swai, amesema kuwa maji katika mji wa Bunda yamekuwa yakitoka kwa mgao na kwamba upungufu wa maji katika hospitali hiyo ni kutokana na tanki moja la maji kupasuka.

Injinia Swai ameutaka uongozi wa hospitali hiyo kutengeneza tanki hilo ili wanapowasukumia maji waweze kuyahifadhi katika mantaki yote matatu yaliyoko hospitalini hapo, ili wanapopitisha mgao wawe na akiba ya kutosha.

Mwisho

Poleni sana

Mkuu wa wilaya ya Bunda Joshua Mirumbe akimkabidhi mmoja wa wanafunzi waliounguliwa vitu vyao katika shule ya sekondari Ikizu hivi karibuni ,msaada ambao umetolewa na shirika la ADRA la mkoani Arusha.

Thursday, September 13, 2012

Marekani kuchunguza mashambulizi ya Libya


Mashambulizi dhidi ya ubalozi wa Marekani mjini Benghazi
Maafisa wa Marekani wanasema serikali ya nchi hiyo inachunguza ikiwa mashambulio ya jumanne kwenye ubalozi wa Marekani katika mji wa Libya wa Benghazi yalikuwa ni ya kupangwa au la .
Balozi wa Marekani nchini Libya , Christopher Stevens, aliuawa .
Maafisa wa Marekani wameelezea mashambulio hayo kama yenye utata na yenye kupangwa kitaalamu na kuna tetesi kwamba makundi ya jihad huenda yalihusika .
Awali ilifikiriwa kuwa mashambulio hayo yalikuwa na uhusiano na maandamano ya kupinga filamu iliyokuwa inamkejeli Mtume Mohammed.
Takriban waandamanaji mia mbili wamekusanyika karibu na ubalozi wa Marekani mjini Cairo Misri kwa usiku wa pili kuelezea hasira yao juu ya filamu hiyo .
Aliyekuwa balozi wa Marekani nchini Libya Christopher Stevens
Awali waandamanaji walirusha mawe kwenye ubalozi huo na vikosi vya usalama vikafyatua mabomu ya kutoa machozi kuwa tawanya.
Watu wenye silaha waliokuwa na maguruneti walichomo moto jengo la ubalozi na walioshuhudia wanasema watu hao walizingira eneo hilo.
Rais Obama amelaani vikali shambulio hilo na ameahidi kushirikiana na serikali ya Libya kuwafikisha mbele ya sheria wahusika.
Chanzo BBC

Vifo vya watoto vimepungua duniani


Watoto
Takriban watoto milioni 6.9 walifariki kabla ya kufikisha miaka mitano mwaka jana ikilinganishwa na vifo milioni 12 vya watoto wachanga vilivyotokea mwaka 1990. Takriban watoto elfu kumi na tisa walifariki mwaka 2011.
Kwa mujibu wa shirika la kuwahudumia watoto la Umoja wa mataifa Unicef, sababu mojawapo ya kupungua kwa vifo ni nchi maskini kutajirika.
Lakini, sababu nyinginezo ni nchi zinazostawi kupata msaada unaostahili kufanya kampeini za kuhamasisha wanawake kuwanyonyesha watoto na kuwapa chanjo.
Nchi ambazo idadi ilipungua sana ni zile ambazo zilipata msaada mwingi kutoka nje.
"ukiangalia, nchi ambazo idadi ya vifo imepungua sana mfano Jamuhuri ya watu wa Lao, Timor na Liberia
ambazo ni nchi tatu za kwanza katika orodha ya nchi ambako idadi ya vifo ilipungua, nadhani kwa nchi hizi zote msaada unaotoka nje umechangia pakubwa jambo hilo,'' alisema mkurugenzi mkuu wa shirika la Unicef nchini Uingereza, David Bull.
Juhudi zinazolenga magonjwa ya kuambukizana kama Ukambi, zimepunguza vifo duniani kutoka vifo vya watoto laki tano mwaka 2000 hadi vifo laki moja mwaka 2011.
Mwaka jana nusu ya vifo vya watoto wachanga duniani vilitokea katika nchi tano pekee kulingana na Unicef. Hizi nchi ni pamoja na India, Nigeria, Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Pakistan na China.
Katika Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Chad, Somalia, Mali, Cameroon na Burkina Faso idadi ya vifo vya watoto iliongezeka kwa vifo 10,000 au zaidi mnamo mwaka 2011 ikilinganishwa na mwaka 1990.
Karibu vifo hivyo vyote vilichangiwa na ugonjwa wa Malaria kwa watoto walio chini ya miaka mitano katika nchi za Kusini mwa jangwa la Sahara mwaka jana kwa mujibu wa shirika hilo. Mizozo pia ilichangia huku ugonjwa wa kichomi na tatizo la kuharisha vile vile nayo yakichangia vifo hivyo
Chanzo BBC

Madiwani kikaoni

Madiwani wa Halimashauri ya wilaya ya Bunda wakiwa katika kikao cha baraza hilo kilichoketi leo katika ukumbi wa halimashauri hiyo,picha na Berensi Alikadi.

Tunasikilza hoja za madiwani

WAANDISHI MARA WAMFUKUZA MWENZAO NI KWA KUANDIKA HABARI ZA POLISI.


NA Berensi Alikadi-Musoma

CHAMA cha waandishi wa habari mkoani Mara {MRPC] kimemfukuza uanachama wa chama hicho mwandishi wa habari wa radio Free Afrika mkoani Mara Maxmilian Ngesi baada ya kukiuka makubalino ya chama hicho yaliyofikiwa juzi ya kutoandika kabisa habari za jeshi la polisi mkoani humo.

Akizungumza na gazeti hili jana asubuhi mwenyekiti wa chama hicho Emmanuel Bwimbo alisema kuwa Ngesi amekiuka makubaliano ya waandishi wenzake na chama kwa ujumla baada ya kusikika akitangaza habari za jeshi la polisi kuhusiana na ajari ya kipanya iliyotokea juzi katika kijiji cha Muriaza wilayani Butiama  ambapo alimkariri kamanda wa polisi wa mkoa huo.

Bwimbo amesema kuwa kitendo hicho kinaonyesha jinsi mwandishi huyo alivyokishika chama hicho miguu na kuwa saliti wenzao ambao walikubaliana kwa pamoja juzi katika tamko lao walilotoa ofisini hapo baada ya kuzuiwa wasiandamane kulaani mauaji ya mwenzetu Daudi Mwangosi aliyeuwa na polisi hivi karibuni.

Alisema kuwa yeye kama mwanachama alitakiwa kutii maamuzi ya chama na tamko la chama hilo maana ni tamko ambalo limetamkwa na wananchama na siyo kwa mkoa wa Mara tu lakini pia baadhi ya mikoa imetoa matamko na misimamo hiyo lakini cha kushangaza yeye amekaidi na kwenda kujipendekeza kwa polisi.

‘’Kwakweli huyu mzee ni wa ajabu sisi kama chama tumetoa tamko na vyombo vimetangaza sasa tunashangaa kusikia leo asubuhi anatangaza habari kwa kumkariri RPC sasa kamasi unafiki ni nini mimi naona amezeeka ni bora aache kazi aendelee na kazi yake ya uenezi wa CCM’’alisema Bwimbo.

Alifafanua kuwa kamwe chama hicho hakiwezi kuvumilia mwandishi atakaye kiuka agizo hilo hivyo Ngesi atakuwa mfano kwa waandishi wale ambao wanatakwenda kwenda kujikomba na kuandika habari za polisi hivyo uamuzi pekee wa kumfukuza uanachama ni sahihi kabisa na kwamba chama hicho hakitamrudishia tena uanachama wake.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya wadau wa habari wa mkoa wa Mara na wilaya za Bunda,Tarime na Serengeti wameonyeshwa kusikitisha sana na kitendo cha mwandishi huyo cha kuwasaliti waandishi wenzake ambapo wamedai kuwa mwandishi huyo hafai tena kuwa mwanachama wa chama hicho.

Nao baadhi ya waandishi habari wa mkoa wa Mara wameonyesha kukerwa na tabia ya mwandishi huyo ya kukiuka makubalino na wenzake ambapo wamedai kuwa amewadhalilisha hivyo hawako tayari kufanya kazi naye na kwamba hata kama akipata matatizo hawako tayari kufika kwake.

Juzi waandishi wa habari walifanya maandamano nchi nzima wakilaani mauaji ya mwandishi mwenzao Daudi Mwangosi  ambapo kwa mkoa wa Mara maandamano hayo yaliuzuiwa na polisi hali iliyofanya chama cha waandishi wa habari kukataa kuandika habari za jeshi hilo mkoani Mara.

MWISHO

Wednesday, September 12, 2012

Rais wa Somalia anusurika shambulizi


Rais mpya wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud , amenusurika jaribio la kumuua mjini Mogadishu.

Milipuko miwili imetokea nje la lango la makao ya rais huyo katika hoteli ya Al-Jazeera wakati rais huyo alipokuwa anajiandaa kufanya mkutano na waandishi wa habari.

Taarifa zinasema kuwa waziri wa mambo ya nje wa Kenya Sam Ongeri pia alikuwa katika hoteli hiyo wakati wa shambulizi. Hata hivyo wawili hao wamenusurika. Inaarifiwa watu wanne wameuawa na wengine watatu kujeruhiwa.
Chanzo BBC

Somalia baada ya kuchaguliwa Hassan Sheikh Mohamed kuwa Rais


Rais mpya wa Somalia  Hassan Sheikh Muhamud (katikati)

Matukio ya Afrika

Somalia baada ya kuchaguliwa Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais

Kwa kuzingatia changamoto nyingi zinazobakia nchini Somalia, je Rais Mohamud anatoa matumaini kwa mamilioni ya wakimbizi wa Kisomali hatimaye kuweza kurejea nyumbani? Daniel Gakuba anazungumza na Hussein Bantu, mbunge aliyeko mjini Mogadishu, ambaye pamoja na mengine anaelezea hali ya jumla ilivyo sasa nchini Somalia baada ya kuchaguliwa kwa Rais Mohamud.
(Kusikiliza mazungumzo bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini)
Mwandishi: Daniel Gakuba
Mhariri: Mohammed Khelef
umzo kati ya Daniel Gakuba na Hussein Bantu
Habari hii kwa idhini ya BBC

Tuesday, September 11, 2012

somalia yapata Rais mpya



Rais mpya wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud
Bunge la Somalia limemchagua Hassan Sheikh Mohamud kuwa Rais mpya wa nchi hiyo.
Kulikuwa na wagombea 22 kwenye uchaguzi huo, akiwemo Rais anayeondoka Shariff Sheikh Ahmed na waziri mkuu Abdiweli Mohamed Ali.
Hassan Sheikh Mohamud alishinda kufuatia duru ya tatu ya upigaji kura, ambapo alikuwa anachuana na Rais anayeondoka Shariff Sheikh Ahmed.
Katika raundi ya kwanza Sheikh Ahmed alikuwa amepata ushindi mwembamba wa kura 64 dhidi ya 60 alizopata Sheikh Mohamud.
Kwa jumla wabunge 271 walipiga kura.
Katika duru ya mwisho wabunge wengi waliowaunga mkono wagombea waliochujwa walimuunga mkono Sheikh Mohamud , akapata kura 190 dhidi ya 70 alizopata Rais anayeondoka.
Hii ni mara ya kwanza kwa uchaguzi wa Rais kufanyika katika mji mkuu wa Somalia Mogadishu, tangu kuondolewa kwa serikali ya kijeshi mwaka 1991.
Habari hii kwa idhini ya BBC

Monday, September 10, 2012

Mashushu wavamia wanahabari,wachukuwa picha za marehemu hotelini

Na Waandishi wetu

KUNDI la watu wanaoaminika kuwa maafisa wa Usalama wa Taifa limevamia hoteli kadhaa jijini Dar es Salaam walizofikia viongozi wa klabu za waandishi wa habari kutoka mikoa yote hapa nchini wanaohudhuria mkutano mkuu ambao utatumika kutoa tamko rasmi juu ya mauaji ya mwandishi Daudi Mwangosi aliyeuawa na polisi hivi karibuni.
Habari za kuaminika zimebainisha kuwa zaidi ya maafisa usalama nane walivamia hoteli kadhaa walizofikia waandishi hao, ikidaiwa kusaka kila aina ya taarifa na nyaraka zinazohofiwa kuwa mikononi mwao na ambazo zinaaminika kuwa zitaiumbua serikali ikiwa zitachapishwa katika vyombo vya habari.
Imedaiwa kuwa, hadi sasa maafisa hao wamefanikiwa kunasa lundo la picha za marehemu Mwangosi alizopiga wakati wa uhai wake, zikiwemo zile zinazoonesha matukio yote yaliyotokea kwa siku nzima, kabla na wakati wa vurugu na tukio zima la kupigwa na kuuawa kwake.
Maafisa hao inasemekana wanatafuta pia picha hasa za waandishi wa mikoa ya Iringa na Mbeya ambazo zilipigwa kuonesha jinsi polisi walivyokuwa tayari na kuanza kuwaandama waandishi wa habari watatu ambao inadaiwa kuwa walikuwa walengwa pia wa tukio hilo.
Upelelezi huo unakuja kukiwa na taarifa kwamba, waandishi wa habari walifanikiwa kunasa mazungumzo ya polisi mkoani Iringa yanayoanika waziwazi kile kilichoongelewa na kukubalika kifanyike katika mikutano ya CHADEMA itakayofuata.
Kitu kingine kinachosakwa na maafisa hao ni madai kwamba waandishi wa habari, kutoka mkoani Mbeya na wale wa Mwanza, wanazo nyaraka na vielelezo sahihi vinavyoonesha mauaji yenye utata ya aliyekuwa mtangazaji wa ITV, John Lubungo na mwandishi wa habari wa Mwanza, Richard Masatu ambaye awali alikuwa mwandishi wa habari wa kujitegemea kabla ya kuanzisha gazeti la kasi mpya.
Inasemekana kuwa Masatu siku ya kifo chake alipigiwa simu akiwa anarudi mjini Mwanza kutoka kwenye maonesho ya Nanenane mwaka jana yaliyokuwa yanafanyika mpakani mwa vitongoji vya Igoma na Kisesa, na kukutana na afisa mmoja wa polisi na wa serikali ya wilaya katika baa moja, na baada ya kuachana nao, muda mchache aliokotwa mtaroni eneo la Igoma akiwa mahututi na alifia katika hospitali ya Mkoa ya Sekou Toure.
Maafisa usalama hao, sasa imedaiwa kuwa wanasaka nyaraka za kifo hicho ambacho kama kilivyokuwa kile cha Mwangosi, polisi walitoa ripoti iliyokinzana kwa kiwango kikubwa na ile ya madaktari wa hospitali ya rufaa ya Bugando.
Katika ripoti ya polisi, ilidaiwa kuwa Masatu alikufa baada ya kugongwa na gari, lakini ile ya madaktari inadaiwa kuonesha kuwa alipigwa na kitu kizito kifuani, kutobolewa na kitu chenye ncha kali chini ya kidevu na kutokeza kwa nyuma na kuharibiwa kwa jicho la kushoto.
Aidha, baadhi ya mashuhuda walikiri kutotokea tukio lolote la ajali kama ilivyoelezwa na polisi, kwa vile eneo hilo lina shughuli nyingi za kijamii, na hivyo kama ajali ingetokea ingefahamika kwa wengi.
Maafisa usalama hao, wamegundulika baada ya wanne kati yao, kukutwa katika hoteli kadhaa zilizoko maeneo ya Sinza ambako waandishi wengi wamefikia.
Hata hivyo, mmoja wa maafisa hao alidiriki kujitambulisha akiomba waandishi wasiogope kuwapa kile wanachokijua kwa madai kuwa mauaji ya Mwangosi yamewaumiza hata wao.
Mwanausalama huyo katika hali iliyozidi kuwashangaza baadhi ya waandishi waliokuwepo katika eneo hilo, alidai kuwa wanahabari wasifikiri kuwa serikali imefurahishwa na tukio hilo, ndiyo maana wanalifanyia kazi suala hilo, hivyo ni vizuri waandishi wa habari watulie na waache kuropoka ovyo.
Waandishi wa habari zaidi ya 70 kutoka mikoani wamekutana jijini Dar es Salaam chini ya umoja wao wa klabu za waandishi wa habari hapa nchini (UTPC) katika mkutano wao wa nane ambao pamoja na kufanya uchaguzi wa bodi, utatoa tamko zito lililohusu mauaji ya Mwandishi wa Habari, Daudi Mwangosi yaliyotokea Septemba 2, mwaka huu Nyololo Mkoa wa Iringa kwa kuuawa na polisi.

Habari soma Tanzania daima


juu

Comments System

disqus

Disqus Shortname

msora

Popular Posts

Header Ads

ad